Kuzaliwa kwa Uongofu: Nuru Inayoondoa Giza Lililopo
- Imepeperushwa katika Al-Rayah
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Sayari ya Dunia, na hasa Bara Arabu, lilikuwa likiishi katika giza kuu lililofanya maisha ya binadamu yafanane na kuzimu. Kulikuwa na giza katika nyanja za itikadi, siasa, uchumi, mahusiano ya kijamii, na nyanja zote za maisha. Vita viliwasaga watu bila sababu, wenye nguvu walikuwepo huku wanyonge wakipotea na kutokuwepo, dhulma ilitanda maeneo yote, na utumwa ulifikia viwango vyake vya chini kabisa na vya udhalilishaji kabisa.



