Alhamisi, 14 Jumada al-thani 1447 | 2025/12/04
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Mwaliko wa Kuhudhuria Mkutano na Waandishi wa Habari

Sisi, katika Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan, tunafuraha kuwaalika ndugu wanahabari, wanasiasa, na wale wanaopenda masuala ya umma kuhudhuria mkutano na waandishi wa habari ambapo msemaji rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan atazungumza, wenye kichwa: Mkanganyiko wa Serikali Kuhusu Jinsi ya Kudhibiti Miamala ya Dhahabu.

Soma zaidi...

Ni lini Tutakomesha Uingiliaji wa Kafiri Magharibi na Mashirika yake ya Kikoloni katika Maisha Yetu, na Kuelekeza Nyuso Zetu Kwa Al-Waahid, Al-Haakim?

Chini ya ufadhili wa shirika la Ufaransa la Promediation, vyama vya kisiasa vya Sudan vilifanya warsha jijini Port Sudan, kama ilivyoripotiwa kwenye tovuti ya Sudan Tribune mnamo tarehe 5 Oktoba 2025: “Warsha inalenga kufafanua vigezo vya mazungumzo ya mustakbali yatakayoongozwa na Sudan, ikiwemo washiriki wake, eneo, na dori ya upatanishi wa kimataifa, kulingana na msemaji wa kambi hiyo Mohammed Zakaria. Viongozi wa muungano huo walisisitiza haja ya muungano wa ndani ulioshikamana. Minni Arko Minnawi, mkuu wa kamati ya kisiasa ya umoja huo, alisema hatua ya pamoja kati ya viongozi wa kiraia na kijeshi ni muhimu kwa ajili ya utulivu.

Soma zaidi...

Maradhi ya Mkurupuko Yawaangamiza Watu kwa Kukosekana kwa Dola ya Ustawi

Maradhi matatu ya kimazingira—kipindupindu, homa ya dengue, na malaria—yanawaangamiza watu katika majimbo ya Khartoum, Al-Jazirah, na Darfur, katikati ya uzembe wa kutisha na aibu ya kukosekana kwa serikali inayojiita “Serikali ya Matumaini”! Kuna matumaini aina gani wakati watu wanaishi katika mazingira yasiyostahili hata kwa wanyama—mazingira yanayotawaliwa na waenezaji magonjwa, ikiwemo mbu wa malaria, mbu wa dengue, na nzi?

Soma zaidi...

Mwaliko wa Kuhudhuria Kikao cha Kisiasa

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan inafuraha kuwaalika wanahabari, wanasiasa, na wale wote wanaopenda masuala ya umma, kuhudhuria na kushiriki katika kikao kipya cha Kisiasa, ambapo Ustadh Ya‘qub Ibrahim, mwanachama wa Hizb ut Tahrir/Wilayah Sudan, atakuwa mgeni, chini ya kichwa: Ulaya na Ushawishi Wake kwa Matukio nchini Sudan.

Soma zaidi...

Majibu ya Vyombo vya Habari kwa Yaliyomo kwenye Makala ya Mwandishi Sabah Muhammad Al-Hassan

Hizb ut Tahrir ni chama cha kisiasa ambacho mfumo wake ni Uislamu, kinataka kurudisha mfumo kamili wa maisha ya Kiislamu kwa kusimamisha Khilafah Rashida ya pili kwa njia ya Utume kwa njia ya kisiasa, na hakitekelezi vitendo vyovyote vya kisilaha si kwa kumwogopa mtu yeyote, bali ni kujifunga na njia ya Mtume (saw) katika kusimamisha dola ya kwanza ya Kiislamu.

Soma zaidi...

Hotuba ya Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilaya ya Sudan katika Mkutano na Waandishi wa Habari yenye kichwa: “Taarifa ya Quad na Ubwana Uliopotea”

Wanaofuatilia suala la Sudan na mapambano makali ya kimataifa juu ya ardhi yake wanajua vyema kwamba vita hivi vinaendeshwa na Marekani ili kung'oa ushawishi wa Kiingereza na kuichana Sudan kwa kutenganisha Darfur, na kwamba hatua zote za kisiasa zinazofanywa na Amerika au vyombo vyake nchini Sudan zinalenga kuondoa juhudi zozote ambazo zingewarudisha watu wa Uingereza kwenye mandhari.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Yafanya Kisimamo katika eneo la Nile Mashariki

Leo, Jumatano, tarehe 25 Rabi’ al-Awwal 1447 H sawia na 17 Septemba 2025 M, Mashababu wa Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan katika eneo la Nile Mashariki walifanya kisimamo baada ya Swala ya Adhuhuri katika Msikiti Mkuu wa Souq Sitta Al-Wahda. Ndani yake, mabango yaliinuliwa kuwataka Waislamu kusimama kidete kuzuia njama ya kuichana Sudan kwa kuitenganisha Darfur.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu