Gazeti la Al-Raya: Vichwa Vikuu vya Toleo 541
- Imepeperushwa katika Al-Rayah
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Hizb ut Tahrir/Amerika inaandaa kongamano lake la kila mwaka la Khilafah kwa mwaka huu, 2025, chini ya kichwa: “Ulimwengu uko katika Njia panda: Mgogoro wa Kimfumo na Njia ya Kusonga Mbele”
Televisheni ya serikali ya Pakistan ilisema mnamo 19 Machi 2025: “Pakistan inalaani vikali mashambulizi ya anga ya Israel.” Hivi ndivyo watawala wa Pakistan walivyolaani hujuma ya Mayahudi na jinai zake zinazoendelea dhidi ya Ukanda wa Gaza! Bila kusonga askari au kuinua silaha!
Kufuatia umbile halifu la Kiyahudi kukiuka makubaliano dhaifu ya kusitisha mapigano alfajiri ya Jumanne, Machi 18, 2025, na kuanza tena mauaji ya kimpangilio ya Waislamu wasio na ulinzi, ambao wengi wao ni wanawake, watoto, na wazee, Hizb ut Tahrir / Uholanzi iliandaa matembezi na kisimamo cha halaiki katika mji mkuu wa Uholanzi, Amsterdam, kwa kichwa: “Harakati kwa ajili ya Gaza!”
Hebu Idd hii na iwe ukumbusho kwamba faraja iko pamoja na dhiki. Kupitia umoja, ukakamavu, na imani isiyoyumbayumba, tunatoa njia kwa ajili ya mustakabali wa heshima na nguvu. Simameni imara katika Dini yenu, na simamisheni haki, hebu Taqwa na iongoze kila kitendo.
Ndugu na Dada Wapendwa: Idd hii inakuja na dola ovu ya Kiyahudi inafanya ukatili dhidi ya watu, miti na mawe huko Gaza na Palestina yote, inafanya hivyo kwa msaada wa Marekani, ambayo inaipatia mabomu, makombora na ndege. Ingawa si ajabu kwamba umbile la Kiyahudi kwa kuungwa mkono na Marekani linatekeleza hili, kwani wao ni adui wa Uislamu na Waislamu, lakini cha ajabu ni kwamba hakuna hata mmoja wa watawala katika nchi za Kiislamu anayechukua hatua, hasa wale walioko pambizoni mwa Palestina, ili kuyakusanya majeshi yao kuinusuru Gaza, watu wake, Al-Aqsa, na viunga vyake, na kuling'oa umbile la Kiyahudi kutoka kwenye mizizi yake, na kisha kuiregesha Palestina yote kwa watu wake. Je, yule anayeikalia kwa mabavu ardhi ya Kiislamu na akawatoa watu wake humo hastahiki kupigwa vita na majeshi ya Waislamu na kufukuzwa humo kama walivyowafukuza watu wake?
Ummah umepitia mateso ya kubaki chini ya nira ya tawala za vibaraka. Umeshuhudia kwa macho yake wenyewe watawala wakifuja mali zake kwa makafiri, wakoloni wa Magharibi, kuzitelekeza kwao na sababu zake, kuzuia kwao majeshi kusonga ili kuinusuru Palestina kutoka kwenye makucha ya Mayahudi wahalifu, uingiliaji wa wazi wa Magharibi katika dini yake na uadilifu wake, na jaribio la kuulazimisha kulishuhudia umbile la Kiyahudi, na kuuacha na chaguo kati ya uhalalalishaji mahusiano au kifo. Mandhari na matukio haya yote yameufanya utambue kwamba bila ya utawala wa Uislamu, utabakia kukoloniwa, kulengwa, na kudhalilishwa. Kukinaika kwake kwa haja ya dola ya Khilafah kumeimarishwa, na kwa hakika, Khilafah imekuwa ni kiu yake.
Hizb ut Tahrir / Wilayah Pakistan: Pongezi kwa Mnasaba wa Ujio wa Idd ul-Fitr 1446 H
Hizb ut Tahrir / Wilayah Syria: Pongezi kwa Mnasaba wa Ujio wa Idd ul-Fitr Al-Mubarak 1446 H
Pongezi za wabebaji da’wah miongoni mwa mashababu wa Hizb ut Tahrir kutoka kote ulimwenguni kwa Umma wa Kiislamu kwa mnasaba wa ujio wa Idd ul-Fitr Al-Mubarak 1446 H