Gazeti la Al-Raya: Vichwa Vikuu vya Toleo 608
- Imepeperushwa katika Al-Rayah
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Rais wa Misri el-Sisi alisisitiza umuhimu wa kuimarisha mfumo wa hatua za pamoja za Waarabu na kuamsha dori ya Umoja wa Kiarabu kama "mwavuli mkuu na mfumo kamili wa kutetea maslahi ya dola za Kiarabu na Waarabu." Hii ilikuja wakati wa mapokezi yake mnamo Jumapili ya Nabil Fahmy, mgombea wa wadhifa wa Katibu Mkuu wa Umoja huo, na Ahmed Aboul Gheit, Katibu Mkuu wa sasa, ambaye muhula wake unaisha mwishoni mwa mwezi huu. El-Sisi pia alithibitisha "maono ya Misri ambayo yana nia ya kuchukua dori za kujenga ambazo zinakuza masuluhisho ya amani kwa migogoro ya eneo hilo."
Tunawajulisha kwamba Mkuu wa Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir / Wilayah Syria sasa ni Ustadh Ali Mustafa Al-Bakri, kuanzia 1 Muharram 1448 H, sawia na 16/06/2026 M, pamoja na shukrani za dhati kwa Ustadh Ahmad Abdul Wahhab kwa juhudi zake na kujitolea kwake katika miaka yake uongozi wa afisi hii.
Mwaka Mpya wa Hijri unatujia tarehe 1 Muharram 1448 H, sawia na 16/06/2026 M. Hii ndiyo tarehe iliyochaguliwa na Al-Faruq Umar ibn Al-Khattab na Maswahaba watukufu (ra) kama kalenda ya Waislamu. Alichagua tarehe hii kwa sababu iliashiria kuzaliwa kwa Dola ya kwanza ya Kiislamu iliyosimamishwa na Mtume wetu (saw) mjini Al-Madinah Al-Munawwarah.
Harakati maarufu katika majiji na miji kadhaa ya Syria, zinazojirudia kwa zaidi ya mnasaba mmoja baada ya kuanguka kwa utawala wa kihalifu uliokufa, hivi karibuni zaidi vuguvugu maarufu dhidi ya wale wanaoitwa Shabiha (majambazi), zinathibitisha ukweli kadhaa ambao haupaswi kusahaulika na watu wetu nchini Syria
Ghadhabu na hasira ziliongezeka nchini Tunisia wiki iliyopita kufuatia ajali nyingine mbaya, wakati huu katika wilaya ya Mazouna katika jimbo la Sidi Bouzid. Ajali hiyo iliwaacha wafanyikazi kadhaa wa kike wa shambani wakiwa wamejeruhiwa na wawili wakiwa wamekufa katika eneo la tukio. Tunisia inashuhudia kujirudia kwa matukio kama hayo kutokana na serikali kushindwa kukomesha usafiri usiodhibitiwa na kuboresha hali mbaya ya wafanyikazi wa kike wa mashamba! Bila shaka, serikali hii inakwepa kutoa tarakimu na takwimu sahihi zinazoonyesha ukubwa wa janga hilo!