Jumatatu, 13 Dhu al-Hijjah 1446 | 2025/06/09
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Kwa Washiriki wa Kongamano lenye Kichwa: "Kashmir na Palestina inayokaliwa kwa mabavu - Suluhisho ni Nini?"

Imeharamishwa waziwazi kurudi kwa Umoja wa Mataifa (UN) kuhusiana na kadhia ya Kashmir, kwa sababu Umoja wa Mataifa ni Taghut, mamlaka yaliyojengwa juu ya msingi juu wa hukmu nyengine isiyokuwa ile aliyoiteremsha Mwenyezi Mungu (swt), kwa mujibu wa Sharia. Kuregelea kwa Umoja wa Mataifa ni kukaribisha Ghadhabu za Mwenyezi Mungu (swt).

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Uturuki: Amali Kubwa: “Ni Nani atamzuia Trump?!”

Kwa kuzingatia mauaji ya kikatili (mauaji ya halaiki) ambayo yanayofanywa na umbile nyakuzi la Kiyahudi dhidi ya Waislamu wasio na ulinzi katika Ukanda wa Gaza na Ukingo wa Magharibi katika Ardhi Iliyobarikiwa (Palestina), na kwa kuzingatia matakwa ya adui wa Mwenyezi Mungu, Trump, kuwahamisha Waislamu wasio na ulinzi kutoka Ukanda wa Gaza, Hizb ut Tahrir/Wilayah Uturuki inaandaa amali za halaiki kote nchini Uturuki chini ya kichwa: “Ni Nani atamzuia Trump?!”

Soma zaidi...

Umbile la Kigaidi la Kizayuni Limeufanya Ukingo wa Magharibi kuwa Makaburi ya Watoto kama vile Gaza, Huku Majeshi ya Nchi za Waislamu Yakitazama

Mnamo tarehe 7 Februari, shirika la ‘Save the Children’ liliripoti kwamba watoto wasiopungua 224 wameuawa katika Ukingo wa Magharibi na wanajeshi au walowezi wa Kizayuni tangu Januari 2023, mdogo zaidi akiwa na umri wa miaka 2 pekee. Kulingana na Umoja wa Mataifa, watoto 171 waliuawa katika Ukingo wa Magharibi tangu tarehe 7 Oktoba 2023 - sawia na karibu 1 kila siku. Hakuna mwanajeshi wa Kizayuni aliyefunguliwa mashtaka au kuwajibika kwa mauaji haya. Afisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Masuala ya Kibinadamu ilisema kuwa kumekuwa na ongezeko la mara 20 la idadi ya watoto wa Kipalestina waliouawa na mashambulizi ya anga ya umbile la Kiyahudi katika Ukingo wa Magharibi katika miaka ya hivi karibuni.

Soma zaidi...

Vitisho vya Kutojali vya Trump Vitasambaratishwa dhidi ya Mwamba wa Ustahamilivu wa Gaza

Mara tu Trump alipotwaa urais wa Marekani, alianza kutoa vitisho kushoto na kulia. La kukasirisha zaidi kati ya haya lilikuwa ni tangazo lake la nia yake ya kuwahamisha kwa nguvu watu wa Gaza. Alisisitiza tena uungaji mkono wake wa kufukuzwa kwa kudumu kwa Wapalestina kutoka Ukanda wa Gaza hadi nchi nyingine wakati wa mkutano wake na Waziri Mkuu wa umbile la Kiyahudi mnamo Jumanne, 4 Februari 2025. Hata alitangaza nia yake ya kununua ardhi ya Gaza na kuigeuza kuwa mradi wa uwekezaji!

Soma zaidi...

Trump asingeweza Kututawala kama Tungekuwa na Khalifa, na Umbile la Kiyahudi Lisingekuwepo bila Usaliti wa Watawala wetu

Viongozi wa ukafiri nchini Amerika na Ulaya, pamoja na chombo chao, umbile la Kiyahudi, wanajua kwamba misimamo ya watawala wa Waislamu, duara zao za kisiasa, na wapambe wao—wanaowatukuza—hawawakilishi wengi wa Waislamu, wala hawaakisi matumaini yaliyo ndani ya nyoyo zao kwa ajili ya kuregeshwa kwa mamlaka yao. Ukitaka kuelewa msimamo wao wa kweli na jibu lao kwa maamrisho ya Mwenyezi Mungu mbele ya chuki kwenu na kuwaua duniani kote, na kusubutu kwenu kutishia kukalia ardhi zao zaidi na kupora mali zao, musiangalie zaidi ya kiburi cha kiongozi wenu Trump. Kwa kutokuwa na haya mbele ya ulimwengu, ameonyesha kiburi cha Amerika kafiri na msaada wake kwa wale walioshukiwa na ghadhabu ya Mwenyezi Mungu.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu