Ijumaa, 27 Rabi' al-awwal 1447 | 2025/09/19
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Waziri wa Mambo ya Nje wa Denmark Ajifanya Kuijali Palestina, Huku Mikono Yake Ikiloa Damu ya Watu Wasio na Hatia wa Gaza

Tarehe 07-09-2025, Waziri wa Mambo ya Nje wa Denmark, Lars Løkke Rasmussen, alisafiri hadi Palestina inayokaliwa kwa mabavu na kukutana na marafiki zake na wenzake Wazayuni “kuonyesha kujali” na “kutia shinikizo” kwa serikali vamizi ya Kizayuni. Ziara hii ya kirafiki utawala vamizi wa Kizayuni inakuja siku chache tu baada ya Waziri wa Mambo ya Nje huyo kuchapisha video kwenye mtandao wa kijamii, ambapo alitoa maoni kwamba “Serikali ya Denmark sasa inachukua hatua za kuondoa kura ya turufu ya Israel juu ya msimamo wetu [kuhusiana na utambuzi wa baadaye wa Palestina]”.

Soma zaidi...

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Wakutana na Mkurugenzi wa Khalawi na Idara za Misikiti katika Mji wa Port Sudan

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir/Wilayah Sudan ukiongozwa na Ustadh Nasser Ridha Mkuu wa Kamati Kuu ya Mawasiliano ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Sudan akifuatana na Ustadh Abdullah Ismail Mjumbe wa Kamati ya Mawasiliano, ulimtembelea Sheikh Onour Muhammad Ahmed, Mkurugenzi wa Khalawi na Idara za Misikiti katika Mji wa Port Sudan, afisini kwake, kama sehemu ya kampeni iliyoandaliwa na Hizb kutibua njama ya kuichana Sudan kwa kuitenganisha Darfur.

Soma zaidi...

Ghasia za Indonesia: Mabadiliko Ambayo (Bado) Yamefungwa?

Msiba wa Affan Kurniawan, dereva wa teksi ya pikipiki wa mtandaoni wa Indonesia aliyeuawa baada ya kugongwa na gari la polisi aina ya barracuda mnamo 28 Agosti 2025, uliishia katika msururu wa maandamano katika miji mingi kote Indonesia. Makala haya hayakusudii kujibu maswali, bali kuibua maswali kwa yeyote anayedai kuwa mwanaharakati wa Kiislamu.

Soma zaidi...

Swahaba Mtukufu Mus’ab ibn Umair, Mwenyezi Mungu (swt) Amuwie Radhi

Katika kundi la majina yenye kung'aa ya maswahaba watukufu, jina la Mus’ab bin Umair (ra) linajitokeza kama ishara ya muhanga na uthabiti. Mus’ab alikuwa mshika mwenge wa Da’wah katika hatua zake zote, kwani alikuwa ni kijana miongoni mwa vijana bora wa Makka, aliyejulikana kwa uzuri wake, harufu ya kupendeza, na maisha ya anasa, kiasi kwamba Maswahaba, Mwenyezi Mungu (swt) awawie radhi wote, wakasema juu yake, ما رأينا بمكة أحدا انعم عيشا من مصعب بن عمير “Hatujamuona mtu yeyote mjini Makka ambaye aliishi kwa neema kuliko Mus’ab bin Umair.”

Soma zaidi...

Mtihani wa Gaza

Mwenyezi Mungu (swt) hakumuumba mwanadamu bila ya kuweka mbele yake mitihani kulingana na ukubwa wa Imani yake na kujitolea kwake katika Dini, ili Mwenyezi Mungu (swt) apate kujua ni nani atakayekuwa na subira mbele ya mitihani hiyo na kuweka tegemeo lake (tawakkul) kwa Mwenyezi Mungu (swt) . Haya ni ili Mwenyezi Mungu (swt) amuepushe na fitna. Ama wale ambao watafeli ndani ya mitihani hiyo, watafeli tu kwa sababu ya hukumu yao mbaya, kughafilika kwao na Amri za Mwenyezi Mungu (swt), na Imani yao dhaifu.

Soma zaidi...

Iwe ni Suala la Mafuriko au Kashmir, Suala la Uchumi au Kukaliwa Kimabavu kwa Mito Yetu na Dola ya Kibaniani —Je, Tutaendelea Kungoja ‘Jumuiya ya Kimataifa’ Mpaka Lini Kutatua Matatizo Yetu?

Baada ya mafuriko makubwa katika majimbo ya kaskazini ya Khyber Pakhtunkhwa, hasa katika Buner na maeneo ya karibu, ambapo mamia ya watu walipoteza maisha na nyumba, mifugo, mali na magari kusombwa na maji, mafuriko mapya sasa yanapitia Punjab na baadaye yataelekea Sindh. Hapo awali, Karachi pia ilikumbwa na mvua kubwa. Tunamuombea Mwenyezi Mungu Mtukufu usalama na kheri, kwani pamoja na utabiri zaidi wa mvua, watawala wetu wameinua mikono juu tu na kuliacha suala zima kwa rehema ya jumuiya ya kimataifa. Wanaendelea kuwasilisha suala hili zima kwa namna ambayo ni kana kwamba haya ni mabadiliko ya tabianchi ambayo hayawezi kudhibitiwa kabisa na wao, na ikiwa ‘jumuiya ya kimataifa’ haitaingilia kati, wataachwa bila msaada kabisa – kana kwamba ulinzi wa maisha na mali ya watu wao sio jukumu lao bali ni la mfumo wa kimataifa!

Soma zaidi...

Ukosoaji wa Trump wa India ... Maslahi ya Amerika, Sio Urafiki na Pakistan

Mnamo 30 Julai 2025, Rais wa Marekani, Donald Trump alitangaza msururu wa ushuru wa kulipiza kisasi dhidi ya India, akiikosoa kwa kuwa na “vizuizi vizito na visivyo vumilika vya biashara visivyo vya ushuru” na kutoza ushuru wa forodha wa 25% pamoja na faini. Huku Trump alkikiri “urafiki” na India, aliikosoa vikali kwa kununua vifaa vya kijeshi vya Urusi na mafuta ya bei nafuu wakati Marekani ilikuwa ikiishinikiza Urusi kumaliza vita nchini Ukraine. Katika karipio la hadharani lisilo la kawaida, Trump aliusifu uchumi wa Urusi na India kuwa “umekufa” na akamuonya Rais wa zamani wa Urusi Medvedev “kuchunga mdomo wake.”

Soma zaidi...

Marekani ya Kibeberu Inatumia Wakala Wake Shirika la Excelerate Energy kutia Udhibiti juu ya Bandari na Bahari zetu za Kimkakati ili Kuendeleza Udhibiti wake wa Kisiasa

Balozi wa zamani wa Marekani nchini Bangladesh Peter D Haas alifanya mkutano wa karibu saa moja na Waziri wa Mambo ya Nje Asad Alam Siam mnamo Alhamisi (4 Septemba). Ingawa hakuna upande uliofichua maelezo ya majadiliano hayo, vyanzo vya habari viliripoti kuwa mazungumzo hayo yalihusu uwezekano wa kuagiza LNG kutoka Marekani, pamoja na ushirikiano wa sasa na miradi ya mustakabali. Kwa sasa Haas anatumika kama Mshauri wa Kimkakati wa Excelerate Energy - shirika la kimataifa la Texas ambalo linaendesha kituo cha LNG kinachoelea huko Maheshkhali, Cox’s bazar.

Soma zaidi...

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan Wakutana na Mwenyekiti wa Mamlaka ya Wanazuoni katika Jimbo la White Nile

Jana, Jumatatu, tarehe 8/9/2025, huko Rabak, mji mkuu wa Jimbo la White Nile, ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir/Wilayah ya Sudan ulikutana na Sheikh Abdullah Al-Nur Tutu, Imam na Khatib wa Msikiti Mkuu wa Asalaya na Mwenyekiti wa Mamlaka ya Wanazuoni wa Sudan, Tawi la White Nile, nyumbani kwake katika kitongoji cha Asalaya. Ujumbe huo uliongozwa na wafuatao Dkt. Ahmad Mohammad, mwanachama wa Hizb ut Tahrir, akifuatana na Ustadh Faisal Madani, Abdul Majeed Osman Abu Hajar, na Al-Zein Abdul Rahman, wanachama wa Hizb ut Tahrir. Mkutano huo ulikuwa sehemu ya kampeni ya Hizb ut Tahrir ya kuzuia kujitenga kwa Darfur.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu