Jumamosi, 10 Muharram 1447 | 2025/07/05
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Kuganda Baridini hadi Kufa kwa Watoto Wachanga, na Njaa na Uuaji wa Watoto Hayatoshi Kukomesha Mauaji ya Halaiki huko Gaza!

Mnamo tarehe 30 Disemba, iliripotiwa kuwa mtoto wa 6 waliganda hadi kufa mjini Gaza ndani ya wiki mbili kutokana na hali ya baridi inayovumiliwa na wakimbizi wa Kipalestina katika mahema ya muda, waliohamishwa kutoka kwa nyumba zao kutokana na mashambulizi ya mara kwa mara ya Ukanda huo na uvamizi wa Kiyahudi. Ali al-Batran mwenye umri wa mwezi mmoja alifariki siku moja baada ya kaka yake pacha, Jumaa al-Batran, huko Deir el-Balah. Baba yao, Yahya Muhammad al-Batran, alisema kuwa Jumaa alipatikana kichwa chake kikiwa kama “donge la barafu”. Nariman, mama wa Sila Mahmoud al-Fassih mwenye umri wa siku 20, ambaye pia alifariki kutokana na kupungua kwa joto la mwili, alielezea kumkuta mtoto wake akiwa rangi ya bluu na kuuma ulimi wake huku damu ikimtoka mdomoni. Zaidi ya watu milioni 1.6 wa Gaza wamelazimishwa kuingia kwenye makaazi ya muda, wakiishi katika mahema hafifu ambayo hayatoi ulinzi kutokana na hali ya hewa ya baridi kali.

Soma zaidi...

Hakuna Tofauti Kati ya Uhalifu wa huko New Orleans na Ukatili Unaofanywa na Umbile la Kizayuni huko Gaza

FBI imefichua utambulisho wa mhusika wa shambulizi la kugonga na gari huko New Orleans, Marekani, ambalo lilisababisha vifo na majeruhi ya makumi ya watu wakati wa sherehe za mwaka mpya. Mshambuliaji huyo alitambuliwa kama askari wa zamani wa Wanamaji. Mamlaka mjini New Orleans ziliripoti vifo vya watu 10 na wengine 30 kujeruhiwa baada ya lori kuingia kwenye umati wa watu. Vyombo vya habari vya Marekani viliripoti kwamba watu kadhaa walipoteza maisha baada ya gari hilo kugonga mkusanyiko wa watu kwenye Barabara ya Bourbon katika Mtaa wa Wafaransa wa New Orleans mnamo siku ya Jumatano. Wakati huo huo, Wizara ya Mambo ya Nje ya “Israel” ilisema kwamba “Waisraeli” wawili walijeruhiwa katika tukio hilo.

Soma zaidi...

Uchumi wa Kibepari Unasambaratisha Familia na Misingi yake

Warsha ya karibuni ya kinachoitwa ‘usawa wa kijinsia’ iliyofanyika ndani Ngorongoro, Kaskazini mwa Tanzania iliibua suala la uwepo baadhi ya wanandoa kutoka katika jamii za wafugaji ambao wametelekezwa na waume zao walioondoka vijijini kwenda mijini kutafuta kazi, na wakati mwengine waume hao hawarudi katika familia zao.

Soma zaidi...

Hotuba Inayohusu Bendera za Rayah na Liwaa za Mtume (saw) Ilipambwa kwa Takbira na Machozi katika Soko Kuu la Port Sudan

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan ilitoa hotuba yake ya kisiasa ya kila wiki, iliyokuwa na kichwa: “Je, Mtume (saw) alikuwa na bendera na Rayah?”, mnamo Jumatatu tarehe 28 Jumada al-Akhirah 1446 H sawia na 30/12/2024 M. Ustadh Muhammad Jami’ (Abu Ayman), Msaidizi wa Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Sudan, alizungumza akisisitiza kuwa bendera ya Liwaa na Rayah katika Uislamu ni suala la dini, itikadi, mfumo na nembo ya Uislamu. Mtume (saw), ana benera (Liwaa) nyeupe kama bendera ya amiri jeshi, na bendera (Rayah) nyeusi kwa makamanda wa majeshi na vikosi, na inaitwa Uqab, zimeandikwa juu yazo “La Ilaha illa Allah Muhammad Rasulullah”.

Soma zaidi...

“Mayahudi Hawawi Radhi Nawe, Wala Wakristo, Mpaka Ufuate Mila Yao” [Al-Baqarah: 120]

Utawala mpya nchini Syria umetoa taarifa mtawalia kuhusu mfumo wa serikali ambayo wananuia kutekeleza baada ya dhalimu kutoroka. Ni wazi kuwa si mfumo aliouweka Mwenyezi Mungu (swt) bali ni mfumo wa kisekula unaotenganisha dini na maisha kwa kisingizio cha kuwapa watu uhuru wa kuchagua mfumo wa utawala. Wanawaruhusu waandamanaji wa kike wanaodai uhuru na kuvua hijab, huku wakiwateka nyara waandamanaji wasafi wanaodai kuachiliwa kwa jamaa zao wanaotaka kutabikishwa kwa Shariah ya Mwenyezi Mungu (swt)!

Soma zaidi...

Tukio la Jalalabad: Kuilinda Dawah ni Wajibu kwa Kila Mmoja Wetu

Mnamo tarehe 26 Novemba, Mashababu wa Hizb ut Tahrir waliandaa amali dhidi ya rasimu ya sheria ya “Uhuru wa Dini na Mashirika ya Kidini” katika eneo la Jalalabad. Wiki tatu baadaye, kati ya Disemba 10 na 14, Kamati ya Serikali ya Usalama wa Kitaifa ilifanya msako katika nyumba 21 katika eneo hilo na kuwaweka kizuizini kinyume cha sheria wanachama wa Hizb ut Tahrir. Vikosi vya usalama havikuruhusu wanachama waliozuiliwa (Mashababu) kukutana na mawakili wao na badala yake walifanya uchunguzi mbele ya mawakili waliofunzwa mahususi kwa kesi hii. Kutokana na hali hiyo, Mashababu wetu walizuiliwa kwa muda kwa kipindi cha mwezi mmoja kwa kisingizio cha kusambaza vipeperushi misikitini vinavyopinga sheria hiyo. Kesi ya jinai ilifunguliwa dhidi yao chini ya shtaka la “kuandaa na kuendesha shughuli za itikadi kali.”

Soma zaidi...

Mamlaka ya Palestina Yafuata Mbinu za Mashetani Kuhalalisha Uhalifu wake katika Kambi ya Jenin!

Mamlaka ya Palestina (PA) ilikusanya vyombo vyake vya habari na vipaza sauti vya wasemaji na nzi wa kielektroniki (wanyanyasaji wa mtandaoni wanaounga mkono serikali) ili kuchafulia jina kambi ya Jenin na watu wake na kuhalalisha umwagaji wa damu yao. Kisha, ilikusanya vyombo vyake na majambazi katika mji wa Khalil al-Rahman, na wachache wa wale walioitwa watu mashuhuri waliojiuza kwa PA kwa manufaa maovu, na wale ambao iliwatishia kutoka kwa wafanyikazi na walimu. Ilitumia wizara, shule zilizofungwa, na kukodi mabasi ili Jimbo la Khalil al-Rahman, mji na wilaya, ionekane kuwa pamoja nayo katika kumwaga damu ya watu wa kambi ya Jenin. Hii ijapokuwa inajua na wale walio nyuma ya kwamba Khalil al-Rahman, pamoja na watu wake na koo zake, hawawezi kukubali kwamba itoa nusu ya neno kumwaga tone la damu ya Waislamu. Kwa kitendo hiki kiovu, inataka kuleta mgawanyiko kati ya watu wa Palestina (kaskazini na kusini) chini ya pazia la uongo la uhalifu wake.

Soma zaidi...

Amerika ni Adui Yenu Dhahiri. Majaribio ya Kuidekeza ni Batili. Ni kwa Kusimamisha Khilafah Rashida Pekee, ndio Mnaweza Kuzima Faida ya Kimkakati ya Amerika na Kuipa Jibu Lililofaa!

Mnamo tarehe 21 Disemba, 2024, Afisi ya Mambo ya Nje ya Pakistan “ilipinga vikali ukosoaji wa Marekani wa mpango wa makombora wa masafa marefu wa Pakistan, na kuuita usio na mantiki na usio na muktadha wa kihistoria kwani iliapa kuendelea kukuza uwezo wake wa makombora sambamba na kiwango cha chini uzuiaji wake wa kuaminika wa kimkakati, ikisisitiza hitaji lao la kukabiliana na vitisho vinavyoibuka kutoka India.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu