Jumatatu, 25 Rabi' al-thani 1446 | 2024/10/28
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

بسم الله الرحمن الرحيم

Mkutano wa SCO jijini Islamabad:
Siasa za Jiografia ndani ya Kivuli cha Uhasimu wa Marekani na China

Na Abdul Majeed Bhatti

(Imetafsiriwa)

Chini ya ulinzi mkali jijini Islamabad, Mkutano wa 23 wa Shirika la Ushirikiano la Shanghai (SCO) ulianza kwa kishindo cha kawaida. Mkutano huo uliohudhuriwa na dola zenye nguvu kama China, Urusi, India, Pakistan, Iran na baadhi ya jamhuri za Asia ya Kati, ulimalizika kwa kutiwa saini hati nane, zinazohusu bajeti ya shirika hilo, shughuli za sekretarieti ya SCO, na juhudi za kukabiliana na ugaidi katika kanda. Jambo kuu lililoangaziwa lilikuwa ni kuidhinishwa kwa China kama Mwenyekiti kwa kipindi cha 2024-2025 na uthibitisho kwamba Urusi itakuwa mwenyeji1. Kwa mtazamaji asiyefahamu mkutano huo unaonekana kusisitiza matarajio ya SCO kujiweka kama kambi kuu ya siasa za kijiografia. Walakini, nyuma ya matangazo makubwa kuna kitu kidogo.

Kilichoonekana ni kwamba shirika hilo lilishindwa kuchukua msimamo thabiti dhidi ya Magharibi, haswa Amerika na NATO. SCO haikukubali azimio la kuionya ‘Israel’ na Amerika juu ya hatua kali za kulipiza kisasi ikiwa Iran itashambuliwa. Wala wanachama wa SCO hawakuongeza uungaji mkono wa dhati kwa vita vya Urusi dhidi ya Ukraine inayoungwa mkono na NATO. Pengine, jambo la kuvunja moyo zaidi kuliko yote lilikuwa ushirikiano wowote wa maana uliotolewa kwa China ili kukabiliana na mkusanyiko wa kijeshi unaotisha wa Amerika katika Ukingo wa Pasifiki. Moscow na Beijing zilitarajia kwa muda mrefu kuwa SCO siku moja itashindana na NATO2 na kurudisha nyuma “agizo lenye msingi wa utawala” la Magharibi, lakini huenda wakasubiri kwa muda usiojulikana. Ukosefu wa umoja kati ya nchi wanachama ulitumika kama taswira ya ushindani unaozidi kudhoofisha uwezo wa SCO kushawishi siasa za kikanda lakini kwa kiasi kikubwa kudhoofisha nafasi ya China ya kushinda ushindani na mwenza Marekani kudhibiti ulimwengu.

China inatazamia mashirika kama SCO na BRICs kuisaidia kupinga utawala wa Marekani huko Eurasia. SCO ni sehemu muhimu ya Mpango mpana wa Beijing wa ‘Belt and Road Initiative (BRI)’, unaolenga kupanua ushawishi kupitia miradi ya miundombinu kote Eurasia. Walakini, kwa Urusi hili ni tatizo. Moscow inatazama uingiaji wa BRI katika duara lake la jadi la ushawishi-dola za Asia ya Kati. Licha ya uhusiano wa karibu kati ya Moscow na China-kutokana na mbinu kali za Marekani za kuitumia Ukraine kama ngome dhidi ya Urusi na juhudi kubwa za Marekani za kuizingira China-kutoaminiana kati ya majirani hao wawili kulikokita mizizi katika Uasi wa Boxer wa 1899 ni vigumu kumaliza.

Halafu kuna ugomvi wa hivi majuzi zaidi wa China na India ambao unazunguka eneo la Himalaya, Bahari Hindi, Ukingo wa Pasifiki na anga. Mbali na dola kubwa, uadui kati ya India na Pakistan umesababisha vita vinne, mapigano ya mpaka kati ya Iran na Pakistan yanaongezeka na mzozo wa mara kwa mara wa mpaka kati ya Kyrgyzstan na Tajikistan unaendelea kuhujumu malengo ya juu yaliyowekwa na SCO. Zaidi ya hayo, shirika limegawanywa na mahesabu ya mizani ya mamlaka. Kyrgyzstan na Tajikistan zinashindana ili kuimarisha mafungamano na Urusi kwa gharama ya kila mmoja. China inataka kuimarisha Pakistan kupitia CPEC na silaha za kijeshi, wakati India inafuatilia upanuzi wa uhusiano na Iran na Urusi ili kukabiliana na hatari ya Pakistan. Zaidi ya hayo, kukosekana kwa usawa mkubwa wa kibiashara kati ya uchumi wa China na nchi zingine wanachama huzua malalamiko ya ndani dhidi ya uagizaji wa bei nafuu kutoka China. Kutokana na hayo, SCO inakabiliwa na mvunjiko wa kiusalama na kiuchumi lakini kinachotishia kufichua shirika zima ni uhusiano wa kimkakati wa India pamoja na Amerika na Ulaya.

Licha ya juhudi bora zaidi za China, SCO kama BRICs haiwezi kuleta changamoto kubwa kwa ukuu wa Amerika katika eneo hilo na kuwa kama mzani wa NATO. Kivuli cha Amerika kinaning'inia sana juu ya SCO na kupitia India na Pakistan, Marekani inaweza kudhoofisha zaidi SCO. Kwa hiyo, matarajio ya China ya kuiondoa Eurasia kutoka kwa utawala wa Marekani yamepata upinzani mkubwa.

Kinachosikitisha zaidi ni kwamba kati ya nchi kumi wanachama, sita ni nchi za Waislamu huku India na China zikiwa na idadi kubwa ya Waislamu. Kwa hivyo, swali linazuka kwa nini Waislamu wanatamani usalama na ustawi katika shirika linalotawaliwa na China na mshirika wake mdogo Urusi. Wote wawili ni maadui wakubwa wa Ummah. Ukaliaji wa kikatili wa Afghanistan na kufutwa kwa Grozny na Urusi, na unyanyasaji wa kikatili wa Wauighur ni uhalifu usiofutika ambao hauwezi kusamehewa au kufuta kumbukumbu zetu. Mbali na hilo, dola zote mbili ni viongozi wasiostahili. Haziweza hata kukusanya azimio la pamoja la kisiasa la kutumia aibu ya kimataifa ya Amerika na janga la kimaadili juu ya Gaza na kuchukua nafasi ya mfumo mbovu wa utawala.

Iwapo Waislamu watatazama historia yao tajiri, watagundua kwamba zama tukufu zaidi za mafanikio ya kiuchumi na usalama katika eneo la SCO zilikuwa chini ya utawala wa Kiislamu. Khilafah Rashida, Khilafah Umawiyya, Khilafah Abbasiyya na baadaye usultani wa Seljuk, na usultani wa Timuriy ni mifano ya mitandao ya kibiashara iliyostawi, maendeleo ya kisayansi, na utulivu wa kisiasa. Zama hizi za ukuaji chini ya utawala wa Kiislamu zinasimama kinyume na mivutano ya leo inayowakabili wanachama wa SCO, ambao wengi wao wanatatizika na kuyumba kisiasa na kiuchumi, kwa sababu ya kujifungamanisha na dola makubwa.

Waislamu wa eneo la SCO ni lazima waregee katika Uislamu kwa ajili ya masuluhisho yao yote, la sivyo wataendelea kupata udhalilifu na fedheha chini ya kutawaliwa na dola kubwa. Mwenyezi Mungu (swt) asema:

[وَمَن يَبْتَغِ غَيْرَ الإِسْلاَمِ دِينًا فَلَن يُقْبَلَ مِنْهُ وَهُوَ فِي الآخِرَةِ مِنَ الْخَاسِرِينَ]

“Na anaye tafuta dini isiyo kuwa Uislamu haitakubaliwa kwake. Naye Akhera atakuwa katika wenye kukhasirika.” [Aal-i Imran: 85]. Wokovu pekee ni katika ufufuo wa Khilafah Rashida kwa njia ya Utume.

Maregeleo

[1] Gazeti la ‘Pakistan Tribune’, (Oktoba 2024). Mkutano wa SCO: Mwanachama watia Saini makubalinao manene, kuidhinisha China kama mwenyekiti wa Kipindi cha 2024-2025: gazeti hilo la ‘Pakistan Tribune linapatikana katika:

https://tribune.com.pk/story/2503156/sco-summit-kicks-off-pm-shehbaz-sharif-delivers-keynote-speech

[2] Taasisi ya Amani ya Marekani, (Julai 2024). China, Urusi Zaiona SCO kama Mzani wa NATO lakini India haina hakika. Inapatikana katika:

https://www.usip.org/publications/2024/07/china-russia-see-sco-counterweight-nato-india-ambivalent

Yaliyomo ndani ya kifungu hichi: « Wakenya Amkeni

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

rudi juu

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu