Jumatano, 04 Rabi' al-awwal 1447 | 2025/08/27
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Iwapo Kuanguka kwa ‘Jamhuri’ Hakukupelekea Kusimamishwa kwa Khilafah, Ni lazima Kutumike kama Hatua ya Mpito kuelekea Khilafah Rashida

Kuporomoka kwa serikali ya Jamhuri nchini Afghanistan ni moja ya matukio muhimu zaidi kwa watu wa Afghanistan na Umma mpana wa Kiislamu katika karne ya 21. Serikali hii sio tu kwamba haikuwa na mizizi yoyote katika itikadi ya Kiislamu, bali ilikuwa ni zao la muundo wa ukoloni mamboleo - mfumo ulioagizwa kutoka nje uliojengwa ili kurasimisha ufisadi, utegemezi, na dhulma. Kuanguka kwake lilikuwa ni mwisho wa kimaumbile na usioepukika wa mfumo ambao, tangu kuanzishwa kwake, ulikuwa ngeni kwa kitambulisho cha Kiislamu na kupingana na maadili ya Uislamu.

Soma zaidi...

Kauli za Netanyahu kuhusu "Israel Kubwa" ni Tangazo la Vita ambalo linafuta Mikataba, na, kwa sababu hiyo, Majeshi Yanasonge, na Jambo jengine lolote lisokuwa hilo ni Usaliti

Huyu hapa mhalifu wa kivita Netanyahu anatangaza waziwazi na bila kufasiriwa kwa watawala waoga wa Kiarabu na wasemaji wao, akisema katika mahojiano na chaneli ya Kiebrania i24: “Mimi niko kwenye misheni ya vizazi na kwa jukumu la kihistoria na la kiroho, ninaamini kwa dhati ruwaza ya Israel Kubwa, ambayo ni pamoja na Palestina ya kihistoria na sehemu za Jordan na Misri.” Mhalifu Smotrich alikuwa amemtangulia kwa kauli zile zile na kunyakua sehemu za nchi za Kiarabu zinazoizunguka Palestina, ikiwemo Jordan. Katika muktadha huo huo, adui namba moja wa Uislamu na Waislamu, Rais Trump wa Marekani, alimpa idhini ya upanuzi wake akisema, “Israel ni sehemu ndogo sana ikilinganishwa na ukubwa wa ardhi hizo, na najiuliza ikiwa inaweza kupata ardhi zaidi kwa sababu kweli ni ndogo sana.”

Soma zaidi...

Msako Mkali wa Amerika dhidi ya Mashirika ya Kiislamu

Katika mahojiano ya hivi majuzi na mtangazaji wa redio Sid Rosenberg, Katibu wa Waziri wa Mambo ya Nje Marco Rubio alionyesha mchakato unaoendelea wa kuiorodhesha Ikhwan al-Muslimin na CAIR kama mashirika ya kigaidi. Waziri Rubio alisema kwamba uorodheshaji kama huo ulikuwa "katika kazi zao, na ni wazi kuna matawi tofauti tofauti ya Ikhwan al-Muslimin, kwa hivyo itabidi uliorodheshe kila moja yao."

Soma zaidi...

Kauli za Netanyahu baina ya Uhalisia wa Umbile lake na Msimamo Unaofifia wa Serikali ya Misri

Kauli za Waziri Mkuu wa umbile la Kiyahudi, Benjamin Netanyahu, ambazo alizungumza moja kwa moja kuhusu kile kiitwacho “Israel Kubwa zaidi” na kuhusu mipango ya uhamishaji na upanuzi, zinafichua kwa mara nyengine tena itikadi iliyokita mizizi ndani ya nyoyo za viongozi wa umbile hili; itikadi ya khiyana, usaliti, na ulafi wa ardhi ya Waislamu. Matamshi haya si kuteleza kwa ulimi, bali ni tafsiri ya kivitendo ya mipango iliyoandikwa katika fikra ya kisiasa ya Kizayuni, na mipango inayotekelezwa uwanjani hatua kwa hatua.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan: Mwaliko wa Kuhudhuria Mkutano na Waandishi wa Habari

Sisi, katika Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan, tuna furaha kuwaalika ndugu zetu katika vyombo vya habari, wanasiasa, na wale wenye hamu na mambo ya umma kuhudhuria kwenye mkutano na waandishi wa habari, ambapo msemaji rasmi wa Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan atatoa hotuba kwa anwani: "Wito kwa Watu wa Sudan: Ikamateni Darfur ili Isijiunge na Kusin"

Soma zaidi...

Kuundwa kwa cheo cha "Mufti Muongofu" katika Zama za Akili Bandia Kuunda Sheria Inayoafikiana na Magharibi na Watawala wake Vibaraka

Katikati ya mporomoko wa kisiasa na kifikra wa Umma wa Kiislamu, na wakati ambapo njama dhidi ya dini yake na hukmu zake zikiongezeka, serikali tawala na zana zao - taasisi rasmi za kidini - zinazindua makongamano yenye kauli mbiu za kustaajabisha na misamiati ya uchochezi ya kiteknolojia, wakikopesha mradi wao wa kupotosha kuwa dini ni kero kwa “usasa” na “maendeleo”. Hii ni pamoja na kongamano la "Kuunda cheo cha Mufti Sahihi Katika Zama za Akili Bandia,” lililoandaliwa na Dar al-Ifta ya Misri chini ya udhamini wa moja kwa moja wa Rais Abdel Fattah el-Sisi.

Soma zaidi...

“Siku ya Uhuru” ya 78 Pakistan Itakuwa Huru Kupitia Kuanzishwa kwa Khilafah Rashida

Chini ya mfumo wa sasa wa kimataifa, kile kinachoitwa uhuru si kitu zaidi ya usanii wa mchezo wa kuigiza, kwan maana ukombozi wa kweli (tahrir) uko pale tu dola inapoweza kupanga mambo yake ya ndani na mahusiano ya nje kwa mujibu wa itikadi yake. Watu wanaoamini “La ilaha illa Allah Muhammadur RasulAllah” kamwe hawatakombolewa kikweli mpaka watabikishe katika ardhi yao mfumo wa Kiislamu wa utawala, uchumi, jamii, elimu, na mahakama, pamoja na sera ya kigeni yenye msingi wa Da‘wah na Jihad. Hii ndiyo maana halisi ya uhuru, na katika suala hili, Pakistan bado haijakombolewa!

Soma zaidi...

Tanzia ya Anas Al-Sharif na Wenzake

Jioni ya Jumapili, 10 Agosti 2025, hema dogo la vyombo vya habari mbele ya Hospitali ya Al-Shifa Medical Complex katika Mji wa Gaza liliharibiwa kabisa na shambulizi la moja kwa moja kutoka kwa umbile la Kizayuni, na kuua waandishi wa habari watano waliokuwa wakinakili mauaji ya halaiki yanayoendelea huko Gaza. Miongoni mwa waliouawa shahidi walikuwa wanahabari Anas Al-Sharif, Mohammad Qreiqeh, na wapiga picha Ibrahim Zaher, Moamen Aliwa, na Mohammad Noufal. Mwenyezi Mungu (swt) awakubalie miongoni mwa Mitume, wakweli, mashahidi na watu wema – ni maswahaba wema walioje.

Soma zaidi...

Mkataba wa Gesi na Umbile la Kiyahudi Ununuzi wa Utajiri wetu ulioibiwa na Msaada kwa Adui yetu Mnyakuzi

Katika kitendo kipya kinachojumuisha kiwango cha mporomoko na ubaraka ambao utawala wa Misri umefikia, ilitangaza kusainiwa kwa makubaliano makubwa na umbile la Kiyahudi ya kuagiza gesi asilia kutoka kwa uwanja wa Leviathan katika ardhi iliyonyakuliwa ya Palestina, kwa thamani inayokaribia dolari bilioni 35 hadi mwaka wa 2040. Chini yake, umbile la Kiyahudi linauza nje ya nchi karibu mita za ujazo 130 za gesi nchini Misiri, kutumika kukidhi mahitaji ya ndani na kusafirisha nje kupitia vituo vya kutengeneza gesi vya Misri. Makubaliano haya yamepigiwa debe kama "kuimarisha usalama wa nishati," huku kiuhalisia yakiwa ni usaliti kwa Ummah, kupuuza utajiri wake, muungano na adui yake, na msaada kwa uchumi wake unaodhoofika.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu