Watawala wa Waislamu Wameshikana Mkono kwa Mkono na Marekani na Mayahudi Kupitisha Mipango Yao, Na kwa Kauli na Shutma Tupu Pamoja na Waislamu
- Imepeperushwa katika Afisi Kuu ya Habari
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Umbile la Kiyahudi linaendelea kutekeleza jinai zake dhidi ya Gaza, Ukingo wa Magharibi, Lebanon na Syria; kumuua limtakaye, kupiga mabomu popote lipendapo, kubomoa nyumba na vituo, kujenga makaazi, na kuwaandama watu katika nyumba na ardhi zao, huku watawala wa Waislamu wakiendelea na misimamo yao ya fedheha ya kula njama na kurahisisha mambo kwa ajili yake, wakicheza dori ya mwangalizi na mwandishi wa habari anayeripoti habari na kutoa maoni yake kwa misemo isiyozuia wala kutibua njama.



