Jumatano, 13 Rabi' al-awwal 1448 | 2026/08/26
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan: Amali za Kuhuisha Ibada za Dhu al-Hijjah za Mwaka 1447 H

Katika kuhuisha ibada za Dhul-Hijjah na kwa heshima ya Sunnah tukufu ya Mtume, Hizb ut Tahrir/Wilayah Sudan iliandaa maandamano ya takbira na tahlil mnamo Jumatatu, ya kwanza ya Dhul-Hijjah 1447 H. Maandamano yalianza kwenye lango la afisi ya hizb mjini Port Sudan, yakipita kwenye njia kuu, na kufikia Soko Kuu, ambapo yalifikia kilele chake katika ua wa Hoteli ya Al-Haramain, mahali pa mikutano ya kisiasa ya mji huo. Wakati wa maandamano hayo, umati mkubwa wa watu ulijiunga, wakipiga takbira na tahlil pamoja na ndugu zao, wakionyesha furaha yao kwa amali ya hizb na kusifu amali hii ya kipekee nchini, kwa mujibu wa maelezo yao.

Soma zaidi...

Makala Mbalimbali kutoka Gazeti la Ar-Rayah Toleo la 601

Hakika, sisi katika familia ya Gazeti la Ar-Rayah tunatoa pongezi zetu za dhati kwa Ummah wetu wa Kiislamu kwa mnasaba wa Idd al-Adha iliyobarikiwa. Tunamwomba ﷻ aifanye Idd hii kuwa mwanzo wa kheri na baraka kwetu, ili Idd ijayo ije huku tukiishi chini ya heshima, ushindi, na tamkini, tukiwa tumehifadhiwa chini ya bendera ya Khilafah Rashida bendera ya (لا إله إلا الله محمد رسول الله) “La ilaha illa Allah, Muhammadur Rasul Allah” “Hakuna mungu wa haki ila Mwenyezi Mungu, Muhammad ni Mtume wa Mwenyezi Mungu.” Na hilo si gumu kwa Mwenyezi Mungu ﷻ. Mtume wa Mwenyezi Mungu (ﷺ) amesema, «... ثُمَّ تَكُونُ مُلْكاً جَبْرِيَّةً فَتَكُونُ مَا شَاءَ اللَّهُ أَنْ تَكُونَ ثُمَّ يَرْفَعُهَا إِذَا شَاءَ أَنْ يَرْفَعَهَا ثُمَّ تَكُونُ خِلَافَةً عَلَى مِنْهَاجِ النُّبُوَّةِ» “…Kisha kutakuwa na utawala wa dhulma, na utabakia kwa muda anaotaka Mwenyezi Mungu uwe kisha atauondoa anapotaka kuuondoa. Kisha itakuwepo Khilafah kwa Njia ya Utume.”

Soma zaidi...

“Imekwisha fichuka chuki yao katika midomo yao. Na yanayo ficha vifua vyao ni makubwa zaidi.” [Aal-i-Imran: 118]

Chansela wa Ujerumani Friedrich Merz alitangaza mnamo Ijumaa kupinga kwake Muungano wa Ulaya kuweka vikwazo kwa umbile la Kiyahudi, huku Ufaransa ikitangaza kwamba haitakubali kuondoa vikwazo vilivyowekwa na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuhusu Iran isipokuwa makubaliano yoyote ya mwisho kuhusu mpango wake wa nyuklia yajumuishe kushughulikia mpango wake wa makombora ya masafa marefu na uungaji mkono wake kwa makundi yenye silaha katika eneo hilo.

Soma zaidi...

Je, Erdogan Anasubiri Mayahudi Waipige Mabomu Ankara Kabla ya Kuhamasisha Jeshi Lake?!

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdoğan, katika hotuba aliyotoa wakati wa mkutano wa kundi la wabunge wa Chama cha Haki na Maendeleo katika Bunge la Uturuki, alisema: "Tunafahamu vyema lengo kuu la udanganyifu wa 'Ardhi iliyo Ahidiwa', na Mungu akipenda, hatutaruhusu kamwe." Alifafanua kwamba usalama wa Uturuki hauanzii katika mkoa wa Hatay kusini mwa Uturuki, bali Aleppo, Damascus, na Beirut. Aliendelea: "Ikiwa uonevu wa Israel hautasimamishwa, gharama haitalipwa na eneo hilo pekee, bali na wanadamu wote." Erdoğan alizisihi dola kuu duniani kuchukua msimamo wazi dhidi ya umbile hilo la Kizayuni, akisema: "Kuirudisha Israel katika kufuata sheria sio tena jukumu la baadhi ya nchi tu, bali ni jukumu la pamoja linalowaangukia wanadamu wote."

Soma zaidi...

Moto Mijini: Jinsi Ubepari Unavyowasha Moto katika Miji ya Waislamu yenye Wakaazi Wengi

Mnamo Jumatatu, tarehe 1 Juni 2026, vyombo vya habari viliripoti kuhusu moto mkubwa ulioharibu eneo la makaazi lenye watu wengi huko Kebon Kosong, Kemayoran, Jakarta ya Kati, Indonesia. Takwimu rasmi kutoka kwa Wakala wa Kupunguza Maafa wa DKI Jakarta (BPBD) na uthibitishaji wa uwanjani zinaonyesha takriban familia 354—takriban watu 620—waliachwa bila makao. Takriban watoto 160 wenye umri wa kwenda shule waliathiriwa moja kwa moja.

Soma zaidi...

Ardhi Zetu Zitabaki Kukiukwa na Damu Yetu Itaendelea Kumwagika Hadi Tutakaposimamisha Khilafah Rashida Yetu

Mnamo Jumapili, tarehe 14 Juni 2026, jeshi la Kiyahudi lilifanya shambulizi la anga likilenga vitongoji vya kusini mwa Beirut, saa chache tu baada ya kuwaonya wakaazi wa takriban miji 30 kusini mwa Lebanon na kuwaamuru waondoke. Tovuti ya habari ya Axios iliripoti kwamba “jeshi la ‘Israel’ liliiarifu CENTCOM muda mfupi kabla ya shambulizi jijini Beirut kutokea.” Trump aliandika kwenye jukwaa lake la ‘Truth Social’ mnamo Jumapili: “Shambulizi la asubuhi ya leo dhidi ya Beirut halikupaswa kutokea, haswa katika siku maalum ambapo tuko karibu sana na Mkataba wa Amani na Iran.”

Soma zaidi...

Mtoto Aliyeuawa Shahidi, Kuhesabiwa kwa Waathiriwa Kutaisha Lini? Watu wa Damu hiyo Watainuka Lini Kuwalipiza Kisasi?

Wizara ya Afya ya Palestina ilisema kwamba vikosi vya uvamizi vilifyatua risasi kwenye gari moja lililokuwa limebeba raia wa Palestina katika mji wa Hebron katika Ukingo wa Magharibi wa kusini unaokaliwa kimabavu, na kusababisha kifo cha kishahidi cha mtoto mchanga wa miezi saba Sam Abu Hikal huku akiwa mikononi mwa mamake. Mamake na babake pia walijeruhiwa.

Soma zaidi...

Enyi Ummah wa Kiislamu na Majeshi Yake: Ikiwa Hamkasirishwi kwa ajili ya Mwenyezi Mungu na Mambo Yake Matakatifu, Basi Mtakasirishwa na Kuchukua Hatua kwa ajili ya Nini?!

Mnamo Jumatano, 27/5/2026, vyombo vya habari na mitandao ya kijamii vilirusha picha zinazoonyesha vikosi vya umbile la Kiyahudi vikimshambulia kikatili mwanamke mchanga wa Kipalestina huko Bab Hutta, moja ya malango ya Msikiti mtukufu wa Al-Aqsa, vikimnyang'anya kitambaa chake cha kichwani kwa nguvu kabla ya kumkamata. Tukio hili linajiri huku kukiwa na ongezeko la ukiukwaji wa sheria na hatua za usalama ulioongezeka kutoka kwa vikosi vya uvamizi katika milango ya kuingia katika Jiji la Kale la Al-Quds na malango ya Msikiti wa Al-Aqsa, sanjari na Idd al-Adha. Waliweka vituo vya ukaguzi na kuchunguza vitambulisho vya wapita njia, wakizuia idadi kubwa ya watu kuingia msikitini.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu