Alhamisi, 05 Rabi' al-awwal 1447 | 2025/08/28
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Yaandaa Kisimamo Mbele ya Msikiti Mkongwe jijini Port Sudan cha Kuinusuru Gaza

Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan imeandaa kisimamo mbele ya Msikiti Mkongwe jijini Port Sudan leo, Ijumaa, 7 Safar 1447 H sawia na tarehe 1 Agosti 2025 M, baada ya swala ya Ijumaa. Wanachama wa Hizb waliinua mabango yenye alama ishara: “Angusheni viti vya utawala vinavyozuia kusonga kwa majeshi kuinusuru Gaza.”

Soma zaidi...

Hotuba Iliyotolewa na Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilaya ya Sudan Mbele ya Msikiti Mkongwe jijini Port Sudan mnamo Ijumaa tarehe 1/8/2025 M

Je, hili linaweza kuwaziwa kutoka kwenu?! Vipi mnaweza kula, kunywa na kulala na hali ndugu zenu mjini Gaza wanauawa, wanahamishwa na kuwekwa njaa na Mayahudi wanaokalia kimabavu eneo la Isra ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw)?! Dhambi liko juu ya shingo zetu sote ikiwa hatutawanusuru ndugu na dada zetu wa Gaza. Hatutaweza kuwanusuru isipokuwa majeshi ya Umma yasonge, kwani wao ni watoto wenu na ndugu zenu, na hakuna kitakachowaondoa Mayahudi isipokuwa dola ya Waislamu; Khilafah.

Soma zaidi...

Magereza ya Misri: Kati ya Mateso na Mauaji Pindi Heshima Inapokanyagwa Haki Huuawa!

Katika tukio jengine la mara kwa mara la uhalifu uliofichwa, kijana mmoja aitwaye Ayman Sabry alikufa ndani ya kituo cha polisi katika Jimbo la Dakahlia kutokana na mateso ya kikatili, ambayo yaliacha alama wazi kwenye mwili wake. Chini ya masaa 48 baadaye, kijana mwengine alikufa ndani ya Kituo cha Polisi cha Al-Saff katika Jimbo la Giza, huku kukiwa na ripoti thabiti za kutelekezwa kimakusudi, dhulma, na ukatili, na kuvigeuza vituo vya polisi kuwa sehemu za vifo cha polepole.

Soma zaidi...

Yeyote Anayezuia Mkate Usifike Gaza Hapaswi Kuzungumzia kuhusu Utu, Ewe Waziri wa Mambo ya Nje Rafah: Imo ndani ya Tundu la Uvamizi... au imo Ndani Mshiko wa Serikali ya Misri?!

Katika mandhari ambayo hakuna jicho linaloweza kukosa kuiona, watoto wa Gaza wanasimama kwenye vifusi vya nyumba zao, wakikimbilia tama la maji, kipande cha mkate, au dozi ya dawa, wakati Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri anajitokeza mbele yetu akizungumzia "nia ovu" na "heshima ya sera ya kigeni," katika jaribio la kuiondolea serikali ya Misri dori yake halisi katika mzingiro wenye kunyonga pumzi uliolazimishwa juu ya Ukanda wa Gaza.

Soma zaidi...

Ni Lazima ikumbukwe kwamba Marekani ni Nchi ya Kikoloni; Kujisalimisha kwa Sera zake za Ushuru Kutahatarisha Ubwana wa Taifa!

Marekani, mchuuzi wa kimataifa wa ubepari, imeibua 'dhoruba ya ushuru' duniani kote, ikipuuza kanuni za uchumi wa soko huria – moja ya falsafa kuu za ubepari – na sheria na kanuni za kile kinachojulikana kama Shirika la Biashara Duniani (WTO) ililounda. Hii, kwa mara nyingine, inathibitisha kwamba mfumo wa kibepari hauna utu na wa kinyonyaji. Serikali ya mpito ya Bangladesh imetabanni sera ya utiifu katika kukabiliana na hatua za ushuru za Marekani. Tayari wamefanya uamuzi wa kujitoa mhanga kununua ndege 25 za gharama kubwa aina ya Boeing, pamoja na kuagiza pamba na LNG kutoka Marekani, ingawa nchi nyingi zinaghairi oda zao kutokana na utendakazi duni wa Boeing. Na wanafanya mikutano ya moja kwa moja na Marekani, wakiweka umma katika giza kupitia 'makubaliano fiche ya kihistoria' (NDA).

Soma zaidi...

Serikali ya Muungano Msingi ni Hatua ya Juu katika Kuharakisha Mpango wa Amerika wa Kutenganisha Darfur

Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF), kupitia muungano wao unaoitwa Muungano Msingi wa Sudan "Ta'sis," ulitangaza mnamo Jumamosi, 26/7/2025, uteuzi wa Rais na Makamu wa Rais wa Baraza la Rais, na Waziri Mkuu, ambayo ina maanisha kuundwa kwa serikali sambamba katika mamlaka inayoendeshwa na jeshi kutoka mji wa Port Sudan, mashariki mwa nchi.

Soma zaidi...

Pindi Milango Inapofungiwa wenye Njaa na Kunusuriwa Kukanyimwa, Sura Hasiri ya Serikali ya Misri na Wapambe wake Inafichuliwa

Katika wakati ambapo Gaza inastahamili moja ya nyakati kandamizi na za kikatili zaidi katika historia, ambapo, pamoja na kuuawa kwa mashambulizi ya mabomu, watoto wanakufa kwa njaa, wanawake kwa huzuni, na wazee kwa magonjwa, Meja Jenerali Khaled Mewaghar, Gavana wa Sinai Kaskazini, alitoa matamshi ambayo yanakinzana na matakwa rahisi zaidi ya  maadili ya kiakhlaki na ya kibinadamu matakwa ya udugu wa Kiislamu. Alisema: “Ikiwa watu wa Gaza watafikia kiwango fulani cha njaa, wana chaguzi tatu: ima kwenda upande wa Israel na kukabili milio ya risasi, kujitupa baharini, au kuelekea Misri—jambo ambalo haliwezekani.”

Soma zaidi...

Kuzingirwa kwa Gaza ni Ushahidi wa Khiyana ya Serikali ya Misri

Gaza imeingia katika awamu ya tano njaa (awamu ya janga la njaa), kulingana na ripoti ya Umoja wa Mataifa. Huku Waislamu kila mahali wakijaribu kuwanusuru ndugu zao kwa michango na kuanzisha misafara ya kuvunja mzingiro dhidi yao, nchi jirani zinatazama bila harakati yoyote—mbele yao zaidi ni Misri, ambayo ina mpaka na Gaza, lakini inadai kuwa haina usemi katika suala hilo na imeridhia kuchukua dori ya mpatanishi. Hivyo, je, kweli Misri haina uwezo wa kuwanusuru watu wa Gaza?!

Soma zaidi...

Mkasa wa Milestone: Watoto Wasio na Hatia na Rubani wetu Jasiri Tauqir, walikuwa Waathiriwa wa Ukatili wa Kukosekana kwa Dola yenye kujali inayowachunga Watu

Jumatatu iliyopita (21 Julai, 2025) alasiri, ndege ya kivita ya Jeshi la Anga la Bangladesh F-7 BGI iligonga jengo katika sehemu ya chini ya Shule ya Milestone na Chuo katika eneo la Uttara katika Mji Mkuu kutokana na hitilafu ya kiufundi. Hii ilisababisha hali ya kusikitisha na ya kuhuzunisha kwa matukio ya kutisha ya watoto walioungua na kukatwa viungo na vijana waliouawa na kujeruhiwa. Sisi katika Hizb ut Tahrir, tunamuomba Mwenyezi Mungu (swt) msamaha kwa marehemu hao, na tunawaombea nafuu ya haraka waliojeruhiwa. Na tunamuomba Mwenyezi Mungu (swt) awajaalie wahasiriwa hadhi ya mashahidi Peponi kwa mujibu wa bishara njema ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw).

Soma zaidi...

Serikali ya “Matumaini” Yageuka Jinamizi kwa Wananchi kwa Kuporomoka kwa Pauni ya Sudan!

Katika hotuba yake baada ya kula kiapo cha kuwa Waziri Mkuu, Kamil Idris alisema: “Kauli mbiu yetu ni matumaini, na dhamira yetu ni kufikia usalama, ustawi, na maisha ya utulivu kwa kila raia wa Sudan!” Katika taarifa yake ya kwanza kwa vyombo vya habari, alitangaza kuwa atatoa muda na juhudi zake kuhakikisha maisha ya heshima kwa kila Msudan.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu