Ijumaa, 20 Rajab 1447 | 2026/01/09
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Dola ya Kitaifa ndiyo Kikwazo Kikubwa Zaidi katika Kulinda Heshima na Maisha ya Waislamu Iwe nchini India au Gaza

Waziri wa Mambo ya Nje na Naibu Waziri Mkuu Ishaq Dar alilaani vikali tukio ambapo Waziri Mkuu wa Bihar Nitish Kumar alivua hijabu ya mwanamke wa Kiislamu Nusrat Parveen katika hafla ya serikali, akilitaja kuwa ‘la kuchukiza sana’. Dar alielezea tukio hilo kama la aibu, akisema lilionyesha haja ya haraka ya kulinda haki za wachache na kupunguza wimbi linaloongezeka la chuki dhidi ya Uislamu.

Soma zaidi...

Ukandamizaji Unaoongezeka wa Marekani dhidi ya Mashirika ya Kiislamu - Toleo la Texas

Katika hatua ya kushangaza wiki hii, Gavana wa Texas Greg Abbott alitangaza Baraza la Mahusiano ya Kiislamu na Kiamerika (CAIR) na Ikhwan al-Muslimin kama “mashirika ya kigaidi ya kigeni.” Tangazo lake linaharamisha makundi haya kumiliki mali huko Texas na kuidhinisha hatua za kisheria za serikali dhidi ya vyama vinavyohusiana nayo. Ingawa Abbott aliweka uamuzi huo kama msimamo dhidi ya “misimamo mikali,” hatua hiyo inawakilisha ongezeko kubwa la ulengaji unaoendelea wa mashirika ya Kiislamu na inaangazia mgogoro mkubwa wa uhuru wa kuzungumza, ukandamizaji wa serikali, na unafiki katika jinsi Amerika inavyowatendea raia wake Waislamu.

Soma zaidi...

Kifo cha Imam Fouad Saeed Abdulkadir: Pindi Hifadhi Inapogeuka Kuwa Mkasa

Idara ya Uhamiaji na Forodha ya Marekani (ICE) imethibitisha kifo cha Fouad Saeed Abdulkadir, raia wa Eritrea mwenye umri wa miaka 46, ambaye alifariki tarehe 14 Disemba akiwa kizuizini mwa ICE katika Kituo cha Ushughulikiaji cha Moshannon Valley huko Pennsylvania. Kulingana na ICE, Imam Abdulkadir anaripotiwa kupata maumivu ya kifua na kupokea uangalizi kutoka kwa wafanyikazi wa matibabu na huduma za matibabu za dharura. Kifo chake, mojawapo ya vifo kadhaa vilivyoripotiwa katika vituo vya ICE, bado kinachunguzwa na kimeongeza uchunguzi wa hali za uzuizi na upatikanaji wa huduma za afya za kutosha kwa wafungwa.

Soma zaidi...

Kipindi cha Tarique Rahman: Purukushani ya Kisiasa Kutoka kwa Mfumo wa Kisekula Uliovunjika

Huku Bangladesh ikiingia katika awamu muhimu ya kabla ya uchaguzi, kutangazwa kwa kurudi kwa Tarique Rahman, mwana wa Waziri Mkuu wa zamani wa Bangladesh Khaleda Zia na kaimu Mwenyekiti wa Chama cha Kizalendo cha Bangladesh (BNP), kumesababisha wimbi linalotabirika la umaarufu inaozingatia shakhsiya ya mtu. Simulizi hii, iliyokuzwa kwa ukali na chama chake, inamwakilisha kama suluhisho la pekee kwa changamoto za taifa. Lazima tuone hili kwa jinsi lilivyo: udanganyifu mkubwa wa kisiasa ambao unaficha kwa hatari uhalisia msingi wa mamlaka na mfumo wa leo.

Soma zaidi...

Taarifa ya Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilaya ya Sudan katika Mkutano na Waandishi wa Habari Wenye Kichwa: “Usimamizi wa Amerika wa Mgogoro wa Sudan Unazidisha Majeraha na Kugawanya Nchi”

Katika taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na Naibu Katibu wa Wizara ya Mambo ya Nje, Balozi Muawiya Othman, kufuatia ziara ya Mwenyekiti wa Baraza la Mpito la Utawala na Kamanda wa Jeshi, Luteni Jenerali Burhan, nchini Saudi Arabia, Muawiya alisema mnamo Jumatatu jioni, 15/12/2025: “Rais alielezea shukrani zake kamili kwa azimio la Rais wa Marekani Donald Trump la kushiriki katika juhudi za kufikia amani na kukomesha vita nchini humo, kwa ushiriki wa Ufalme wa Saudi Arabia. Mheshimiwa alithibitisha nia ya Sudan kufanya kazi na Rais Trump, Waziri wake wa Mambo ya Nje, na Mjumbe wake Maalum wa Amani nchini Sudan, ili kufikia lengo hili zuri bila shaka.”

Soma zaidi...

Mwaliko wa Kuhudhuria Mkutano na Waandishi wa Habari

Tunafurahi, katika Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan, kuwaalika wataalamu wa vyombo vya habari, wanasiasa, na wale wanaopenda masuala ya umma kuhudhuria mkutano na waandishi wa habari ambapo Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan atazungumza chini ya kichwa: “Usimamizi wa Amerika wa Mgogoro wa Sudan: Kuongeza Majeraha na Kugawanya Nchi”

Soma zaidi...

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Wakutana na Kiongozi wa Al-Ikhwan Al-Muslimina Hassan Abdel Hamid

Jana, Ijumaa 19/12/2025, ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan, ukiongozwa na Ustadh Nasser Ridha, Mkuu wa Kamati Kuu ya Mawasiliano ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan, akifuatana na Ustadh AbduAllah, Mratibu wa Kamati hiyo, ulikutana na Ustadh Hassan Abd Al-Hameed kiongozi katika Al-Ikhwan Al-Muslimina nchini Sudan.

Soma zaidi...

Vyombo vya Usalama Vyawakamata Mashababu wa Hizb ut Tahrir kwa Kutoa Wito wa Kutibua Mpango wa Amerika wa Kutenganisha Darfur

Kikosi kutoka kwa vyombo vya usalama kiliwakamata Mashababu watano (wanachama) wa Hizb ut Tahrir katika mji wa Al-Shawak, ambao ni: Othman Al-Amin Kanda, Hassan Al-Amin Kanda, Muhammad Thamin Adam, Ahmad Babikr, na Al-Amin Abdullah. Hili lilikuja kufuatia Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan kufanya kisimamo mbele ya Msikiti wa Kale huko Al-Shawak, ambapo Sheikh Othman Al-Amin Kanda, mwanachama wa Hizb ut Tahrir, alihutubia hudhuri ya watu mashuhuri wa eneo hilo na umma kwa jumla. Katika hotuba yake, alielezea hatari ya mpango wa Marekani unaotaka kuigawanya Sudan kwa kuikata Darfur, akiwapa wale waliohudhuria jukumu la Kisharia linalofanya umoja wa Ummah na umoja wa dola kuwa suala nyeti. Baadhi ya watu mashuhuri walishiriki kwa kutoa kauli zinazothibitisha msimamo wao na pamoja na hizb ili kuzuia mpango wa kujitenga.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu