Jumanne, 29 1448 | 2026/06/16
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Pongezi kutoka kwa Amiri wa Hizb ut Tahrir, Mwanachuoni Mkubwa Ata Bin Khalil Abu Al-Rashtah, kwa Waislamu kwa Jumla na Mashababu (Wanachama wa Hizb) Hasa kwa Mnasaba wa Sikukuu ya Idd al-Adha 1447 H Sawia na 2026 M

Wapendwa ndugu na dada: Idd hii inakuja huku uvamizi wa Mayahudi, unaoungwa mkono na Amerika na silaha zake, ukiendelea dhidi ya Gaza (Hashim) na Palestina yote. Watawala katika nchi za Kiislamu wanaangalia kinachoendelea, wakiwahesabu mashahidi (shuhadaa) na kuwaita wafu! Na bora zaidi kati yao ni wale wanaopatanisha kana kwamba hawaegemei upande wowote, lakini wako karibu zaidi na Mayahudi!

Soma zaidi...

Watawala wa Pakistan Wanatoa Kile Ambacho Marekani Imekuwa Ikikiota Siku Zote na Kuiondoa Katika Hatari Yake

Rais wa Marekani Donald Trump alitangaza mnamo Jumamosi, Mei 23, 2026, kwamba makubaliano na Iran yalikuwa karibu kukamilika, akisema, “Makubaliano yamejadiliwa kwa kiasi kikubwa, yanakaribia kukamilika.” Aliongeza kwamba alikuwa na “wito mzuri sana” na viongozi na maafisa nchini Saudi Arabia, Imarati, Qatar, Pakistan, Uturuki, Misri, Jordan, na Bahrain kuhusu Iran. Hii ilikuja saa chache baada ya afisa mmoja wa Iran kufichua kwa Al Jazeera kwamba mkataba wa maelewano ulikuwa umefikiwa na mpatanishi wa Pakistan, lakini kwamba Tehran ilikuwa ikisubiri majibu ya Marekani. Afisa huyo aliashiria kwamba Mkuu wa Jeshi la Pakistan Asim Munir alipangwa kutangaza mkataba huo wa maelewano jijini Tehran, lakini alikuwa ameondoka ili kufanya uratibu pamoja na Washington

Soma zaidi...

Kama Hujui, Hilo Ni Janga; Lakini Kama Unajua, Basi Janga Ni Kubwa Zaidi!

Wakati wanasiasa wa Iraq na kambi zao wakigombea nyadhifa, matukio yanajitokeza ambayo yanathibitisha tena kwamba nchi hii si tu kwamba haina ubwana, bali pia kwamba maamuzi yake, ardhi, na anga zake vinakiukwa waziwazi na mtu yeyote na kila mtu. Amri za Marekani zinatolewa waziwazi na bila kuficha kuhusu uundaji wa serikali. Uingiliaji kati wa Iran kupitia kamanda wa Kikosi cha Quds cha Iran na ziara zake za mara kwa mara pia ni uko hadharani na haujafichika. Suala jengine lilikuwa ni ufichuzi wa ‘New York Times’ wa kuwepo kwa kambi mbili za kijeshi za umbile la Kiyahudi wakati wa vita vya Marekani dhidi ya Iran: moja katika Jangwa la Al-Nukhaib na nyingine katika jangwa la magharibi.

Soma zaidi...

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan Ulikutana na Kiongozi (Amir) wa Makabila ya Hausa Mjini Port Sudan

Mnamo Alhamisi, 21/5/ 2026, ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir/ Wilayah ya Sudan, ukiongozwa na Mkuu wa Kamati Kuu ya Mawasiliano ya Hizb ut Tahrir/ Wilayah ya Sudan, Ustadh Nasser Ridha, akifuatana na Ustadh Abdullah Ismail, Mratibu wa Kamati ya Mawasiliano, walikutana na Amiri wa makabila ya Hausa katika Wilayah ya Port Sudan, Ustadh Salih Abdul Rahman, nyumbani kwake.

Soma zaidi...

Msamaha Jumla; Uadilifu Nusu ni Dhulma, na Hakuwezi Kuwa na Msamaha Jumla wa Kibaguzi!

Mnamo Mei 19, 2026, tovuti ya Lebanon Debate ilichapisha kile ilichokiita toleo la mwisho lililorekebishwa la sheria ya msamaha wa jumla. Ilionekana wazi kwamba sheria hii haikuwa ya jumla, ikiwajumuisha raia wote, bali iliundwa kwa vipimo vya kimadhehebu, ubaguzi, na hesabu finyu, zisizo na uwazi. Inaonyesha mwendelezo wa enzi ya dhulma iliyowekwa na utawala wa Assad mhalifu na wafuasi wake nchini Lebanon, na mtazamo unaokataa kuhama kutoka wazo la udhalimu hadi wazo la haki na usawa. Zaidi ya hayo, ukiukwaji wa kisheria uliibuka katika kuingiliwa kwa kimabavu wakati wa uandishi wa sheria ya msamaha wa jumla! Ni chini ya kanuni gani za kisheria au mifumo ya kimataifa ambapo kitu kama hicho kipo?! Ni katika chombo hiki dhaifu tu, ambacho kinathibitisha kila siku kwamba ni mkusanyiko tu wa madhehebu ambayo nchi imeundwa, si nchi ya kawaida ambapo madhehebu huishi pamoja kama mataifa mengine, mradi tu yachague mfumo wa utawala unaoegemea msingi wa utunzaji wa haki wa raia wake, usio na ukandamizaji na unyanyasaji wa kiholela!

Soma zaidi...

Jibu la Swali: Mazungumzo ya Usaliti Kati ya Lebanon na Umbile la Kiyahudi

Jijini Washington, mazungumzo yalifanyika kati ya mabalozi wa Lebanon na umbile la Kiyahudi. Hii ilionekana kama mazungumzo ya kiwango cha juu cha amani, pamoja na makubaliano ya kusitisha mapigano ya siku kumi ambayo baadaye yaliongezwa hadi miezi mitatu mnamo Aprili 24, 2026. Hata hivyo, umbile la Kiyahudi linaendelea kuzidisha uchokozi wake, “jeshi la uvamizi lilitangaza kwamba lilifanya mfululizo wa mashambulizi usiku kucha likilenga zaidi ya maeneo hamsini kusini mwa Lebanon...” (Al-Jumhur, Mei 2, 2026). Je, nia, kama Trump alivyosema, ni amani kupitia nguvu? Basi watawala wa Lebanon wanawezaje kukubali mazungumzo haya ya usaliti ambayo waziwazi, na si kwa siri, yanamaanisha kupanda treni ya uhalalishaji mahusiano?

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu