Jarida la Al-Waie: Vichwa Vikuu vya Habari vya Toleo (477)
- Imepeperushwa katika Jarida la Al-Waie
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
Kwa kuamini qadhaa ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, Hizb ut Tahrir / Wilayah Syria inamuomboleza kwa Waislamu jumla, na kwa wabebaji dawah haswa, Ndugu Omar Abdul Rahim Khatib (Abu Abdo Khatib), mmoja wa wanachama wake, kutoka kijiji cha Arhab katika vijiji vya magharibi mwa Aleppo, na ambaye alifariki akiwa na umri wa miaka 50, ambayo aliitumia kwa utiifu kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu.
Video ya Sehemu ya Hotuba ya Amiri wa Hizb ut Tahrir mwanachuoni Mkubwa Ata bin Khalil Abu Rashtah Mwenyezi Mungu Amhifadhi kwa Mnasaba wa Kumbukumbu ya Miaka 105 ya Kuvunjwa kwa Khilafah
Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Uturuki, kupitia matembezi mikubwa na taarifa kwa vyombo vya habari zilizoandaliwa kote Uturuki chini ya kauli mbiu “Iokoeni Al-Aqsa! Simameni dhidi ya Amerika!”, ililaani ukandamizaji wa umbile nyakuzi la Kizayuni, kiburi cha mkoloni Amerika, na kimya cha watawala wa nchi za Kiislamu kuhusu udhalilishaji huu.
Mnamo siku ya Ijumaa, 3 Aprili 2026, matembezi yaliyoandaliwa na Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Tunisia, mji mkuu wa Tunisia, yalianza kutoka Msikiti wa Al-Fath baada ya swala ya Ijumaa. Matembezi hayo, yaliyofanyika kwa ajili ya kuunusuru Msikiti wa Al-Aqsa na wafungwa wa Palestina, yalikuwa na kichwa: “Kuhamasisha majeshi, kupindua viti vya watawala, na kutangaza jihad ndiyo njia pekee ya kuwaokoa wafungwa na kuikomboa Masra.”
Hizb ut Tahrir / Wilayah Uturuki iliwasilisha taarifa kwa vyombo vya habari yenye hoja kumi kwa Umma wa Kiislamu wakati wa mkutano na waandishi wa habari, yenye kichwa cha habari: “Vita dhidi ya Iran: Ukafiri ni Mila Moja, Na Waislamu ni Umma Mmoja”
Katika siku ya tatu ya Idd al-Fitr Iliyobarikiwa, sawia na Jumamosi, 12 Machi 2026 M, mashababu wa Hizb ut Tahrir/Wilayah Sudan walikusanyika katika afisi ya hizb katikati mwa jiji la Khartoum ili kupeana salamu za Idd. Mkutano huo ulijumuisha mashababu kutoka kote Khartoum, Omdurman, Jabal Awliya, Kalakila, Nile Mashariki, na maeneo mengine. Walitoa pongezi zao kwa Idd iliyobarikiwa na kuelezea furaha yao ya kuonana baada ya miaka mingi ya vita.