Jumamosi, 03 Ramadan 1444 | 2023/03/25
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Vichwa vya Habari 2/11/2022

Marekani inajiandaa kutuma ndege sita zenye uwezo wa nyuklia aina ya B-52 bombers kwenye kambi moja ya anga kaskazini mwa Australia, kulingana na Shirika la Utangazaji la Australia (ABC). Ikinukuu nyaraka za Marekani, ABC iliripoti kwamba Washington ilikuwa imeandaa mipango ya kina ya kuunda huduma maalum kwa ajili ya ndege hiyo katika Kambi ya Anga ya Tindal, takriban maili 185 kusini mwa jiji la Darwin katika Wilaya ya Kaskazini ya Australia.

Soma zaidi...

Vichwa vya Habari 28/10/2022

Kwa maana hiyo, kupanda kwa Sunak ni mafanikio makubwa yasiyopingika, iwe unakubaliana na siasa zake au la. Bila kuwa na uwezo wa kudai aina yoyote ya historia ya kuwa mhamiaji mzuri zaidi, Sunak bado amekaidi uwezekano kama mtu wa Asia kufika nafasi ya juu zaidi nchini. Safari yake ni ukumbusho wa jinsi Waingereza weusi na kahawia wanapaswa kupigana dhidi ya mkondo ili kuchukuliwa kwa uzito.

Soma zaidi...

Uhakiki wa Habari 15/10/2022

Kushindwa vibaya kwa Urusi katika vita vya Ukraine chini ya uongozi wa Rais Vladimir Putin kunafichua kwa haraka udhaifu wa kweli wa dola ya Urusi. Wakati fulani karibu kuchukuliwa kuwa dola kuu yenye nguvu sawa na Marekani, sasa haijulikani ikiwa Urusi itaweza hata kuendelea kuhesabiwa miongoni mwa dola kubwa duniani.

Soma zaidi...

Vichwa vya Habari: 12/10/2022

Rais wa Urusi Vladimir Putin ametangaza kwamba vikosi vya Urusi vilikuwa vimefanya mashambulizi makubwa ya silaha za masafa marefu, zenye usahihi wa hali ya juu zikilenga vituo vya kawi, maamuzi na mawasiliano vya Ukraine, mnamo Oktoba 10, baada ya kukumbwa na vizingiti vingi katika vita hivyo vya miezi minane.

Soma zaidi...

Vichwa vya Habari: 05/10/2022

Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Antony Blinken alisema katika mkutano na waandishi wa habari pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje wa Canada kwamba mashambulizi dhidi ya mabomba ya gesi asilia ya Nord Stream yanayounganisha Urusi na Ujerumani yanatoa "fursa kubwa" ya kukomesha utegemezi wa Ulaya kwa nishati ya Urusi.

Soma zaidi...

Uhakiki wa Habari 01/10/2022

Rais wa Urusi Vladimir Putin alitia saini amri Ijumaa ya kuyaunganisha majimbo manne ya Ukraine. Katika sherehe kubwa jijini Kremlin, alisema Urusi itajumuisha rasmi majimbo ya Ukraine ya Donetsk, Luhansk, Kherson na Zaporizhzhia - na kwamba watu wanaoishi huko "watakuwa raia wetu milele."

Soma zaidi...

Vichwa vya Habari 28/09/2022

Vyombo vya habari vya Uturuki vimeripoti kuwa Rais Recep Tayyip Erdogan aliwaambia wanachama wa chama chake kwamba alisikitishwa na kukosa nafasi ya kukutana na Rais wa Syria Bashar al-Assad katika Mkutano wa hivi karibuni wa Shirika la Ushirikiano la Shanghai mapema mwezi Septemba. Kauli ya Erdogan ilifuatia ripoti kwamba mkuu wa ujasusi wa Uturuki amekuwa akikutana na mwenzake wa Syria hivi majuzi katikati mwa Septemba.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu