Huku Ramadhan Ikikaribia Gaza Inaendelea Kufa Njaa
- Imepeperushwa katika Habari na Maoni
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Kulingana na Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa, wakaazi wote wa Gaza milioni 2.3 kwa sasa wameainishwa kama wanakabiliwa na mgogoro, dharura, au viwango vya janga vya uhaba wa chakula. Picha zimesambazwa kwenye mitandao ya kijamii zikionyesha watu, haswa kaskazini mwa Gaza, wakila nyasi, magugu na malisho ya wanyama.