Jumamosi, 24 Muharram 1447 | 2025/07/19
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Mwaliko wa Kuhudhuria na Kushiriki katika Kikao cha Masuala ya Ummah

Sisi, katika Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan, tunafuraha kuwaalika wanataaluma wa vyombo vya habari, wanasiasa, na wale wanaohusika na masuala ya umma kuhudhuria na kushiriki katika Kikao cha Masuala ya Ummah wa kila mwezi, ambacho mwezi huu kitakuwa na kichwa: “Hatari ya Kuyatazama Mamlaka Kama Keki Inayopaswa Kugawanywa”

Soma zaidi...

Haya ndiyo Matendo ya Umoja wa Mataifa... Mutaendelea Kuwahadaa Wananchi Mpaka Lini? Ni Kipi Kipya? Yako wapi Mabadiliko, Ee Wizara ya Ujenzi na Mabadiliko?

Mnamo Jumapili, tarehe 29/6/2025, jijini Sana'a, Waziri wa Masuala ya Kijamii na Leba, Samir Baja'ala, alifanya mkutano na kamati za maandalizi ya Kongamano la Vyama vya Ushirika la 2025, litakaofanyika mapema Julai 2025. Mkutano huo ulihudhuriwa na Ali Al-Razami, Katibu Mdogo wa Wizara ya Sekta ya Maendeleo na Nasser Al-Kahili, Mkurugenzi wa Afisi ya Masuala ya Kijamii na Afisi ya Leba katika Sekretarieti Kuu.

Soma zaidi...

Trump na Netanyahu Wanajigamba na Kujisifu Huku Watawala Wetu Wakikaa Kimya Mithili ya Wafu Makaburini Mwao!

Vita kati ya Iran na umbile la Kiyahudi vimemalizika, na jinai za Mayahudi mjini Gaza hazikukoma wakati wa vita hivyo, wala hadi wakati huu. Marekani ilifanya ujanja wa kiusanii, ikidai kuwa imeangamiza uwezo wa nyuklia wa Iran. Hatua hii imekuja baada ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran kukutana na wale wanaojiita mawaziri wa Troika wa Ulaya, ambao walikuwa sehemu ya mazungumzo ya nyuklia ya Iran kabla ya Marekani kujitoa katika mazungumzo hayo wakati wa muhula wa kwanza wa Trump. Iran pia ilifanya mbwembwe za kiusanii kwa kurusha makombora kadhaa katika Kambi ya Kimarekani ya Al Udeid nchini Qatar, baada ya kuifahamisha Marekani kuhusu hilo, kama Trump mwenyewe alivyosema.

Soma zaidi...

Harakati ya Taliban na Fursa ya Kusimamisha Khilafah

Maisha haya ya dunia ni kama dimbwi la hasara, ambalo ni wale tu wanaojua kukamata fursa ndio wataokolewa. Kwa sababu hii, Siku ya Kiyama inaitwa “Siku ya Majuto,” kwa sababu watu wengi wamezama katika hasara ya kidunia, na wameshindwa kutumia fursa za thamani walizopewa katika maisha yao. Walipoteza kwa urahisi nyakati za dhahabu alizozitoa Mwenyezi Mungu (swt) kwa ajili ya mwamko na izza ya Umma.

Soma zaidi...

Uamuzi wa Mahakama ya Upeo Unaipa Zinaa Nafasi sawa na Ndoa

Mahakama ya Upeo imeamua kuwa watoto waliozaliwa nje ya ndoa na baba Waislamu wana haki ya kurithi mali ya baba yao, jambo linaloashiria maendeleo makubwa katika tafsiri ya sheria za kibinafsi za Kiislamu nchini Kenya. Hii ni baada ya Mahakama ya Juu mnamo Jumatatu tarehe 30 Juni kutupilia mbali rufaa ya Fatuma Athman Abud Faraj, ambaye alitaka kuwatenga watoto wa marehemu mumewe, Salim Juma Hakeem Kitendo, katika mali yake kwa madai kwamba walizaliwa nje ya ndoa inayotambulika ya Kiislamu.

Soma zaidi...

Maumbile ya Mahusiano kati ya Uingereza na Urusi

Maumbile ya mahusiano kati ya Uingereza na Urusi yamekuwa makali na yenye taharuki tangu karne ya 18, na uadui wa wazi na dhahiri kati yao. Kwa mfano, Dmitry Medvedev, Naibu Mwenyekiti wa Baraza la Usalama la Urusi, alisema mnamo Aprili 21, 2023, "Uingereza daima imekuwa, na sasa, na itakuwa adui yetu wa milele. Angalau hadi wakati ambapo kisiwa chao chenye majivuno kitazama ndani ya shimo la bahari kutokana na wimbi lililochochewa na mfumo wa kivita wa Urusi."

Soma zaidi...

Ongezeko la Wanamgambo nchini Sudan Linasonga Kaskazini!

Tangu Ijumaa, tarehe 27/6/2025, vyombo vya habari vimeripoti kuwa Rais wa Eritrea Isaias Afwerki amekubali kutoa mafunzo kwa wapiganaji elfu 50 kutoka majimbo ya Kaskazini na Mto Nile katika mafunzo ya juu ya kijeshi, kulingana na ombi lililowasilishwa na mkuu wa Jimbo la Kaskazini, Mohamed Sayed Ahmed Al-Jakoumi, mkuu wa Upande wa Kaskazini wa Makubaliano ya Juba ya Amani ya Sudan.

Soma zaidi...

Jibu la Swali: Uvamizi wa Umbile la Kiyahudi dhidi ya Iran na Athari zake

Al Arabiya ilichapisha kwenye tovuti yake mnamo tarehe 27/6/2025: "Vyanzo vinne vyenye taaarifa vilisema kuwa utawala wa Rais Donald Trump ulijadili uwezekano wa kuisaidia Iran kufikia hadi dolari bilioni 30 ili kujenga mpango wa nyuklia kwa ajili ya uzalishaji wa nishati ya kiraia. Vyanzo hivyo viliongeza kuwa majadiliano haya yaliendelea wiki hii baada ya kufikiwa kwa makubaliano ya kusitisha mapigano. Maafisa wa utawala wa Trump walithibitisha kwamba mapendekezo kadhaa yamewsilishwa, ya awali pamoja na yaliyoboreshwa, yakiwa na kifungu kimoja kisichobadilika, kisichoweza kujadiliwa : “kukomeshwa kabisa kwa urutubishaji wa urania ya Iran.”

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu