Jumatano, 04 Rajab 1447 | 2025/12/24
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Kilio cha Haraka cha Msaada, Enyi Ummah wa Kiislamu!

Wanawake na watoto wa Gaza wanalilia msaada... wanawake na watoto wa Sudan wanalalamika... wanawake na watoto wa Uyghur huko Turkestan Mashariki wanateseka na kupiga kelele... Wanawake wa Kiislamu na watoto wao kila mahali wanapaza kilio baada ya kilio, wakiita: Je, kuna mtu yeyote wa kusaidia? Je, kuna mtu yeyote wa kuitikia wito? Je, kuna mtu yeyote wa kujibu?!

Soma zaidi...

Wakati Dola ya Kibaniani Inapozivua Niqab Kwenye Nyuso za Mabinti wa Kiislamu, Warithi wa Muhammad Bin Qasim Wako Wapi Ndani ya Jeshi la Pakistan?

Mnamo Jumatatu, 15 Disemba 2025, katika sherehe moja, Waziri Mkuu wa jimbo la India la Bihar, Nitish Kumar, aliichana niqab kutoka kwa daktari mmoja Muislamu, Nusrat Parveen. Baada ya kufanya hivyo, alicheka kana kwamba kuichana niqab hiyo kutoka kwa uso wa mwanamke wa Kiislamu ilikuwa ni mzaha. Ilhali, Mayahudi walipomfunua mwanamke mmoja wa Kiislamu na kumdhihaki hali yake, Swahaba aliyekuwepo alimuua Myahudi huyo; na Mayahudi walipomuua shahidi Swahaba huyo baadaye, Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw) alizingira kabila lote, akawakamata na kuwafunga wote, na alikuwa akitoa hukumu juu yao, lakini hatimaye, baada ya maombezi, adhabu ndogo ilitolewa: kabila lote lilifukuzwa Madina. Lakini leo hakuna dola ya kulinda heshima ya Dkt. Nusrat Parveen na kumpa Baniani huyu muovu, Nitish Kumar, funzo.

Soma zaidi...

Tafsiri Al-Baqarah [Muhkam na Mutashabiha]

Jambo muhimu katika sayansi ya Quran linalohusiana na tafsiri ya aya za Mwenyezi Mungu, mbali na maana halisi na ya kimajazi, ni kuwepo kwa yaliyo wazi na yaliyo na utata katika Kitabu. Mwenyezi Mungu (saw) amesema, “Yeye ndiye aliye kuteremshia Kitabu hichi. Ndani yake zimo Aya muhkam, zenye maana wazi. Hizo ndizo msingi wa Kitabu hichi. Na ziko nyengine za mifano. Ama wale ambao nyoyoni mwao umo upotovu wanafuata zile za mifano kwa kutafuta fitna, na kutafuta maana yake; na wala hapana ajuaye maana yake ila Mwenyezi Mungu. Na wale wenye msingi madhubuti katika ilimu husema: Sisi tumeziamini, zote zimetoka kwa Mola wetu Mlezi. Lakini hawakumbuki hayo isipo kuwa wenye akili.” 

Soma zaidi...

Mwangwi wa Himaya: Uharamia wa Marekani Pwani ya Venezuela

Mnamo tarehe 10 Disemba 2025, Marekani ilimkamata nahodha wa meli ya mafuta kutoka pwani ya Venezuela, ikipanda meli hiyo na kuelekeza shehena yake ya takriban mapipa milioni 1.8 ya mafuta ghafi ya Venezuela hadi Marekani chini ya kibali cha vikwazo vya Marekani ambacho kilikuwa kinakaribia kuisha. Maafisa wa Marekani walidai hatua hii ya utekelezaji ililenga kuadhibu ukiukaji wa vikwazo vya muda mrefu vinavyohusiana na madai ya usafirishaji haramu wa mafuta. Serikali za Venezuela na Cuba zililaani hatua hiyo kama “wizi wa waziwazi” na “uharamia,” huku Cuba ikiuita “ugaidi wa baharini” ikiathiri mahitaji yake ya nishati. Usumbufu huo umeacha zaidi ya mapipa milioni 11 ya mafuta ya Venezuela yamekwama baharini, huku meli za mafuta na wafanyibiashara wakitathmini upya hatari za kubeba mafuta ghafi ya Venezuela, na kulazimisha punguzo kubwa na mazungumzo ya mikataba na wanunuzi muhimu kama vile China.

Soma zaidi...

Yaonekana Mazuri, lakini Ndani Hamna Kitu!

Rais Erdoğan, katika hotuba yake baada ya mkutano wa baraza la mawaziri, pia aligusia mwelekeo wa Uturuki wa sera ya kigeni, akisema: “Uturuki imeipa dunia funzo katika haki za binadamu kupitia juhudi zake zinazolenga amani na haki katika maeneo yaliyolowa damu na machozi—Gaza, Syria, Somalia, na Libya.” Alisisitiza kwamba taifa hilo limeunganishwa kwa fungamano lisilotikisika, pasi na tofauti kati ya Mturuki, Mkurdi, Muarabu, Alevi, au  Caucassian. (Mashirika, 15.12.2025)

Soma zaidi...

Ubepari kama Chanzo Kikuu cha Maafa ya Mafuriko huko Sumatra

Kimbunga Senyar kilikuwa kichocheo tu; kiwango cha uharibifu nchini Indonesia kinaonyesha miongo kadhaa ya usimamizi mbaya wa ikolojia. Sumatra imepoteza mamilioni ya hekta za misitu, ikidhoofisha maeneo ya maji huko Aceh, Sumatra Kaskazini, na Sumatra Magharibi. Maeneo ya tambarare yalikaushwa maji kwa ajili ya mashamba makubwa, na kusababisha kupungua kwa ardhi na kugeuza vizuizi vya maji asilia kuwa mabonde ya mafuriko. Makaazi ya haraka katika maeneo tambarare ya mafuriko, pamoja na usimamizi dhaifu wa matumizi ya ardhi, yaliongeza athari. Mvua kali ilipofika, mandhari haikuwa na uwezo uliobaki wa kuhimili. Maafa yanaonyesha kwamba muundo wa maendeleo wa Indonesia—unaoendeshwa na uchimbaji na usimamizi duni wa mazingira—umefanya hali mbaya ya hewa kuwa hatari zaidi kuliko inavyopaswa kuwa. (news.mongabay)

Soma zaidi...

Enyi Waislamu: Kufunga Vyumba vya Ibada ni Shambulizi kwa Uislamu na Lazima Kukabiliwe kwa Upinzani Mkali, wa Pamoja wa Kisiasa

Baada ya mwelekeo hasi wa kisiasa kwenye vyumba vya ibada, idara ya Chuo Kikuu cha Copenhagen iliamua mwishoni mwa Novemba kufunga kile kinachoitwa “vyumba vya utulivu,” ambavyo Waislamu walikuwa wakivitumia kwa zaidi ya miaka ishirini, bila matatizo yoyote, na wanafunzi na wafanyikazi kuswali swala za kila siku. Uamuzi huu kwa mara nyingine tena umezua mjadala kuhusu vyumba hivi na kuhusu kama kunapaswa kuwepo na nafasi kwa Waislamu kutekeleza swala zao katika taasisi za elimu.

Soma zaidi...

Unyanyasaji wa Kimpangilio wa Kijinsia Dhidi ya Wanawake wa Sudan Hautoi Jibu lolote kwa Kukosekana kwa Dola Inayojali Heshima ya Mwanamke Mwislamu

Mnamo Alhamisi tarehe 11 Disemba, shirika, ‘The Strategic Initiative for Women in the Horn of  Africa’, liliripoti kuwa limerekodi karibu matukio 1300 ya unyanyasaji wa kijinsia dhidi ya wanawake katika majimbo 14 nchini Sudan tangu vita vianze nchini humo mnamo Aprili 2023, huku Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) vikilaumiwa kwa 87% ya visa hivi. Lilielezea unyanyasaji wa kijinsia dhidi ya wanawake ukitumika kama silaha ya kimfumo katika mzozo huo, likisema “umeenea, unarudiwa rudiwa, unakusudiwa na mara nyingi unalenga”. Ubakaji ulichangia robo tatu ya matukio yaliyorekodiwa, huku visa 225 vikihusisha watoto, baadhi wakiwa na umri wa miaka 4. Matukio yalitokea majumbani, maeneo ya umma na pia yalijumuisha kizuizini cha muda mrefu cha wanawake ambao waliteswa, kubakwa na genge na ndoa za kulazimishwa. Mnamo Jumapili tarehe 7 Disemba, vikundi vya matibabu vya Sudan viliripoti kwamba watoto na wanawake kadhaa walinyanyaswa kingono na kubakwa walipokuwa wakikimbia kukamatwa kwa El Fasher huko Darfur na RSF Oktoba hii.

Soma zaidi...

Je, Vikosi vya Kiislamu vya Jeshi la Pakistan Sasa, Chini ya Uongozi wa Jenerali wa Marekani, Vitawalinda Mayahudi na Kuupokonya Silaha Upinzani wa Palestina?

Gazeti la Dawn liliripoti kwenye tovuti yake mnamo tarehe 13 Disemba, 2025 kwamba majeshi ya Waislamu huenda yakatumwa kuanzia mwezi ujao kwa ajili ya “Kikosi cha Kimataifa cha kuleta Utulivu” mjini Gaza. Hapo awali, mtawala kibaraka wa Marekani Shehbaz Sharif alikuwa tayari ametoa idhini “ya kikanuni” kwa kutumwa kwa vikosi vya Pakistan huko Gaza. Hata hivyo, wakiogopa upinzani mkali wa umma, watawala wa Waislamu mmoja baada ya mwengine wamekuwa wakionyesha kutokuwa na msaada kwao mbele ya Amerika. Hivyo sasa shetani Trump na wafuasi wake, watawala wa Waislamu, wanaunda njama mpya za kutumia vikosi vyetu vya Waislamu vya mujahid kuwalinda Mayahudi na kuwanyang'anya silaha Hamas na vikosi vyengine vya upinzani vya Palestina.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu