Umebarikiwa kwa Nguvu, Umedhoofishwa na Mgawanyiko
- Imepeperushwa katika Habari na Maoni
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
"Pentagon yasema Marekani haitaki kuanzisha vita na Iran" - hii, baada ya kudondosha mabomu kumi na nne aina ya bunker-buster kwenye vituo vitatu vya nyuklia ndani ya ardhi ya Iran. Kauli kama hiyo si ya kinafiki tu - ni ya kuchukiza. Inaakisi mawazo ya kiburi, ya kikoloni. Mtu yeyote mwenye akili timamu anawezaje kuamini kwamba vita sio nia pindi taifa linapofanya mashambulizi yaliyoratibiwa kwa taifa jengine?