Jumanne, 14 Dhu al-Hijjah 1446 | 2025/06/10
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Baada ya Kutazama Tu Mauaji ya Kinyama kwa Siku 467, Watawala wa Pakistan Sasa Wanasherehekea Usitishaji Vita

“Watu wa Pakistan wanaungana nami katika kukaribisha tangazo la usitishaji mapigano uliosubiriwa kwa muda mrefu nchini Palestina,” Waziri Mkuu wa Pakistan, Shehbaz Sharif, aliandika kwenye ukurasa wa Twitter mnamo tarehe 16 Januari 2025. Hata hivyo, ukweli ni kwamba, kwa zaidi ya mwaka mmoja, utawala wa Munir-Sharif umekuwa ukitizama tu vifo na uharibifu huko Gaza, ambako mauaji ya halaiki ambayo hayajawahi kuonekana yalitokea, na walionusurika sasa kuganda kwa baridi hadi kufa. Walikuwa wakiyatazama haya yote, kana kwamba Pakistan haina jeshi kubwa zaidi katika Ulimwengu wa Kiislamu, na kana kwamba jeshi hilo nimeundwa kwa watu wasio na uwezo, dhaifu, waoga na vilema, kwa hivyo watawala hawawezi kufanya chochote kujibu ukatili huu isipokuwa kulaani, kushutumu na kupinga.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Ardhi Iliyobarikiwa: Kitengo cha Wanawake “Kalima kwa Mnasaba wa Kumbukumbu ya Miaka 104 ya Kuvunjwa Khilafah!”

Kwa mnasaba wa ujio wa kumbukumbu ya miaka 104 ya kuvunjwa kwa dola ya Kiislamu na makhaini wa Kiarabu na Kituruki iliyoasisiwa na Bwana wa Mitume Muhammad (saw) na maswahaba zake watukufu na waliobarikiwa, Mwenyezi Mungu awawie radhi, na kukomeshwa kwa mfumo wa utawala wa Kiislamu (Khilafah) mnamo tarehe 28 Rajab al-Muharram katika mwaka wa 1342 H sawia na 03/03/1924 M, Kitengo cha Wanawake cha Hizb ut Tahrir katika The Ardhi Iliyobarikiwa (Palestina) kinawasilisha mkusanyiko wa kalima hizo.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Kenya Iliandaa Msururu wa Amali katika Kumbukumbu ya Miaka 104 ya Kuvunjwa kwa Dola ya Khilafah

Kama sehemu ya kumbukumbu ya miaka 104 ya kuondolewa kwa Khilafah, Hizb ut Tahrir/Kenya ilifanya kampeni nchi nzima katika mwezi mtukufu wa Rajab 1446 H. Kampeni hii iliyoanza mwanzoni mwa mwezi mtukufu wa Rajab ilihusisha shughuli mbali mbali; Darsa, Semina na Visimamo. Hii ilikuwa ni kuukumbusha Ummah kuhusu hali yake ya kusikitisha ambayo umekuwa ukikabiliana nayo tangu kuondolewa kwa Khilafah mnamo tarehe 28 Rajab 1342 H sawia na tarehe 3 Machi 1924 M.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Lebanon: Kongamano la Khilafah: “Mabadiliko katika Ardhi ya Ash-Sham... Wasiwasi na Bishara Njema!”

Kwa mnasaba wa kumbukumbu ya miaka 104 Hijria ya kuvunjwa dola ya Kiislamu (Khilafah) mnamo tarehe 28 Rajab Tukufu mwaka 1342 H sawa na 03/03/1924 M mikononi mwa wahalifu wa Kiarabu na Kituruki, na kwa kuzingatia mabadiliko na mishtuko mikali inayotokea ndani na karibu na ardhi ya Ash-Sham, Hizb ut Tahrir/Wilayah Lebanon inaandaa kongamano lenye kichwa: “Mabadiliko katika Ardhi ya Ash-Sham... Wasiwasi na Bishara!”

Soma zaidi...

Mauaji Baada ya Mauaji Yanaendelea Gaza Huku Marekani Ikiendelea Kuwezesha Mauaji ya Halaiki na Dunia Imetulia Tuli

Mnamo tarehe 5 Januari, iliripotiwa kwamba umbile la mauaji la Kizayuni lililishambulia kwa mabomu Ukanda wa Gaza zaidi ya mara 100 katika muda wa siku 3 tu, na kuua zaidi ya watu 200 - wengi wanawake na watoto. Shabaha hizo zilijumuisha majengo ya makaazi, vikundi vya watu waliokusanyika barabarani na sokoni, na wale walio ndani ya makaazi yao. Pia iliripotiwa kuwa mtoto wa 8 aliganda hadi kufa katika Ukanda huo kutokana na baridi kali inayovumiliwa na wale wanaoishi katika mahema ya muda ambayo hayatoi ulinzi dhidi ya hali ya hewa ya baridi kali, na pia kutokana na kikwazo katili cha Wazayuni ambacho kinazuia mahitaji muhimu kama vile chakula, mafuta na nguo za majira ya baridi na blanketi kutokana na kuingia Gaza.

Soma zaidi...

Kuondolewa kwa Umbile la Kiyahudi ndio Suluhisho Pekee, Sio Suluhisho la Dola Mbili, Safadi

Waziri wa Mambo ya Nje wa Jordan Ayman Safadi, wakati wa kushiriki kwake katika Kongamano la Kiuchumi la Dunia huko Davos mnamo Jumatano, 22/01/2025, alisema kuwa mbinu yoyote ya baadaye ya Gaza lazima iegemee juu ya umoja wa Ukanda wa Gaza na Ukingo wa Magharibi na lengo la kufikia amani tu kwa msingi wa suluhisho la dola mbili. Alisema: “Katika muktadha wa suluhisho la kisiasa, serikali ya Palestina ndiyo pekee inayoshikilia uamuzi wa amani na vita, na hakupaswi kuwe na makundi ya kisilaha nje yake.”

Soma zaidi...

Pesa Zilizotumika Kutuua, Tunawezaje Kujitolea Kuzilipa?!

Katika mahojiano na gazeti la ‘Financial Times’, waziri wa mambo ya nje wa Syria alifichua ruwaza ya serikali mpya ya Syria baada ya Assad, akisisitiza kwamba nchi hiyo “haitaki kuishi kwa msaada,” na kwamba suluhisho liko katika kupunguza vikwazo vya Amerika na Ulaya. Aliongeza kuwa serikali haina mpango wa kusafirisha mapinduzi hayo ng’ambo au kuingilia masuala ya nchi nyingine. Hivyo, ikionyesha mabadiliko makubwa katika sera ya kigeni. Pia alionyesha katika mahojiano yayo hayo nia ya kubinafsisha bandari na viwanda vinavyomilikiwa na serikali na kuvutia uwekezaji wa kigeni, licha ya changamoto kubwa zinazoikabili Syria, ikiwemo madeni ya dolari bilioni 30 kwa washirika wa zamani wa Assad; Iran na Urusi.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu