Jumatatu, 13 Jumada al-awwal 1447 | 2025/11/03
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Na anaye fedheheshwa na Mwenyezi Mungu hana wa kumhishimu. [Al-Hajj: 18]

Baada ya maafikiano yote yaliyofanywa na PLO, ambayo yalifikia uhaini mkubwa kwa kuitoa sehemu kubwa ya Palestina. Na baada ya kukubalika kwake kuwa chombo cha usalama (katika muundo wa mamlaka) kinachowapiga vita watu wa Palestina, kupokonya silaha kambi za ndani ya Palestina kwa kuua, kuzingira na kukamata, na nje ya Palestina kwa uratibu na serikali za Syria na Lebanon, ili kuzuia tishio lolote, kubwa au dogo, kwa usalama wa Mayahudi ndani au karibu na Palestina.

Soma zaidi...

Huku Amerika Ikiunga Mkono Mauaji ya Halaiki mjini Gaza, Inaingia Uzbekistan Kama Mshirika wa Usalama!

Mnamo tarehe 28/8/2025, Rais Shavkat Mirziyoyev alimpokea Mjumbe Maalum wa Rais wa Marekani wa Ushirikiano wa Kimataifa, Paolo Zampoli. Kulingana na taarifa kwa vyombo vya habari kutoka Huduma ya Habari ya Rais, “Mkutano huo ulijadili ushirikiano wa kimkakati kati ya Uzbekistan na Marekani na upanuzi wa ushirikiano wa pande nyingi.”

Soma zaidi...

Kinachoitwa “Tamasha za Hisia” (Zambo) jijini Tripoli ni Jaribio la Kulionyesha Jiji lisilo na Hisia zake kwa Ummah Kwa hivyo Zisusieni na Komesheni utoaji Leseni Kwazo!

Kwa ukaidi wa wazi wa hisia za Umma na maumivu yake, na kwa ukaidi wa wazi wa Tripoli, jiji la elimu na wanazuoni, na licha ya kutolewa kwa tamko kutoka kwa Kamati ya Utunzaji wa Familia katika Dar al-Fatwa jijini Tripoli na Kaskazini kuonya juu ya njia hii hatari kwa jamii, ambapo ilikuja katika taarifa: “Kamati pia inatahadharisha juu ya hatari ya tamasha, sherehe, filamu, na mipango ambayo imejitokeza hivi karibuni katika jiji letu na ambayo yanaathiri maadili na akhlaki, na ambayo hutumiwa kupitisha ujumbe potovu chini ya kauli mbiu za kisanii au kithaqafa, katika jiji linalojulikana katika historia yake kama jiji la elimu na wanazuoni, na kama ngome ya maadili ya kweli na kitambulisho kinachounganisha. Kamati inasisitiza kwamba kuilinda jamii kutokana na hatari ni jukumu tunaloshirikiana pamoja: linaanza na familia na jamaa, kwenda hadi kwa walimu, na wanazuoni, na pia linajumuisha asasi za kiraia, manispaa, na wanasiasa, kufikia hadi kwa watoa maamuzi katika ngazi ya serikali…”

Soma zaidi...

Mvua ni Baraka na Rehema, lakini bila Uchungaji imekuwa ni Laana!

Ni huzuni na pia inasikitisha kwamba msimu wa mvua hauji kwa ghafla, bali ni kipindi cha taarifa ambacho hurudiwa kila mwaka. Kinachoshangaza zaidi ni kwamba vituo vingi vya uchunguzi wa hali ya hewa vilionya kuhusu mvua kubwa, lakini asasi za serikali hazikuchukua hatua yoyote kuzuia madhara yake, ambayo yalikuwa mabaya zaidi kwa vijiji vya Jimbo la Mto Nile, mashariki mwa Sudan na hata Kordofan, miongoni mwa kwengine.

Soma zaidi...

Wilaya ya Al-Arish Mina, Warraq Mpya Kuwahamisha Wakaazi wake: Uwekezaji wa Lazima au Uhalifu wa Uhamishaji?

Siku hizi, mji wa Al-Arish unashuhudia sura mpya ya mateso wanayopata wananchi wa Misri mikononi mwa utawala unaowaona watu kuwa kikwazo tu kwa mipango yake ya uwekezaji na miradi yenye faida. Baada ya kimya cha miaka mingi na ahadi za uwongo kwamba wakaazi wa wilaya ya Mina kwamba hawatadhurika, watu walishangazwa kukuta matingatinga ya serikali yakiregea kubomoa nyumba na kung’oa wakao yao, bila kujali utakatifu wa nyumba, utu, au haki za watu, ambazo Mwenyezi Mungu (swt) amewapa katika ardhi na mali zao.

Soma zaidi...

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Wanamtembelea Mkuu wa Chama cha Democratic Unionist mjini Al-Obeid

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan, ukiongozwa na Ustadh Al-Nazir Muhammad Hussein - Mjumbe wa Baraza la Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Sudan - akifuatana na Ustadh Issam al-Din Abdul Qadir, walimtembelea Ustadh Khalid Hussein, Mkuu wa Chama cha Democratic Unionist, katika afisi yake katika mji wa Al-Obeid, mnamo Jumanne 3 Rabi’ al-Awwal sawia na tarehe 26 Agosti 2025 M, kama sehemu ya kampeni iliyoandaliwa na Hizb ili kutibua mpango wa kuitenganisha Darfur.

Soma zaidi...

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Waitembelea Idara ya Muongozo na Ushauri katika Jimbo la White Nile

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan – Mji wa Rabak, White Nile, uliitembelea Idara ya Muongozo na Ushauri mnamo Jumapili, 1 Rabi' al-Awwal 1447 H sawia na tarehe 24 Agosti 2025. Ujumbe huo ulikutana na mkuu wa Sekretarieti katika Jimbo la White Nile, Sheikh Abdul Mubara Mahmoud Al-Mahmoud. Ujumbe huo uliongozwa na Dkt. Ahmed Muhammad Fadl Al-Sayyid, mwanachama wa Hizb ut Tahrir, na alifuatana na Ustadh Faisal Madani, mwanachama wa Hizb ut Tahrir.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu