Ijumaa, 16 Muharram 1447 | 2025/07/11
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Umebarikiwa kwa Nguvu, Umedhoofishwa na Mgawanyiko

"Pentagon yasema Marekani haitaki kuanzisha vita na Iran" - hii, baada ya kudondosha mabomu kumi na nne aina ya bunker-buster kwenye vituo vitatu vya nyuklia ndani ya ardhi ya Iran. Kauli kama hiyo si ya kinafiki tu - ni ya kuchukiza. Inaakisi mawazo ya kiburi, ya kikoloni. Mtu yeyote mwenye akili timamu anawezaje kuamini kwamba vita sio nia pindi taifa linapofanya mashambulizi yaliyoratibiwa kwa taifa jengine?

Soma zaidi...

Vita vya Amerika na umbile la Kiyahudi dhidi ya Iran: Kimya cha Watawala na Kujisalimisha kwa Murshed

Rais wa Marekani Donald Trump alitangaza makubaliano kamili kati ya Israel na Iran juu ya usitishaji kamili wa mapigano. Katika jukwaa lake la Kijamii la Truth, Trump alisema: "PONGEZI KWA KILA MTU! Imekubaliwa kikamilifu na kati ya Israel na Iran kwamba kutakuwa na Usitishaji Vita Kamili na Jumla (katika takriban saa 6 kutoka sasa, wakati Israel na Iran zitakapomaliza na kukamilisha misheni zao zinazoendelea, za mwisho!), kwa masaa 12, ambapo Vita vitazingatiwa, VIMEMALIZIKA! Trump alisifu pande zote mbili, akisema: "Misuli, Ujasiri, na Ujasusi kumaliza" mzozo na kusema kwamba ulimwengu na Mashariki ya Kati ndio "WASHINDI halisi".

Soma zaidi...

Erdoğan anapaswa Kuhutubia Umma wenye Ikhlasi na sio Walinzi wa Sykes-Picot kwa Umoja na Udugu wa Kiislamu!

Akihutubia Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu jijini Istanbul, Rais Recep Tayyip Erdoğan ametoa wito wa kuwepo umoja na udugu mkubwa zaidi miongoni mwa nchi za Kiislamu. Erdoğan pia alisema, "Hatutaruhusu kuanzishwa kwa agizo jipya la Sykes-Picot katika eneo letu mipaka kuchorwa kwa damu." Na alisisitiza kwa mara nyengine kwamba suluhisho liko katika "diplomasia na mazungumzo".

Soma zaidi...

Msafara wa Uthabiti kati ya Khiyana ya Utawala wa Misri na Wajibu wa Jeshi lake kuchukua Hatua

Huku kukiwa na mikutano tasa na makongamano ya uhadaifu, msafara maarufu unaojiita "Msafara wa Uthabiti" ulitoka Tunisia, Algeria, na Morocco, kuelekea Gaza kupitia Libya na Misri, kwa lengo la kuvunja mzingiro na kusaidia watu wa Ukanda wa Gaza, ambao wamekuwa chini ya vikwazo kwa zaidi ya miezi kumi na nane. Msafara huo uliwabeba wanaume na wanawake wa rika zote, waliounganishwa kwa lengo moja: kuvunja mzingiro huu uliowekwa na umbile la Kiyahudi kwa watu wa Gaza, kwa ushirika na ushiriki wa moja kwa moja wa tawala zilizo jirani, hasa unaoshikilia bendera kati yao utawala wa Misri.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu