Waziri wa Mambo ya Nje wa Denmark Ajifanya Kuijali Palestina, Huku Mikono Yake Ikiloa Damu ya Watu Wasio na Hatia wa Gaza
- Imepeperushwa katika Habari na Maoni
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Tarehe 07-09-2025, Waziri wa Mambo ya Nje wa Denmark, Lars Løkke Rasmussen, alisafiri hadi Palestina inayokaliwa kwa mabavu na kukutana na marafiki zake na wenzake Wazayuni “kuonyesha kujali” na “kutia shinikizo” kwa serikali vamizi ya Kizayuni. Ziara hii ya kirafiki utawala vamizi wa Kizayuni inakuja siku chache tu baada ya Waziri wa Mambo ya Nje huyo kuchapisha video kwenye mtandao wa kijamii, ambapo alitoa maoni kwamba “Serikali ya Denmark sasa inachukua hatua za kuondoa kura ya turufu ya Israel juu ya msimamo wetu [kuhusiana na utambuzi wa baadaye wa Palestina]”.