Jumatatu, 03 Rajab 1447 | 2025/12/22
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Mwangwi wa Himaya: Uharamia wa Marekani Pwani ya Venezuela

Mnamo tarehe 10 Disemba 2025, Marekani ilimkamata nahodha wa meli ya mafuta kutoka pwani ya Venezuela, ikipanda meli hiyo na kuelekeza shehena yake ya takriban mapipa milioni 1.8 ya mafuta ghafi ya Venezuela hadi Marekani chini ya kibali cha vikwazo vya Marekani ambacho kilikuwa kinakaribia kuisha. Maafisa wa Marekani walidai hatua hii ya utekelezaji ililenga kuadhibu ukiukaji wa vikwazo vya muda mrefu vinavyohusiana na madai ya usafirishaji haramu wa mafuta. Serikali za Venezuela na Cuba zililaani hatua hiyo kama “wizi wa waziwazi” na “uharamia,” huku Cuba ikiuita “ugaidi wa baharini” ikiathiri mahitaji yake ya nishati. Usumbufu huo umeacha zaidi ya mapipa milioni 11 ya mafuta ya Venezuela yamekwama baharini, huku meli za mafuta na wafanyibiashara wakitathmini upya hatari za kubeba mafuta ghafi ya Venezuela, na kulazimisha punguzo kubwa na mazungumzo ya mikataba na wanunuzi muhimu kama vile China.

Soma zaidi...

Yaonekana Mazuri, lakini Ndani Hamna Kitu!

Rais Erdoğan, katika hotuba yake baada ya mkutano wa baraza la mawaziri, pia aligusia mwelekeo wa Uturuki wa sera ya kigeni, akisema: “Uturuki imeipa dunia funzo katika haki za binadamu kupitia juhudi zake zinazolenga amani na haki katika maeneo yaliyolowa damu na machozi—Gaza, Syria, Somalia, na Libya.” Alisisitiza kwamba taifa hilo limeunganishwa kwa fungamano lisilotikisika, pasi na tofauti kati ya Mturuki, Mkurdi, Muarabu, Alevi, au  Caucassian. (Mashirika, 15.12.2025)

Soma zaidi...

Ubepari kama Chanzo Kikuu cha Maafa ya Mafuriko huko Sumatra

Kimbunga Senyar kilikuwa kichocheo tu; kiwango cha uharibifu nchini Indonesia kinaonyesha miongo kadhaa ya usimamizi mbaya wa ikolojia. Sumatra imepoteza mamilioni ya hekta za misitu, ikidhoofisha maeneo ya maji huko Aceh, Sumatra Kaskazini, na Sumatra Magharibi. Maeneo ya tambarare yalikaushwa maji kwa ajili ya mashamba makubwa, na kusababisha kupungua kwa ardhi na kugeuza vizuizi vya maji asilia kuwa mabonde ya mafuriko. Makaazi ya haraka katika maeneo tambarare ya mafuriko, pamoja na usimamizi dhaifu wa matumizi ya ardhi, yaliongeza athari. Mvua kali ilipofika, mandhari haikuwa na uwezo uliobaki wa kuhimili. Maafa yanaonyesha kwamba muundo wa maendeleo wa Indonesia—unaoendeshwa na uchimbaji na usimamizi duni wa mazingira—umefanya hali mbaya ya hewa kuwa hatari zaidi kuliko inavyopaswa kuwa. (news.mongabay)

Soma zaidi...

Shambulizi la Muafghani jijini Washington na Maeneo Yaliyofichwa ya Siasa

Shambulizi la silaha jijini Washington, D.C. wiki moja iliyopita—ambapo Rahmanullah Lakanwal, raia wa Afghanistan, anatuhumiwa kuwafyatulia risasi Walinzi wawili wa Kitaifa wa Marekani—lilitokea karibu na kituo cha Metro cha Farragut Magharibi, mita mia chache tu kutoka Ikulu ya White House, eneo ambalo kwa kawaida linalindwa na baadhi ya tabaka kali zaidi za usalama. Kutokana na ufyatuaji risasi huo, Sarah Bäckström, mlinzi wa Kitaifa wa miaka 20, aliuawa na Andrew Wolf alijeruhiwa vibaya.

Soma zaidi...

Utawala wa Sharaa nchini Syria Haujui Mipaka Katika Kujisalimisha Kwake kwa Marekani

Rais wa Marekani Donald Trump alituma barua iliyoandikwa kwa mkono kwa kiongozi wa Syria Ahmed Sharaa, akisisitiza uungaji mkono wake na kuahidi msaada wa Marekani. Barua hiyo iliwasilishwa Damascus kupitia Tom Barrack, mmoja wa washirika wa karibu wa Trump na mfanyibiashara wa kimataifa. Picha ya wakati Trump alipokutana na Sharaa katika Afisi ya Oval iliambatanishwa na barua hiyo. Trump aliandika barua ifuatayo kwenye picha hiyo kwa mwandiko wake mwenyewe: “Ahmed, utakuwa kiongozi mzuri, na Amerika itasaidia!” (Mashirika, 3 Disemba 2025)

Soma zaidi...

Muungano na Amerika hauruhusiwi kwa Pakistan, wala Muungano na India hauruhusiwi kwa Afghanistan

Waziri wa Ulinzi wa Pakistan Khawaja Asif mnamo Jumatatu (20 Oktoba 2025) alitupilia mbali madai ya Afghanistan kwamba Islamabad inatenda kwa niaba ya Marekani ili kuunda mabadiliko ya serikali jijini Kabul, akielezea madai hayo kama “upuuzi mtupu”. Islamabad imesema kwa muda mrefu kwamba India, hasimu wake wa muda mrefu, inafanya kazi pamoja na Afghanistan kusaidia Tehreek-e-Taliban Pakistan (TTP), ambayo inajulikana kama Taliban ya Pakistan, na wanamgambo wengine dhidi ya Pakistan. New Delhi inakanusha madai hayo.

Soma zaidi...

Mafunzo Kutokana Na Jinsi Nchi Kubwa Zaidi ya Kidemokrasia Duniani Inavyowafelisha Wanawake wa Kiislamu

Gazeti la ‘The Indian Express’ limechapisha makala yenye kichwa “Pindi kutokuwepo kukizungumza kwa sauti ya juu zaidi kuliko uwepo: Wanawake wa Kiislamu na Bunge la India”. Yanazungumzia ukosefu mkubwa wa uwakilishi wa wanawake wa Kiislamu katika afisi yake. Tangu Lok Sabha ya kwanza (Bunge la Kidemokrasia la India) mnamo 1952, ni wanawake kumi na nane pekee Waislamu ambao wamekuwa wachangamfu ndani bunge. Uwakilishi mdogo umerekodiwa katika kitabu kipya kilichoandikwa na waandishi wa habari Rasheed Kidwai na mwanasayansi wa siasa Ambar Kumar Ghosh chenye kichwa “Kukosekana Bungeni: Wanawake wa Kiislamu katika Lok Sabha”, kilichochapishwa na Juggernaut (2025). Waandishi hawajali katika utambuzi wao wa jinsi uwakilishi kama huo ulivyokuwa mara nyingi. Kwa vyama vingi vya kisiasa, ugombezi wa mwanamke wa Kiislamu ulifanya kazi kama ishara tu badala ya athari na ushawishi halisi.

Soma zaidi...

Kuwakataa Wanariadha wa ‘Israel’: Kipimo Halisi cha Msimamo Madhubuti wa Indonesia?

Indonesia: Mahakama ya Usuluhishi wa Michezo (CAS) ilikataa rufaa ya Shirikisho la Michezo ya Viungo (Gymnastics) la ‘Israel’ (IGF) kuruhusu wanariadha wake kushiriki Mashindano ya Dunia ya Sanaa za Gymnastiki jijini Jakarta, Indonesia, kuanzia Oktoba 19–25, 2025. Serikali ya Indonesia iliwanyima viza wachezaji sita wa mazoezi ya viungo wa ‘Israel’, ikionyesha uungaji mkono kwa Wapalestina na shinikizo la ndani. IGF ilkata rufaa kwa CAS na Shirikisho la Kimataifa la Gymnastiki (FIG), ikiomba hatua za kuhakikisha ushiriki au kubatilisha michezo hiyo. CAS ilitupilia mbali rufaa zote mbili, na FIG ilisema haina mamlaka juu ya maamuzi ya visa. Indonesia ilithibitisha tena msimamo wake, ikiegemea katika sera yake ya kigeni na hisia za umma.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu