Ijumaa, 03 Jumada al-awwal 1447 | 2025/10/24
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Mayahudi Wanachimba Makaburi kwa Mikono Yao Wenyewe Huku Watawala wa Waarabu na Waislamu Wakiuzuia Ummah wa Kiislamu Usiwazike

Katikati ya milipuko ya mabomu na makombora ya umbile la Mayahudi, ikinyesha moto juu ya vichwa vya watu wetu mjini Gaza, ambapo wanalenga ghorofa za makaazi, vyuo vikuu, shule, hospitali na misikiti, hata kuangusha mahema chini, kiasi kwamba mifupa ya watoto na nyama zao inachanganyika na vifusi, “mkutano wa aibu na waovu” ulikusanyika na kufanywa. Ilikuwa ni mkutano wa kilele wa watawala Ruwaibidha duni, waovu kutoka miongoni mwa Waarabu na wasio Waarabu.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan: Kisimamo cha Port Sudan kwa ajili ya Kufelisha Mpango wa Kuitenganisha Darfur

Kisimamo kilichofanywa na Hizb ut Tahrir/Wilayat Sudan ili kufelisha mpango wa kuitenganisha Darfur kilipokelewa kwa maingiliano makubwa, ikiwemo takbir, tahlil, na kuungwa mkono, pamoja na uhamasishaji wa vyombo vya habari na wa kisiasa mbele ya msikiti mkuu katika mji wa Port Sudan. Waumini walikusanyika baada ya swala ya Ijumaa mnamo 20 Rabi' al-Awwal 1447 H 12 Septemba 2025 M kwenye Msikiti Mkuu wa Port Sudan katika kisimamo kilichofanywa na Hizb ut Tahrir/Wilayat Sudan mbele ya Msikiti huo Mkuu kama sehemu ya kampeni ya Hizb kukwamisha mpango wa kuitenganisha Darfur.

Soma zaidi...

Sehemu za dhati za nchi Lazima Ziungane dhidi ya Sera ya Serikali ya Mpito ya Utiifu kwa Marekani Mkoloni Kafiri

Serikali ya mpito inaisaliti nchi kwa kuonyesha kusitasita kulinda Mipaka yetu kutoka kwa ‘Jeshi la Arakan’ linaloungwa mkono na Marekani, huku ikitamani kuwatumia wanajeshi wetu kwa Misheni ya Amerika nchini Ukraine. Kuanzia Disemba 2024 hadi Septemba 10, kundi la waasi lenye makao yake nchini Myanmar liliwateka nyara wavuvi 325 kutoka maeneo mengi kando ya Mto Naf na Ghuba ya Bengal. (bdnews24.com, Septemba 12, 2025). Kinaya ni kwamba, serikali ya Yunus ilipuuza Jeshi la Arakan (wakala wa Marekani) linalofanya kazi ndani ya ardhi yetu na kutishia watu wetu na ubwana wetu. Wakati huo huo, ilikuwa haraka kuisaidia Ukraine ili kumfurahisha bwana wake wa ubeberu mamboleo, Marekani.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Bangladesh Yawaalika Watu Wote Watambuzi, wakiwemo Wanasiasa, Wasomi, Waandishi wa Habari na Kizazi cha Vijana cha Nchi Kutazama Kongamano lake la Kisiasa Mtandaoni lenye Kichwa “Bangladesh 2.0: Utegemezi au Ukombozi?”

Hizb ut Tahrir / Wilayah Bangladesh, imeandaa kongamano la kisiasa la mtandaoni lenye kichwa “Bangladesh 2.0: Utegemezi au Ukombozi?” kutoa mwongozo kwa wananchi ili kufikia lengo kuu la Mapinduzi ya Julai 24. Munaalikwa kutazama kongamano hili ili kupata mwamko wa kisiasa na kuamua nini cha kufanya katika hatua hii ya kisiasa nchini.

Soma zaidi...

Umbile la Kiyahudi ndilo Tatizo Kubwa zaidi katika Nchi za Kiislamu Na Waungaji Mkono wake ndio Tatizo Kubwa Zaidi Duniani Ewe Trump!

Vyombo vya habari viliripoti taarifa ya Rais wa Marekani Donald Trump kuhusu Gaza, ambapo alisema, “Gaza ni tatizo kubwa kwa Israel na Mashariki ya Kati.” Hatujamsikia hata mmoja wa watawala wajinga wasio na maana (ruwaibidha) katika nchi za Kiislamu akimjibu, akimwambia kwamba umbile nyakuzi la Kiyahudi ndilo tatizo kubwa katika nchi za Kiislamu, na kwamba nyinyi ndio mnaliruzuku zana za kijeshi na msaada wa kisiasa na kiuchumi. Nyinyi ndio tatizo kubwa katika ulimwengu wote. Mfumo wenu wa kibepari ndiyo sababu ya masaibu ya dunia, na nyinyi ndio sababu ya kugawanyika kwa nchi za Kiislamu katika dola dhaifu na maumbo hafifi tiifu kwenu.

Soma zaidi...

“Kujitawala Wenyewe” kwa Mujibu wa Matakwa ya Wakoloni!

Ardhi zetu za Kiislamu zimekuwa jukwaa la kupigania mali na ushawishi kati ya Marekani na Ulaya. Cha kusikitisha ni kwamba, zana za mapambano haya ni baadhi ya wana wa Ummah, iwe katika serikali au vuguvugu la waasi, kama inavyotokea leo nchini Sudan, wakati wanaoshindwa pekee katika vita hivi ni watu wasio na hatia, wasio na nguvu.

Soma zaidi...

Tanzia ya Mwanachama wa Afisi ya Amiri, Ustadh Ahmad Bakr (Abu Osama)

Amiri wa Hizb ut Tahrir, Wanachama wa Afisi ya Amiri, Diwani ya Al-Madhalim (Malalamiko), na Afisi Kuu ya Habari na Hizb ut Tahrir kwa jumla wanaomboleza kwa Umma wa Kiislamu Mwanachama wa Afisi ya AmIrI, Ustadh Ahmad Bakr (Abu Osama) aliyefariki dunia asubuhi ya leo, 22 Rabi’ Al-Awwal 1447 H sawia na tarehe 14 Septemba 2025 M, akiwa na umri wa miaka themanini na saba.

Soma zaidi...

Mateso ya watu wa Palestina kwenye Daraja la Mfalme Hussein (Allenby) Kati ya Msongamano, Ufisadi, na Mfumo wa Hatari wa Tabaka la VIP

Kwa kuzingatia njama ya dola jirani  za eneo dhidi ya Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina ili kukaza mzingiro dhidi ya watu wake, kuwadhuru, na kuwasukuma kuiacha ardhi yao na kuikabidhi kwa Mayahudi, Daraja la Mfalme Hussein (Allenby au Karameh) linaunda njia kuu ya maisha ya watu wa Palestina kwa ulimwengu wa nje. Hata hivyo, kivuko hiki, ambacho kinapaswa kuwa njia ya usafiri, kimekuwa chanzo cha mateso ya kila siku kwa wasafiri, hasa upande wa Jordan, ambapo mambo ya kibinadamu, ya kiutawala, na ya kisiasa yanaingiliana na kuunda mandhari katili sana.

Soma zaidi...

Enyi Watu wa Jordan na Wanajeshi Wake: Jihadharini na Kundi la Kitengo cha Gilead, Vitisho vya Umbile la Kiyahudi kwa Nchi yenu, na Ushiriki na Utiifu wa Serikali!

Jana, 10 Septemba 2025, kamanda wa Kamandi Kuu ya jeshi la umbile la Kiyahudi alitangaza kuundwa kwa kitengo kipya cha kijeshi, kinachoitwa “Kitengo cha Gilead,” katika Bonde la Jordan, kitakacho kaa kwenye Bonde la Jordan. Kitengo hichi cha kikanda kina jukumu la kulinda mipaka ya mashariki ya Mayahudi katika Bonde la Jordan na Bahari ya Dead. Aliashiria kuwa kuanzishwa kwa kitengo hicho kunajiri ndani ya muundo wa kile alichoelezea kama “masomo ya kujifunza kutokana na kushindwa kugumu kwa Israel mnamo Oktoba 7, 2023.” Uundaji huu mpya unakuja baada ya vitisho vya viongozi wa umbile la Kiyahudi kupanuka hadi nchini Jordan na kwengineko chini ya mwavuli wa mradi wa “Israel Kubwa”, uliotangazwa na Netanyahu, uliobarikiwa na Trump, na kutangazwa wazi na Smotrich, Waziri wa Fedha wa umbile la Kiyahudi.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu