“Amali” kama Pazia la Ukaliaji wa Kimabavu
- Imepeperushwa katika Uholanzi
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Yale yanayoitwa makubaliano kati ya dola vamizi “Israel” na Hamas, yaliyopangwa na Washington, yanawasilishwa katika vyombo vya habari vya Magharibi na kwa masikitiko pia katika sehemu za ulimwengu wa Kiislamu kama hatua kuelekea amani. Kiulisia, si kitu chengine ila ni marudio ya mtindo wa zamani: mradi wa kikoloni “Israel” unaimarishwa na kulindwa zaidi, huku jinai zake zikifinikwa na vazi la “amani.”



