Jumamosi, 28 Shawwal 1446 | 2025/04/26
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

بسم الله الرحمن الرحيم

Hizb ut Tahrir / Uholanzi:

Matembezi Jijini Amsterdam “Harakati kwa ajili ya Gaza!”

Kwa kuzingatia mauaji ya kikatili (mauaji ya halaiki) ambayo yamekuwa yakiendelea kwa zaidi ya miezi 17, yanayofanywa na umbile halifu la Kiyahudi dhidi ya Waislamu wasio na ulinzi katika Ukanda wa Gaza uliozingirwa, ambayo yamesababisha kuuawa shahidi na kujeruhiwa kwa wanaume na wanawake wa Kiislamu zaidi ya 170,000 hadi sasa. Kufuatia umbile halifu la Kiyahudi kukiuka makubaliano dhaifu ya kusitisha mapigano alfajiri ya Jumanne, Machi 18, 2025, na kuanza tena mauaji ya kimpangilio ya Waislamu wasio na ulinzi, ambao wengi wao ni wanawake, watoto, na wazee, Hizb ut Tahrir / Uholanzi iliandaa matembezi na kisimamo cha halaiki katika mji mkuu wa Uholanzi, Amsterdam, kwa kichwa:

“Harakati kwa ajili ya Gaza!”

Nukta za matembezi na kisimamo zitakuwa:

Kuwajibisha wanazuoni, wenye ushawishi na taasisi kuchukua hatua za pamoja za kuyashinikiza majeshi katika nchi za Kiislamu na kuyataka yachukue hatua ili kuikomboa ardhi iliyobarikiwa (Palestina), ambayo ni wajibu wao wa kidini na wala haipaswi kupuuzwa.

Kuvunja mipaka ya kitaifa, kwani suala la ardhi iliyobarikiwa (Palestina) ni suala la Kiislamu, si la kitaifa, na kudhihirisha uhalisia wa mipaka bandia tuliyowekewa na mkoloni kafiri ili kutubakisha wanyonge.

Hakuna udhuru kwa watawala na viongozi katika nchi za Kiislamu. Hakuna utetezi kwao. Badala yake, lazima wawe na wajibu wa kukata uhusiano wao na Marekani na umbile la Kiyahudi, iwe uhusiano huo ni wa kisiasa, kiuchumi, au kijeshi.

Suluhisho liko kwetu sisi kama Umma mmoja la Kiislamu. Hatuwezi kutarajia haki na usawa kutoka kwa taasisi za kimataifa zilizounda umbile hili hapo awali. Hatupaswi kudanganywa na masuluhisho ya uwongo.

Umma lazima ufahamishwe nukta hizi, na kwamba hakuna suluhisho kwa masuala ya Umma isipokuwa suluhisho lililofaradhishwa na Uislamu.

Basi kuweni pamoja nasi...

Jumapili, 07 Shawwal 1446 H sawia na 06 Aprili 2025 M

- Ripoti Fupi juu ya Maendeleo ya Amali ya Matembezi -

Katika kuwanusuru watu wetu huko Gaza Hashim na kuongeza ufahamu miongoni mwa Waislamu kuhusu dori yao katika mauaji ya halaiki, mauaji na njaa yanayotokea Gaza, Hizb ut Tahrir nchini Uholanzi iliandaa matembezi yenye kichwa “Harakati kwa ajili ya Gaza” jijini Amsterdam mnamo Jumapili, 6 Aprili 2025.

Matembezi hayo yalianza kuzunguka katika barabara za jiji la Amsterdam, huku kelele za washiriki zikiregea wito wa kuinusuru Gaza, kuhamasisha majeshi ya Umma yaliyofungiwa katika kambi zao, na kuwaangusha watawala wa udhalilishaji na aibu, haswa nchini Misri na Jordan. Nyimbo pia ziliimbwa, zikifichua uongo na njama za Makafiri wa Magharibi na kuporomoka kwa taasisi zake za kimataifa baada ya uongo na ufisadi wao kufichuliwa.

Yalikuwa maandamano makubwa, yaliyojumuisha watu wengi wa jamii ya Kiislamu, wakiwemo wakaazi na wauzaji maduka. Mwishoni, kulikuwa na kisimamo ambacho kilianza kwa usomaji mzuri wa aya za Quran Tukufu. Kisha, Ustadh Okai Bala, Mwakilishi kwa Vyombo vya Habari wa Hizb ut Tahrir nchini Uholanzi, akatoa hotuba ambayo alizungumzia umuhimu wa kufanya sauti za Waislamu zisikike na kueleza msimamo wao juu ya yale ambayo watu wetu wa Gaza wanafanyiwa. Pia alizungumza kuhusu faida za kususia, michango, na dua ya mara kwa mara. Ustadh Okai Bala alihitimisha hotuba yake kwa kueleza mwamko ambao Umma wa Kiislamu ni lazima uwe nao ili kuweza kubadilisha unyonge na udhalilishaji ulioukumba, na jinsi unavyopaswa kujitoa mhanga na kukabiliana na watawala ili kuwaangusha na kuyalazimisha majeshi kuelekea katika ardhi iliyobarikiwa (Palestina) ili kuikomboa na kuukomboa Msikiti wa Aqsa uliobarikiwa, na kukomesha mauaji ya halaiki, mjini wa Gaza yanayofanywa na umbile halifu la Kiyahudi kwa zaidi ya miezi kumi na saba.

Mjumbe wa Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir Ulaya

Jumapili, 8 Shawwal 1446 H sawia na 6 Aprili 2025 M

- Sehemu ya Amali ya Matembezi -

#طوفان_الأقصى

#الجيوش_إلى_الأقصى

#الأقصى_يستصرخ_الجيوش

#ArmiesToAqsa

#AksaTufanı

#OrdularAksaya

#Aqsa_calls_armies

#AqsaCallsArmies

Kwa Maelezo zaidi, Tafadhali Zuru Mitandao ya Hizb ut Tahrir / Uholanzi:

Tovuti Rasmi ya Hizb ut Tahrir / Uholanzi

Facebook: Hizb ut Tahrir / Uholanzi

Twitter: Hizb ut Tahrir / Uholanzi

Instagram: Hizb ut Tahrir / Uholanzi

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

rudi juu

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu