Jumamosi, 12 Sha'aban 1447 | 2026/01/31
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Hizb ut Tahrir / Tanzania Yafanya Semina kwa Mnasaba wa Kumbukumbu ya Miaka 105 ya Kuvunjwa kwa Khilafah

Katika kumbukumbu ya miaka 105 ya kuvunjwa kwa Dola ya Khilafah iliyotokea mnamo Rajab 1342 H / Machi 1924 M, jana, Jumapili, 29 Rajab 1447 H / 18 Januari 2026 m, Hizb ut Tahrir / Tanzania ilifanya semina fupi katika Masjid Taqwa, Ilala Bungoni katika jiji la Dar es Salaam.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Amerika: Kongamano la Khilafah 2026 “Kutoka Mgawanyiko hadi Umoja”

Hizb ut Tahrir Amerika ilifanikiwa kufanya kongamano lake la kila mwaka kwa mwaka huu 1447 H (2026 M), kama sehemu ya kampeni ya kimataifa iliyoandaliwa na Hizb ut Tahrir kwa mnasaba wa kumbukumbu ya kuvunjwa kwa Khilafah mnamo tarehe 28 Rajab, 1342 H. Kongamano hilo lilitumika kama wito kwa Waislamu kote duniani kutambua na kutimiza wajibu wao wa kuregesha mfumo kamili wa maisha wa Kiislamu kwa kusimamisha Khilafah kwa njia ya Mtume wetu Muhammad (saw).

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Lebanon: Kongamano la Khilafah la kila Mwaka “Kuhalalisha Mahusiano na Kujisalimisha au Ahadi ya Mwenyezi Mungu na Dola ya Kiislamu?!”

Hizb ut Tahrir / Wilayah Lebanon yaandaa kongamano lake la kila mwaka kwa kichwa: “Kuhalalisha Mahusiano na Kujisalimisha au Ahadi ya Mwenyezi Mungu na Dola ya Kiislamu?!” Kwa mnasaba wa kumbukumbu uchungu ya miaka 105 ya kuvunjwa kwa dola ya Khilafah mnamo 28 Rajab 1342 H sawia na 3 Machi 1924 M

Soma zaidi...

Katika Kumbukumbu ya Miaka 105 ya Kuvunjwa kwa Khilafah... Dunia Inajitayarisha Kurudi Kwake

Mtu anaweza kufikiri, huku akiangalia yanayojiri hivi karibuni katika ngazi ya kimataifa na katika ardhi za Kiislamu, kwamba uhalisia unazidi kuwa wa giza tororo kwa Umma wa Kiislamu, na kwamba matumaini ya kuamka kwake na kuregeshwa kwa heshima yake yanafifia au kupungua. Hata hivyo, kutafakari haya yanayojiri kunaonyesha kwamba yanafichua matumaini ambayo yanajajidishwa na kuzidi kuwa makubwa, na mbinu ya kuelekea mwamko siku baada ya siku.

Soma zaidi...

Hotuba ya Mwanachuoni na Amiri wa Hizb ut Tahrir Ata Bin Khalil Abu Al-Rashtah (Mwenyezi Mungu amlinde) Katika Kumbukumbu ya Miaka 105 ya Kuvunjwa kwa Khilafah

Katika siku hizi kama hizi, miaka 105 iliyopita, mwishoni mwa Rajab 1342 H, sambamba na mapema Machi 1924 M, wakoloni makafiri, wakiongozwa na Uingereza wakati huo, kwa ushirikiano na wasaliti wa Kiarabu na Kituruki, waliweza kuivunja Khilafah. Mhalifu wa zama hizo, Mustafa Kemal, alitangaza ukafiri wa wazi kwa kuifuta Khilafah, kumzingira Khalifa jijini Istanbul, na kumfukuza alfajiri siku hiyo hiyo. Hivyo, tetemeko baya la ardhi lilizikumba ardhi za Waislamu kwa kuvunjwa Khilafah, chimbuko la izza yao na radhi ya Mola wao Mlezi.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu