Jumamosi, 04 Jumada al-awwal 1447 | 2025/10/25
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Marekani ya Kibeberu Inatumia Wakala Wake Shirika la Excelerate Energy kutia Udhibiti juu ya Bandari na Bahari zetu za Kimkakati ili Kuendeleza Udhibiti wake wa Kisiasa

Balozi wa zamani wa Marekani nchini Bangladesh Peter D Haas alifanya mkutano wa karibu saa moja na Waziri wa Mambo ya Nje Asad Alam Siam mnamo Alhamisi (4 Septemba). Ingawa hakuna upande uliofichua maelezo ya majadiliano hayo, vyanzo vya habari viliripoti kuwa mazungumzo hayo yalihusu uwezekano wa kuagiza LNG kutoka Marekani, pamoja na ushirikiano wa sasa na miradi ya mustakabali. Kwa sasa Haas anatumika kama Mshauri wa Kimkakati wa Excelerate Energy - shirika la kimataifa la Texas ambalo linaendesha kituo cha LNG kinachoelea huko Maheshkhali, Cox’s bazar.

Soma zaidi...

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan Wakutana na Mwenyekiti wa Mamlaka ya Wanazuoni katika Jimbo la White Nile

Jana, Jumatatu, tarehe 8/9/2025, huko Rabak, mji mkuu wa Jimbo la White Nile, ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir/Wilayah ya Sudan ulikutana na Sheikh Abdullah Al-Nur Tutu, Imam na Khatib wa Msikiti Mkuu wa Asalaya na Mwenyekiti wa Mamlaka ya Wanazuoni wa Sudan, Tawi la White Nile, nyumbani kwake katika kitongoji cha Asalaya. Ujumbe huo uliongozwa na wafuatao Dkt. Ahmad Mohammad, mwanachama wa Hizb ut Tahrir, akifuatana na Ustadh Faisal Madani, Abdul Majeed Osman Abu Hajar, na Al-Zein Abdul Rahman, wanachama wa Hizb ut Tahrir. Mkutano huo ulikuwa sehemu ya kampeni ya Hizb ut Tahrir ya kuzuia kujitenga kwa Darfur.

Soma zaidi...

Hali Baada ya Mvua na Mafuriko kwa Mara Nyingine Tena Imeweka Wazi Kuwa Waislamu Wanahitaji Mchungaji Khalifah

Tangu Juni 26, mafuriko katika maeneo mbalimbali ya Khyber Pakhtunkhwa, Punjab, na Karachi yamesababisha vifo vya zaidi ya watu 650 na kujeruhi zaidi ya elfu moja. Maelfu ya nyumba zimesombwa na maji, pamoja na akiba za maisha yote za watu, mali za nyumbani, na magari. Dada na mabinti zetu—ishara za staha na heshima—wamenyimwa nyumba na faragha zao, wakilazimishwa kuishi chini ya anga wazi.

Soma zaidi...

Ndani ya Muundo wa Kampeni ya Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Kuvuruga Mpango wa Kutenganisha Darfur Wanachama wa Hizb ut Tahrir katika Mji wa Al-Obeid Wahutubia Wito Mzito kwa Waislamu katika Msikiti Mkuu wa Al-Obeid na Kubeba Mabango katika Amali Ny

Katika amali mbili tofauti, Mashababu (wanachama) wa Hizb ut Tahrir katika mji wa Al-Obeid, mnamo Jumamosi tarehe 06/09/2025, na ndani ya muundo wa kampeni iliyoandaliwa na Hizb ut Tahrir/Wilayah Sudan ya kuvuruga mpango wa kuichana Sudan kwa kutenganisha Darfur, na kwa kuzingatia kwamba umoja wa Umma ni suala nyeti ambalo kwalo kipimo ni uha na kifo.

Soma zaidi...

Kuweka Matumaini juu ya Kuvunjika kwa Safu za “Israel” ni Usaliti Mpya wa Gaza

Kura moja ya maoni ilifichua kuwa 56% ya “Waisraeli” wanaogopa kusafiri nje ya nchi, 67% wanaamini kuwa serikali haiwawakilishi na 62% wanaunga mkono makubaliano ya kina ya kusitisha mapigano kati ya umbile la Kiyahudi na Hamas, ikiwemo kuachiliwa huru kwa mateka. Tovuti ya “Zman Yisrael,” ambayo ilichapisha maelezo ya kura hiyo ya maoni mnamo tarehe 5 Septemba 2025, ilifafanua kuwa wengi wa “Waisraeli” walionyesha kutokuwa na uwezo wao wa kusafiri nje ya nchi kutokana na kuongezeka kwa ukosoaji wa kimataifa wa umbile lao pamoja na kutengwa kunakoendelea kwa kimataifa kwa dola yao na kuendelea kwa vita mjini Gaza.

Soma zaidi...

Ndiyo, Uko Gaza na Gaza Inaangamizwa!

Huku uvamizi na mauaji ya halaiki mjini Gaza, yakiendelea kwa muda wa miezi 23, yamefikia kilele kwa matumizi ya silaha ya njaa inayoangamiza watu pamoja na majaribio ya mbinu mpya za mauaji zinazoitwa “mabomu ya roboti”; siasa za kinyonyaji na za kinafiki za watawala wa nchi za Kiislamu—wanaokabiliwa na ghadhabu za watu wao wenyewe kwa kuitelekeza Gaza—pia zimefikia kilele cha vilele.

Soma zaidi...

Marekani inatia Mikono yake Michafu katika Kila Mzozo; Sudan sio Tofauti

Katika kipindi cha muongo mmoja uliopita, Amerika imejidhihirisha kama mpangaji mkuu nyuma ya baadhi ya mizozo ya kunyama na ya ghasia zaidi kote duniani. Kutoka Urusi na Ukraine hadi India na Pakistan hadi China na Taiwan hadi Syria, Iraq, Afghanistan, Yemen, Kenya, Mali, Cameroon, na hii ni mifano michache tu! Hata hivyo, hakuna kilichoifichua Marekani zaidi ya uungaji mkono wake usio na haya na ushiriki wake katika mauaji ya halaiki yanayotokea Gaza dhidi ya watu wa Palestina. Kabla ya uvamizi, kuzingirwa kabisa, na kuangamizwa kwa Gaza, watu wengi hawakujua jinsi serikali ya Marekani ilivyokuwa chafu na jinsi wanavyoweza kuwatembeza wachezaji kama poni kwenye bao la chess.

Soma zaidi...

Jibu la Swali: Mkakati wa Amerika na Suluhisho la Dola Mbili

Tunajua kwamba mkakati wa Marekani wa kuasisi umbile la Kiyahudi katika moyo wa nchi za Kiislamu, kwa sehemu kubwa, umeegemezwa kwenye suluhisho la dola mbili. Hata hivyo, chini ya Trump, mkakati huu umeanza kuatelekezwa, au angalau kunyamaziwa, jambo ambalo limezua maswali. Kwa mfano, Trump alisema, "Unapotazama ramani, ramani ya Mashariki ya Kati, 'Israel' ni sehemu ndogo sana ikilinganishwa na ardhi hizi kubwa mno. Kwa hakika nilisema: 'Je, kuna njia yoyote ya kupata zaidi? Ni ndogo..." (Sky News, 19/8/2024). Je, hii inamaanisha kuwa mradi wa suluhisho la dola mbili wa Amerika umekufa na kukamilika, au bado ungali hai?

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu