Jumanne, 29 Rabi' al-thani 1447 | 2025/10/21
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Maadhimisho ya Mwaka wa Pili wa Operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa Matunda Yaliyonyunyiziwa kwa Damu Safi

Tarehe 7 Oktoba iliadhimisha mwaka wa pili wa operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa. Miaka miwili kamili imepita tangu umbile nyakuzi kulenga watu wetu mjini Gaza, likiwafungulia mpangilio wa kuua, kuhamisha, na njaa, na kutumia viwango vya juu vya ushenzi na ukatili dhidi yao. Kwa hivyo ni nini kimebadilika kwa vita hivi vya dhulma?!

Soma zaidi...

Kongamano la Sharm El-Sheikh Ni Kutangaza Ushindi Juu ya Ummah, Kumakinisha Utiifu, na Kuimarisha Ukaliaji wa Kimabavu

Baada ya Trump kutangaza ushindi yeye na mfuasi wake, umbile la Kiyahudi, walioupata katika hotuba yake mbele ya Knesset. Ushindi huu ulipatikana dhidi ya raia wasio na silaha, wakiwemo wanawake, watoto, na wazee, pamoja na miti na mawe, Muuaji wa Gaza alielekea kwenye kongamano hilo liliopangwa na kibaraka wake nchini Misri, Sisi, ambapo aliwaalika wale wote waliokula njama dhidi ya ardhi iliyobarikiwa.

Soma zaidi...

Kuongezeka kwa Umwagaji damu kwenye Mpaka wa Pakistan na Afghanistan na Kushindwa kwa Pande zote mbili Kushikamana na Hukmu ya Mwenyezi Mungu

Mbali na sera ya “kujizuia” iliyotabanniwa na serikali za sasa za Pakistan na Afghanistan kwa maadui wa Umma – Mayahudi, Mabaniani, na Waamerika – Pakistan pamoja na Afghanistan zilitangaza kwamba makumi ya wanajeshi kutoka kila upande walikuwa wameuawa katika mapigano ambayo yalizuka kwenye mpaka wao wa pamoja. Makabiliano hayo yalianza mnamo Jumamosi jioni kwa operesheni iliyoanzishwa na vikosi vya Taliban, na kusababisha Islamabad kuapa kutoa jibu kali. Kabul, kwa upande wake, ilitangaza kuwa vikosi vyake vilifanya operesheni dhidi ya vikosi vya usalama vya Pakistan ili kulipiza kisasi kwa ukiukaji wa mara kwa mara na uvamizi wa anga unaofanywa na jeshi la Pakistan katika eneo la Afghanistan.

Soma zaidi...

Tanzia ya Mbebaji Ulinganizi Mirza Ahmadov Miraziz

Kwa huzuni na majonzi makubwa, tunaomboleza kuondokewa na mwana wetu mwengine madhubuti na mchamungu, na hatumtakasi yeyote mbele ya Mwenyezi Mungu. Ndugu yetu Mirza Ahmad Mir Aziz alifariki dunia siku ya Ijumaa, 10 Oktoba 2025, na swala ya janaza iliswaliwa kwa ajili yake jana, Jumamosi. Mir Aziz alizaliwa Tashkent mwaka wa 1970. Alikuwa mmoja wa maelfu ya Waislamu wenye ikhlasi na ujasiri ambao waliitikia wito wa Hizb ut Tahrir kwa watu wa Uzbekistan kufanya kazi ya kuregesha mfumo kamili wa maisha wa Kiislamu.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Tunisia: Kikao cha Majadiliano “Mradi wa Ukombozi... Katika Mizani ya Hukmu za Sheria ya Kiislamu”

Mnamo Jumapili, 12 Oktoba 2025, Hizb ut Tahrir/Wilayah ya Tunisia iliandaa kikao cha mazungumzo kwa kichwa “Mradi wa Ukombozi... Katika Mizani ya Hukmu za Sheria ya Kiislamu” katika eneo la Kairouan. Kikao hicho kilihudhuriwa na idadi kubwa ya wakaazi wa eneo hilo.

Soma zaidi...

Kadri Wakati Unavyosonga Mbele, Thaqafa ya Kimagharibi Unarudi Nyuma

Mnamo tarehe 9 Oktoba, Gazeti la ‘the Guardian’ liliripoti kwamba mkuu wa shirika la kutoa misaada la Waislamu wa Uingereza Shaista Gohir, alikuwa na 'wasiwasi mkubwa' huku uhalifu wa chuki dhidi ya Uislamu ukiongezeka kwa theluthi moja kulingana na takwimu za hivi punde za serikali. Alisisitiza kuwa hata takwimu hizi zinazosumbua pengine ni ‘sio halisi’ kwani matukio mengi hayaripotiwi.

Soma zaidi...

Kuangazia Njia ya Shariah Inayofuatwa na Hizb ut Tahrir Kusimamisha Dola

Uhalisia wa sasa wa Waislamu leo ​​ni sawa na awamu ya Makka ya ujumbe wa Mtume, kwani wanaishi katika “Dar ul-Kufr” (Nyumba ya Ukafiri) kutokana na kutawaliwa na sheria zisizokuwa zile zilizoteremshwa na Mwenyezi Mungu (swt) na neno “Dar” ni istilahi ya kifiqhi iliyofafanuliwa kwa kina katika vitabu vya fiqh (Fiqh ya Shariah). Hili linalazimu kufuata njia ya mabadiliko ya Makka. Mtume (saw) alifuata hatua tatu kuu katika njia yake ya kusimamisha dola ya Kiislamu.

Soma zaidi...

Ujumbe kwa Watu Wetu mjini Gaza

Enyi watu wa Gaza: nyinyi leo mmesimama katika msimamo wa Mitume (as) na watu wema, mkisimama kidete kwa ajili ya haki dhidi ya dhulma. Kila dhiki, kila jeraha, kila Shahidi ni riziki katika mizani yenu ya mema, na kunyanyua daraja yenu. Ukuruba wa Mwenyezi Mungu uko pamoja nanyi, na ushindi wake uko karibu, basi subirini na muwe thabiti, na furahieni kwa yale aliyoyaahidi Mwenyezi Mungu (swt) ya bustani na daraja, na heshima ya dunia ambayo hupatikana kwa uthabiti na kujitolea mhanga.

Soma zaidi...

Janga la Gabes, Mhasiriwa wa Machaguo ya Dola ya Kisasa

Maandamano ya watu wa Gabes kusini mwa Tunisia yanaendelea kwa sababu ya sumu inayotolewa kutoka kwa tata ya kemikali, ambayo imegeuza jiji hilo kuwa eneo lililoathirika kimazingira na kiafya, na kuathiri moja kwa moja afya ya wakaazi wa Gabes na mali asili yake. Saratani na magonjwa ya kupumua yameenea, na suala hilo limefikia hata visa vya kukosa hewa miongoni mwa wanafunzi. Miongo kadhaa ya ahadi za uongo na kupuuzwa kwa makusudi kumeifanya Gabes kuwa ishara ya kutengwa na uchafuzi wa mazingira, kwani utajiri wa phosphate umegeuka kutoka kuwa baraka hadi laana kwa sababu ya sera za serikali ya kisasa, ambayo ilichagua faida ya haraka na maslahi ya makampuni makubwa kwa gharama ya afya ya watu na haki yao ya maisha bora.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu