Ijumaa, 27 Rabi' al-awwal 1447 | 2025/09/19
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Hakuna Suluhisho kwa Suala la Sudan Isipokuwa Kutawalisha Uislamu

Tangu uhuru wake mnamo tarehe 1/1/1956, Sudan imeshuhudia mfululizo wa mapinduzi ya kijeshi. Ya kwanza ilikuwa jaribio lililofeli lililoongozwa na Ismail Kabida, ambaye alijaribu kupindua serikali ya kwanza ya kitaifa iliyoongozwa na Ismail al-Azhari. Hii ilifuatiwa na mapinduzi ya kwanza yaliyofaulu yaliyoongozwa na Luteni Jenerali Ibrahim Abboud mnamo Novemba 1958 dhidi ya serikali iliyochaguliwa ya al-Azhari.

Soma zaidi...

Mauaji ya Halaiki ya Sudan: Dori ya Omar al-Bashir

Ingawa mengi yanajulikana kuhusu mauaji ya halaiki yanayowakumba ndugu na dada zetu nchini Palestina, machache sana yanajulikana—au yanasambazwa—kuhusu wale walio nchini Sudan, ambao kwa muda wa miezi 18 iliyopita wamevumilia mauaji ya halaiki ya kimya kimya. Ukatili huo umeua zaidi ya watu 15,000, zaidi ya milioni 10 wamekimbia makazi yao, na kuacha nusu ya watu—watu milioni 25—wakikabili uhaba wa chakula na njaa.

Soma zaidi...

Ubwana Unaofifia: Mpango Mpya wa Mafuta wa Pakistan, Vita vya Kale na Sera ya AI

Mnamo Julai, Rais Trump wa Amerika alichapisha kwenye jukwaa lake la Ukweli wa Jamii. “Hivi punde tumemaliza mkataba na nchi ya Pakistan, ambapo Pakistan na Marekani zitafanya kazi pamoja katika kuendeleza hifadhi yao kubwa ya mafuta.” Mkataba wa mafuta ni sehemu ya mkataba mpana wa kibiashara kati ya nchi hizo mbili, ambapo Marekani imekubali kupunguza ushuru kwa bidhaa za Pakistan kutoka 29% hadi 19%, huku ikitishia kuweka ushuru wa adhabu kwa India, isipokuwa New Delhi imalize uagizaji mafuta ghafi kutoka Urusi.

Soma zaidi...

Waafghani Baina ya Nyundo ya Siasa za Pakistan na Kinoo cha Agenda ya Kikanda

Tangu mwaka wa 2023, serikali ya Pakistan imezidisha uhamishaji wa wakimbizi wa Afghanistan, hatua inayolenga kuishinikiza serikali ya mpito ya Afghanistan inayoongozwa na Taliban jijini Kabul kuwasilisha kikamilifu matakwa ya Amerika. Mawimbi ya Waafghani kuhamishwa kwenda Pakistan yana mizizi ya kihistoria tangu Jihad dhidi ya Muungano wa Kisovieti katika miaka ya 1980, vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyofuata, na uvamizi wa Marekani na kuikalia kijeshi Afghanistan kuanzia 2001 hadi 2021. Pakistan kihistoria imetoa kina cha kimkakati kwa Waislamu wa Afghanistan, shukran kwa mafungamano ya karibu ya kabila yanayovuka Mstari wa Durand.

Soma zaidi...

Mpango wa Mipaka ya Damu na Uhalifu wa Kujitenga kwa Darfur

Baada ya kuanguka kwa kutia shaka kwa miji mikubwa ya Darfur, na kuondolewa kwa jeshi kutoka kwao, mbele ya utekaji nyara wa Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF), pamoja na kuzingirwa kwa nguvu na vikosi hivi katika jimbo la mwisho lililosalia, Darfur Kaskazini na mji mkuu wake, Al-Fashir, wakati jeshi likishindwa kuwafukuza, ghafula yanakuja mazungumzo ya serikali sambamba yakiongozwa nao huko Nyala, mji mkuu wa Darfur Kusini, ambao wanaudhibiti, kwa ushiriki wa vibaraka wa Amerika kama vile Al-Hilu, na uungaji mkono wake kwa serikali hii, hata kuwa naibu ndani yake.

Soma zaidi...

Fahali Wanapopigana, Zinazoumia ni Nyasi “Sudan ni Mfano”

Sijapata katika historia msemo wenye ufasaha zaidi wa uovu wa ukoloni kuliko maneno ya Rabi ibn Amir, Mwenyezi Mungu amuwiye radhi, kwa kamanda wa Kifursi: “Sisi ni watu ambao Mwenyezi Mungu amewatuma kuwatoa wanadamu kutoka katika ibada ya waja wengine hadi kwenye kumwabudu Mola wa waja wote.” Ijapokuwa kauli hii ilitolewa ili kubainisha lengo la ujumbe mtukufu wa Uislamu, unaowakirimu watu kutokana na kumwabudu kwao Mwenyezi Mungu, na kuhifadhi maisha yao, mali zao na heshima zao, hii wakati fulani hujidhihirisha kama kauli iliyo kinyume chake. Rehema ya Uislamu na uhuru unaowadhaminia watu unakinzana na utumwa wa watu na mataifa kwenye ukoloni, ambao unawaona kuwa ni mashini tu za kuzalisha dhahabu na pesa.

Soma zaidi...

Umuhimu wa Kimkakati wa Siasa za Kijiografia za Sudan

Sudan ni nchi yenye umuhimu mkubwa wa kisiasa za kijiografia, unaotokana na ardhi yake kubwa, maliasili nyingi, na eneo ambalo linaiweka kitovu cha baadhi ya njia muhimu zaidi za kibiashara na kisiasa duniani. Licha ya kukabiliwa na miongo kadhaa ya ukosefu wa utulivu wa kisiasa, Sudan inasalia kuwa kitovu cha maslahi kwa dola zenye nguvu za kieneo na kimataifa kutokana na nafasi yake ya kimkakati na uwezo wake ambao haujatumiwa. Umuhimu wake sio wa kisasa tu bali pia wa kihistoria, haswa katika zama ambazo ilikuwa sehemu ya Khilafah kubwa zaidi ya Kiislamu, ambapo ilichukua nafasi muhimu katika kuunganisha na kuimarisha ulimwengu mpana wa Kiislamu. Na umuhimu wake utabaki mbeleni, Khilafah itakaporegea.

Soma zaidi...

Umuhimu wa Kimkakati wa Eneo la Sudan

Aprili 15, 2025 ilitimiza miaka miwili tangu Sudan kukumbwa na vita vya maangamivu vya wenyewe kwa wenyewe, na kusababisha moja ya majanga makubwa zaidi ya kibinadamu duniani leo. Miaka miwili iliyopita mwezi Aprili, mapigano yalizuka kati ya Vikosi vya Wanajeshi wa Sudan (SAF) na Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF), na kuwahamisha mamilioni ya watu, na kuiingiza nchi katika uhaba mkubwa wa chakula, na kuharibu huduma muhimu za afya na elimu. Licha ya maafa ya kibinadamu ambayo yametokea, vita vya Sudan kwa kiasi kikubwa vimeepukana na muanga wa kimataifa. Sudan ni vita iliyosahauliwa, haswa kwa ulimwengu wa Magharibi ambao unaweza kuzingatia Ukraine pekee. Je, ni mambo gani ya siasa za kijiografia ambayo yanaifanya Sudan kushawishika kuyapigania?

Soma zaidi...

Uislamu Uliingiaje Sudan?

Kabla ya kuwasili kwa Uislamu, eneo linalojulikana leo kama Sudan halikuwa umbo lililounganishwa kisiasa, kitamaduni au kidini. Ilikuwa makao ya makabila, desturi, na imani mbalimbali. Upande wa kaskazini, Wanubi walifuata Ukristo wa Kiorthodoksi, na lugha ya Kinubi, pamoja na lahaja zake mbalimbali, ilikuwa njia ya siasa, utamaduni, na mawasiliano. Katika mashariki, makabila ya Beja, vizazi vya Hamu (mwana wa Nuhu), walikuwa na lugha yao wenyewe tofauti, utamaduni, na matendo ya kidini. Upande wa kusini, makabila ya Zanj, yenye sifa na lugha zao za kipekee, yalishikamana na imani za kipagani, na tofauti kama hizo zilikuwepo katika upande wa magharibi.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu