Pakistan, Nchi Safi, Haiwakaribishi Wala Haiwasalimu Vizazi vya Khiyana vya Wasaliti
- Imepeperushwa katika Pakistan
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Baada ya kimya cha wafu makaburini cha serikali za vibaraka zinazobebesha mzigo ardhi za Waislamu, kuhusu mauaji ya Kiyahudi mjini Gaza kwa zaidi ya miaka miwili, vibaraka wa Amerika na Uingereza, washirika wa Mayahudi, walianza kuchukua hatua na kuwa wachangamfu katika kutekeleza mpango wa Trump wa kufilisi kile kilichobaki cha upinzani huko Palestina, kukandamiza na kuua watu mjini Gaza, na kubomoa kile ambacho Mayahudi hawakubomoa cha mawe. “Jenerali anayependwa zaidi wa Trump” Asim Munir alitembelea Jordan mnamo 26 Oktoba, na kwa badali yake, mnamo 16 Novemba 2025, Mfalme Abdullah II bin Al-Hussein, Mfalme wa Ufalme wa Hashimiya wa Jordan na Kamanda Mkuu wa Vikosi vya Wanajeshi wa Jordan, alitembelea Pakistan, akifuatana na binti yake Salma binti Abdullah II bin Al-Hussein, na ujumbe wa maafisa wa kiraia na kijeshi wa Jordan.



