Ijumaa, 28 Dhu al-Qi'dah 1447 | 2026/05/15
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Ziara ya Asim Munir jijini Cairo ni Hatua ya Kutekeleza Ruwaza ya Trump kwa Mashariki ya Kati

Katika utekelezaji wa ruwaza ya Trump kwa Mashariki ya Kati, ambayo inatazamia kupandishwa cheo kwa umbile la Kiyahudi ndani ya ulimwengu wa Kiislamu baada ya usawazishwaji mahusiano, na kujumuishwa kwa serikali zote zilizopo katika ulimwengu wa Kiislamu ndani ya kile kinachoitwa ruwaza ya Mikataba ya Abraham, uhusiano wa hivi karibuni kati ya vibaraka wa Amerika katika ulimwengu wa Kiislamu umefanyika, kwa lengo la kutimiza ndoto za Trump katika eneo hilo.

Soma zaidi...

Kumwalika Adui wa Mwenyezi Mungu, Mtume Wake, na Waumini Ni Sawa na Kualika Ghadhabu ya Mwenyezi Mungu na Msiba: Mche Mwenyezi Mungu, Ewe Waziri Mkuu wa Malaysia!

Hizb ut Tahrir / Malaysia inalaani vikali mwaliko uliotolewa na Waziri Mkuu wa Malaysia, Dato’ Seri Anwar Ibrahim, kwa Rais wa Marekani, Donald Trump — ambaye mikono yake imejaa damu ya Waislamu wa Gaza — kuja nchini Malaysia kuhudhuria Mkutano wa 47 wa ASEAN jijini Kuala Lumpur. Mwaliko huu si tu ishara ya aibu ya kidiplomasia isiyo na msimamo wa kimaadili; ni aibu kubwa kwa hadhi ya Ummah huu, usaliti unaojeruhi dhamiri ya kila Muislamu ambaye bado ana heshima karibu na moyo wake, hasa zaidi watu wa Palestina.

Soma zaidi...

Tafakari Muhimu Kuhusu Taarifa ya Chama cha Maimamu nchini Uholanzi

Taarifa ya Chama cha Maimamu nchini Uholanzi (VIN) inadai kwamba ushiriki wa kisiasa ndani ya jamii za Ulaya ni “njia inayoruhusiwa na halali,” na kwamba ushiriki unaweza hata wa kupendekezwa au wa lazima kulingana na hali. Msimamo huu unahitaji kuzingatiwa kwa makini, kwani unaegemezwa juu makisio ambayo hayaakisi vya kutosha uhalisia wa mfumo wa kisekula.

Soma zaidi...

Watawala wa Pakistan wanaogopa mwamko wa Kiislamu unaoongezeka miongoni mwa Waislamu wa Pakistan na, kupitia utekelezaji wa Mpango wa Kitaifa wa Utendakazi, wanajaribu—bila mafanikio—kuusimamisha kwa kuigeuza Pakistan kuwa “dola ngumu zaidi.”

Mwenendo mkali na wa kikatili wa watawala dhidi ya mkutano wa TLP umesababisha mawimbi ya wasiwasi katika duara za kidini za Pakistan na kumshangaza kila Muislamu mwenye ufahamu. Hata hivyo, mbinu hii ya kiimla ya watawala wa Pakistan si kitendo cha pekee au kisicho cha kawaida; bali ni sehemu ya msururu wa hatua mfululizo ambazo watawala wamechukua katika siku za hivi karibuni, hatua zilizozidi wakati watawala wa Pakistan walipokubali kutekeleza mpango wa Trump pamoja na watawala wa nchi za Kiarabu na zengine za Kiislamu, mpango ambao lengo lake ni kulinda uwepo wa Mayahudi kutokana na upinzani wa Waislamu wa Palestina.

Soma zaidi...

“Vita vya Burqa” vya Wananchi Ni Mwangwi wa Kisasa wa Ukoloni wa Ulaya, Uliotumika Kupuuza Mauaji ya Halaiki mjini Gaza na Kumvua Mwanamke wa Kiislamu Kitambulisho Chake cha Kiislamu

Vita vya hivi karibuni vya watu wengi kutoka kwa vyama vya kidemokrasia na serikali za mrengo wa kulia vinavyotaka kupigwa marufuku kwa burqa sasa vinajumuisha Australia, Italia na Ureno. Mataifa haya ni sehemu ya kundi kubwa la nchi adui za Ulaya ambazo tayari zimepiga marufuku burqa. Ufaransa, Ubelgiji, Denmark, na Uswizi zinatekeleza marufuku ya kitaifa katika maeneo yote ya umma, huku Uholanzi na Ujerumani, zikiwa na marufuku ya sehemu inayolenga muktadha maalum kama vile shule au afisi za serikali. Nchini Uingereza, mjadala unalenga wafanyikazi, ambapo chama cha mrengo wa kulia cha Mageuzi cha Uingereza kinasema kwamba burqa kama hizo zinazuia uoanishwaji, mawasiliano, na usalama, zikiziita “nembo za mgawanyiko.”

Soma zaidi...

Mayahudi Hawaheshimu Maagano Wala Hawawezi Kuaminiwa, Na Wapatanishi Si Waaminifu

Umbile la Kiyahudi limekiuka makubaliano ya kusitisha mapigano dhidi ya Gaza zaidi ya mara 80, na kusababisha mashahidi wengi na majeraha, pamoja na kubomolewa kwa nyumba na uharibifu wa mali. Waziri mkuu wa umbile la Kiyahudi hata alijisifu kwamba aliangusha tani 153 za mabomu kwenye Ukanda wa Gaza kwa siku moja.

Soma zaidi...

Mwaliko wa Kuhudhuria Kikao cha Kisiasa

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Sudan inafuraha kuwaalika ndugu zetu wanahabari, wanasiasa, na wote wanaopenda masuala ya umma kuhudhuria na kushiriki katika kikao kipya cha kisiasa, ambacho kitamkaribisha Ustadh Muhammad Jami’ (Abu Ayman), Msaidizi wa Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Sudan, chenye kichwa: Msimamo wa Serikali kuhusu Kufutwa kwa Kadhia ya Palestina na Hukmu ya Sharia juu yake.

Soma zaidi...

Watu Wapendao Uislamu wa Nchi Wameukataa Mkataba wa Julai, ambao umejengwa juu ya Msingi wa Usekula na Demokrasia Batili ya Magharibi, Na Wanataka Mkataba wa Madina uliojengwa juu ya Msingi wa Imani yao Safi ya Kiislamu

Mnamo 17 Oktoba 2025, kipote cha wanasiasa wenye uchu wa madaraka nchini humu walitia saini ‘Mkataba wa Julai - suluhisho la kisiasa lililoandikwa kwa kuzingatia imani potofu za kidemokrasia ya kisekula na mfumo wa Wakoloni makafiri wa Magharibi hasa Marekani-Uingereza, na kuweka mfano mwengine wa kuchukiza wa usaliti kwa Uislamu na Waislamu, na utiifu kwa nchi za Magharibi. Mfumo huu wa kisekula wa kibepari uliotungwa na wanadamu umefeli katika nchi zote duniani. Jambo hili ni la kweli mithili ya mwangaza wa mchana kwamba, mfumo huu wa ukandamizaji unalinda maslahi ya tabaka tawala, mabepari wachache na wakoloni wa Magharibi, na kuwanyonya watu wengi zaidi. Mnashuhudia kwamba kizazi cha vijana (Gen-Z) katika nchi nyingi wanaasi tabaka tawala la kibepari moja baada ya jengine na kuwaangusha watawala.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu