Jumamosi, 30 Jumada al-thani 1447 | 2025/12/20
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Mpango wa Trump ni Sumu Hatari, Ukaliaji Kimabavu wa Marekani na Umoja wa Mataifa wa Gaza, na Uhalifu Mkubwa Uliofanywa na Watawala wa Waislamu

Kujisalimisha na kutoa silaha, kuregeshwa kwa mateka na mabaki ya wafu, na uvamizi unaoongozwa na Marekani, inayoongozwa na Trump kwa jina la Baraza la Amani, likisaidiwa na mwenye chuki dhidi ya Uislamu, Tony Blair, na kutekelezwa na tawala za eneo hili – hizi ndizo sifa za mpango mpya wa Trump, ambao aliutangaza. Amewashukuru viongozi wa nchi za Kiarabu na Kiislamu na washirika wake barani Ulaya kwa mwitikio wao wa dhati kwake, na kutangaza kuwa viongozi wa eneo hilo wanashiriki kikamilifu katika mpango huo wa amani.

Soma zaidi...

Musibabaishwe na Mikutano, Fungueni Mipaka

Katika Mkutano wa Kilele wa Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) na Ligi ya Nchi za Kiarabu uliofanyika jijini Doha, mji mkuu wa Qatar, Rais Erdoğan alisema: “Tunafahamu kuwa Israel haitasimama katika muda mfupi isipokuwa itakabiliwa na hisia kali na vikwazo. Tunafahamu kwamba tunazo mbinu za kuzuia hili.” (Agencies 15.09.2025)

Soma zaidi...

Kilio kwa Wabebaji Dawah “Mulikuwa wapi Muda wote huu?!”

Katika ghururi ya maisha na kutojali kwa jamii, neno moja pekee linabaki kuwa na uwezo wa kutikisa milima, kuchochea dhamiri, na kuamsha ari ya uwajibikaji katika nyoyo za Umma wa Uislamu. Ni neno lililotoka katika vinywa vya wale ambao miili yao ilichakaa kwa mateso na ambao fremu zao zilisagwa kwa dhulma ndani ya magereza ya madhalimu: “Mulikuwa wapi muda wote huu?!” Ilisemwa na mmoja wa wale walioachiliwa huru kutoka magereza ya mtoro Bashar al-Assad, wale walioonja majanga na ambao miaka yao ilizimwa gerezani; alipokutana na baadhi ya watu waliokuwa wameachiliwa huru, hakuuliza kuhusu idadi ya miaka gerezani, badala yake alipiga kelele usoni mwake: “Mulikuwa wapi, mulikuwa wapi muda wote huu? Kwa nini hamkutuachilia huru wakati tulipokuwa tunazikwa tukiwa hai?”

Soma zaidi...

Wilaya ya Al-Arish Mina, Warraq Mpya Kuwahamisha Wakaazi wake: Uwekezaji wa Lazima au Uhalifu wa Uhamishaji?

Siku hizi, mji wa Al-Arish unashuhudia sura mpya ya mateso wanayopata wananchi wa Misri mikononi mwa utawala unaowaona watu kuwa kikwazo tu kwa mipango yake ya uwekezaji na miradi yenye faida. Baada ya kimya cha miaka mingi na ahadi za uwongo kwamba wakaazi wa wilaya ya Mina kwamba hawatadhurika, watu walishangazwa kukuta matingatinga ya serikali yakiregea kubomoa nyumba na kung’oa wakao yao, bila kujali utakatifu wa nyumba, utu, au haki za watu, ambazo Mwenyezi Mungu (swt) amewapa katika ardhi na mali zao.

Soma zaidi...

Enyi Wanajeshi wa Misri (Kinana): Vivuko vya Gaza havihitaji Malori, Bali vinahitaji Majeshi na Magari ya Kivita

Hali ya kibinadamu mjini Gaza imefikia viwango vya maafa ambavyo havijawahi kushuhudiwa. Idadi ya vifo vya mashahidi imezidi 65,000. Ripoti za kimataifa zinaweka idadi hiyo kuwa 40% zaidi. Hao ni zaidi ya mashahidi 100,000 na takriban wakimbizi wa ndani milioni 1.9, ambao ni karibu asilimia 90 ya wakaazi wa Ukanda wa Gaza, ambao wanaishi katika mazingira yasiyo ya kibinadamu, na kunyimwa mahitaji ya kimsingi ya maisha. Gaza inakabiliwa na njaa ya kweli, haswa katika sehemu ya kaskazini ya Ukanda huo. Hospitali zinafanya kazi chini ya 30% ya uwezo wao, na uhaba wa dawa na mafuta unaweka makumi ya maelfu ya wagonjwa katika hatari ya kifo cha polepole. Takwimu hizi zinafichua ukubwa wa maafa hayo na kuthibitisha kuwa kinachoendelea ni vita vya mauaji ya halaiki dhidi ya Waislamu wa Gaza.

Soma zaidi...

Msimamo kwa Sherehe za Maadhimisho ya Mapinduzi Mawili ya Septemba Moja yaliingiza Usekula nchini Yemen na Mengine Yalitoa Wito wa Kuuimarisha!

Katika mwezi wa Septemba wa kila mwaka Yemen ina matukio mawili; la kwanza mnamo tarehe 26 Septemba 1962 ambayo ni kumbukumbu ya kupinduliwa kwa mfumo wa kifalme nchini Yemen Kaskazini, na la pili mnamo tarehe 21 Septemba 2014 ambayo ni kumbukumbu ya kuingia kwa Mahouthi jijini Sana’a ambayo ilisababisha udhibiti wao wa mikoa ya kaskazini.

Soma zaidi...

Tamasha la OIC Lahitimisha kwamba Qatar na Dola za Kiarabu Zisalie Waaminifu kwa Kuwa Kiatu Kilicho Chakaa cha Amerika Huku Zikibweka Vikali Mawinguni

Kufuatia shambulizi la kombora la umbile la Kizayuni dhidi ya wanachama wa Hamas nchini Qatar, taarifa ya mwisho ya mkutano wa dharura wa kilele wa Waarabu-Waislamu (OIC na Ligi ya Waarabu) uliofanyika jijini Doha mnamo 15 Septemba 2025, “unashutumu vikali uvamizi wa Israel dhidi ya Qatar, na kuutaja kuwa ni kama pigo kwa matarajio yoyote ya amani katika eneo hilo. Tangazo hilo zilizisihi nchi wanachama kuzingatia upya mafungamano yao ya kidiplomasia na kiuchumi na Israel na kufuata hatua za kisheria dhidi yake.”

Soma zaidi...

Trump, Msaidizi Mkuu wa Umbile la Kiyahudi katika Uhalifu wake wa Kinyama mjini Gaza na Palestina Yote, Anatoa Suluhisho la Maangamivu kwa Gaza, Hata Kulilazimisha, Juu ya Kundi la Watawala katika Nchi za Waislamu!!

Trump alisema katika chapisho kwenye jukwaa lake la Kijamii la Ukweli: “Ninafuraha kuripoti kwamba tuna mazungumzo yenye msukumo na yenye natija na Jumuiya ya Mashariki ya Kati kuhusu Gaza,” na kuongeza kuwa, “mazungumzo makali yamekuwa yakiendelea kwa siku nne, na yataendelea kwa muda mrefu iwezekanavyo ili kupata Makubaliano Yanayokamilishwa kwa Mafanikio.” (Truth Social; TRT Kiarabu, 27/9/2025)

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu