Jumapili, 02 Rajab 1447 | 2025/12/21
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Bajeti za Jordan Ni Nakala Zinazorudiwa katika Ufisadi Wao na Kuzishughulikia Kupitia Madeni Kuna Wiana na Dori ya Kiutendaji ya Serikali na Haijali Uchungaji wa Mambo ya Watu

Serikali ilikadiria, katika Rasimu ya Sheria ya Bajeti Kuu ya mwaka 2026, mapato ya umma yangekuwa takriban dinari bilioni 10.931, 75% kati yake yakiwa ni kutokana na kodi, na dinari milioni 735 kutoka kwa ruzuku za kigeni. Waziri wa Fedha alisema kwamba kiasi cha matumizi ya sasa ni dinari milioni 11,456, huku matumizi makuu yakifikia dinari milioni 1,600 pekee. Kuhusu nakisi inayotarajiwa kwa mwaka 2026, inakadiriwa kufikia takriban 4.6% ya Pato la Taifa.

Soma zaidi...

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Wamzuru Sheikh wa Twarika ya Sammaniyah katika Mji wa Wad Madani

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan ulitembelea Sheikh wa Twarika ya Sammaniyah katika Jimbo la Al-Jazirah jana, Jumamosi, 13/12/2025. Ujumbe huo uliongozwa na Ustadh Mahdi Muhajir, mwanachama wa Hizb ut Tahrir, akifuatana na Ustadh Abdulaziz Ibrahim, mwanachama wa Hizb ut Tahrir, na mhandisi Walid Kamil.

Soma zaidi...

Je, Vituo vya Mafuta Vina Thamani Zaidi na Hadhi Kubwa Zaidi kuliko Watu?!

Imeripotiwa katika habari kwamba Vikosi vya Ulinzi vya Wananchi wa Sudan Kusini vilianza kupeleka vikosi vyake kulinda Uwanja wa Mafuta wa Heglig kufuatia makubaliano ya pande tatu kati ya Mwenyekiti wa Baraza la Uhuru la Utawala la Sudan, Abdel Fattah al-Burhan, Rais wa Sudan Kusini, Salva Kiir Mayardit, na kamanda wa Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF), Mohamed Hamdan Dagalo. Mkuu wa Majeshi ya Wananchi wa Sudan Kusini, Paul Nang, alielezea katika taarifa kwa vyombo vya habari kutoka ndani ya uwanja wa mafuta wa Heglig kwamba makubaliano hayo yalibainisha kuondolewa kwa jeshi na kuondoka kwa Vikosi vya Msaada wa Haraka kutoka eneo hilo, na alithibitisha kwamba lengo la makubaliano hayo lilikuwa kuhakikisha kwamba hakuna hujuma yoyote inayotokea kwenye vituo vya mafuta!!

Soma zaidi...

Chuo Kikuu cha Al-Quds Kinafanya Kongamano kwa Ufadhili wa Magharibi na Programu Iliyoundwa na Magharibi Chini ya Kauli Mbiu “Usawa wa Kijinsia na Uwezeshaji wa Wanawake”

Mnamo Jumanne, 2 Disemba 2025, Kitivo cha Sheria katika Chuo Kikuu cha Al-Quds – Abu Dis kilizindua kongamano la kimataifa lililopewa kichwa “Usawa wa Kijinsia na Uwezeshaji wa Wanawake: Changamoto, Masuluhisho, na Mbinu Bora katika Eneo la Mediterania,” kwa ushirikiano na Wizara ya Masuala ya Wanawake ya Palestina, Jukwaa la Mashirika Yasiyo ya Kiserikali ya Kupambana na Ukatili Dhidi ya Wanawake, Shirika la Idadi ya Watu la Umoja wa Mataifa (UNFPA), na Chuo Kikuu cha Perugia, Italia, kwa usaidizi wa ushirikiano wa Italia.

Soma zaidi...

DVD “Amali za Kimataifa za Hizb ut Tahrir katika Kuinusuru Gaza!”

Kwa kuzingatia matendo ya kishujaa ya mujahidina katika ardhi iliyobarikiwa ya Palestina mnamo 7 Oktoba 2023, chini ya kauli mbiu ya “Kimbunga cha Al-Aqsa,” dhidi ya umbile nyakuzi la Kizayuni, ambalo limeendelea katika uvamizi wake dhidi ya Msikiti uliobarikiwa wa Al-Aqsa na kuzingirwa kwake na mashambulizi ya mabomu yanayoendelea ya Ukanda wa Gaza kwa zaidi ya miaka 19, umbile hilo limefichuliwa jinsi lilivyo: umbile la kuchukiza, msingi wake ni dhaifu kuliko utandu wa buibui.

Soma zaidi...

Tanzia ya Mbebaji Ulinganizi Miongoni mwa Mashababu wa Hizb ut Tahrir Mwalimu Ustadh Ahmad Muhammad Al-Saharin (Abu Khalid)

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir/Wilayah Jordan inaomboleza kifo cha mwalimu mtukufu, Ustadh Ahmad Muhammad Al-Saharin (Abu Khalid), mwanachama wa Hizb ut Tahrir, aliyefariki Jumatano, 10 Disemba 2025, akiwa na umri wa miaka 79. Alikuwa miongoni mwa wabebaji da’wah wa muda mrefu na anayejulikana sana huko Tafila.

Soma zaidi...

Licha ya Serikali ya Jordan Kuwaangusha Watu wa Gaza na Kujisalimisha Kwake kwa Mpango wa Trump, Vyombo Vyake vya Usalama Vyamkamata Mmoja wa Wanachama wa Hizb ut Tahrir

Serikali ya Jordan inaendelea kwa kiburi katika dhambi na uvamizi, licha ya kuwaangusha watu wa Gaza, na kwa hakika ushirikiano wake na umbile la Kiyahudi katika vita vya mauaji ya halaiki ambavyo imepigana katika Ukanda wa Gaza, kwa kulipatia njia za uwezeshaji na uhai. Haikusita kumbariki Trump mhalifu katika kuifilisi kadhia ya Palestina kwa kuhudhuria kile kinachoitwa “Baraza la Amani” ili kuwa shahidi wa uongo wa mpango wa Trump wa udhibiti juu ya ardhi za Waislamu na kwa kupotea kwa Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Uturuki: Amali ya Umma “Moto mjini Gaza Hautazima, na Dhulma Haitakwisha!!

Katika kukabiliana na mauaji ya kikatili yanayoendelea (mauaji ya halaiki) yaliyofanywa na umbile halifu la Kizayuni dhidi ya Waislamu wasio na ulinzi katika Ukanda wa Gaza kwa zaidi ya miaka miwili, ambayo yamesababisha kuuawa shahidi, kujeruhiwa, na kutoweka kwa Waislamu zaidi ya 220,000 hadi sasa, Hizb ut Tahrir / Wilayah Uturuki iliandaa usomaji wa taarifa kwa vyombo vya habari katika miji kumi mikubwa chini ya kichwa: “Moto Hautazima Gaza, na Dhulma Haitakwisha!”

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu