Jumamosi, 21 Muharram 1446 | 2024/07/27
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Masuluhisho Yaliyopendekezwa kwa Gaza ya baada ya Vita

Huku vita vya mauaji ya halaiki vya umbile la Kiyahudi, kwa uungaji mkono muovu wa Marekani ya Magharibi, vikiendelea dhidi ya watu wa Gaza kwa zaidi ya miezi mitano, na wahanga wake kufikia zaidi ya mashahidi na majeruhi 100,000, pamoja na kuangamizwa kwa sehemu kubwa ya majengo yake, kuna mazungumzo mengi kuhusu miradi ya massuluhisho ya kile kitakachokuja baada ya vita vya Gaza na jinsi mambo yatakavyokuwa kisiasa kulingana na mipango ya dola za kikoloni zikiongozwa na Marekani.

Soma zaidi...

Kwa Nini Wafungwa wa Kisiasa wa Zamani Wanakamatwa Tena?

Vijana 23 wanaoshtakiwa kwa sasa huko Tashkent wote wamekuwa gerezani kwa zaidi ya miaka ishirini na hawajaregea kwa familia zao kwa muda mrefu. Ni wanaume mashujaa wa zama zetu waliotaka kufuata Dini yetu kikamilifu, hawakukaa kimya mbele ya ukandamizaji, na kisha wakatuhumiwa kwa sababu ya fikra na imani zao, wakistahamili karibu robo karne ya mateso yasiyo ya kibinadamu kizuizini.

Soma zaidi...

Barua kwa Raisi wa Uzbekistan Shavkat Mirziyoyev

Tunamwambia Bw. Shavkat Mirziyoyev: Mashababu wote wa Hizb ut Tahrir wanaozuiliwa katika magereza ya Uzbekistan, ambao kwa sasa wako katika kesi, wanaofanyiwa uchunguzi, au wanaoishi uhamishoni, ni Wauzbekistani. Mwenyezi Mungu amewapa haki kamili ya kutoa maoni yao kwa manufaa ya nchi hii... Zaidi ya hayo, ulipochukua urais, ulikula kiapo kwenye muundo huo wa kikatiba uliothibitisha haki ya kujieleza na kuabudu. Hivyo basi, utawala haujashikamana na amri ya Mwenyezi Mungu wala muundo huo wa kikatiba kiutendaji!

Soma zaidi...

Wakenya Amkeni

Kenya, shamba la kikoloni, kwa mara nyingine imo katika mchafuko na mtikisiko kwa kuwa mchezo wa bahati nasibu wa kidemokrasia umezunguka nyuzi 360! Walioko madarakani na walioko barabarani wakiandamana wanalaumiana, huku madai yakielekezwa kwa Mswada wa  Kifedha wa 2024 ulioandaliwa kwa maelekezo ya Mfuko wa Fedha wa Kimataifa (IMF) (Business Daily, 28 Juni 2024)! Mswada huo unapendekeza mikakati ya kuzidisha ukusanyaji wa ushuru ambao unatajwa kuwa ni wenye kukandamiza na kuwadidimiza  raia katika umasikini zaidi!

Soma zaidi...

Utawala wa Mirziyoyev nchini Uzbekistan Unafuata Nyayo za Karimov Aliyekufa, katika Kuwatesa Mashababu wa Hizb ut Tahrir na Kukabiliana na Uislamu

Vyombo vya usalama nchini Uzbekistan vimewakamata tena wanachama 23 wa Hizb ut Tahrir na kuendelea na taratibu za kesi zao Mei 9 2024 kwa mashtaka yale yale waliyoshtakiwa wakati wa enzi ya dhalimu aliyefariki Karimov. Mashababu hao tayari walikuwa washatumia karibu miaka 20 jela na mateso tangu 1999 - 2000 M.

Soma zaidi...

Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir: Kampeni “Enyi Umma; Kilio Wanacholia Wafungwa wa Dhamiri nchini Uzbekistan!”

Vyombo vya usalama nchini Uzbekistan vimewakamata tena wanachama 23 wa Hizb ut Tahrir na kuendelea na taratibu za kesi zao Mei 9 mwaka huu kwa mashtaka yale yale waliyoshtakiwa wakati wa enzi ya dhalimu aliyefariki Karimov, ambayo kwayo walitumia karibu miaka 20 jela na mateso tangu 1999 - 2000 M.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Syria: Kalima katika Kisimamo cha Ijumaa: “Dua za kina Mama Zinawakisha Moyo wa kila Mwanamapinduzi na Kuteketeza Kiti cha Enzi cha kila Msaliti!”

Kalima yenye kichwa “Jueni kwamba katika Mapinduzi yenu munaelekea Njia Panda!” Imetolewa na Ustadh Abdo Al-Dalli (Abu Al-Mundhir), Mwanachama wa Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Syria.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu