Jumatatu, 28 Safar 1446 | 2024/09/02
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Kitengo cha Wanawake Katika Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir Kimezindua Kurasa Mpya za Facebook: “Familia: Changamoto na Suluhisho la Kiislamu”

Kufuatia mafanikio ya kampeni yetu ya kiulimwengu na kongamano la wanawake la kimataifa mnamo Oktoba 2018, “Familia: Changamoto na Suluhisho la Kiislamu”, Kitengo cha Wanawake katika Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir kina furaha kutangaza uzinduzi wa kurasa zetu mpya za Facebook zinazojitolea kuangazia kadhia zinazo husiana na mgogoro wa kiulimwengu unao athiri “Kiungo cha Familia”. Kurasa hizi mpya, ambazo zitakuwa kwa Kiarabu, Kiingereza, Kituruki na Kiindonesia, zitawasilisha tena shehena ya fasihi zilizo chapishwa katika kampeni na kongamano pamoja na kutafuta mada za ziada kuhusiana na uhalisia, sababu na masuluhisho ya ukosefu wa utulivu na mfarakano unao athiri muundo wa familia katika jamii kote ulimwenguni.

Soma zaidi...

Wanawake wa Palestina Wangali Wanamsubiri Al-Mu’tassim ili Kuitikia Kilio Chao!!

Vyombo vya habari vilichapisha picha na video za majeshi vamizi ya umbile la Kiyahudi yakifurusha katika nyumba moja ya familia ya Jerusalem eneo la Aqaba Al-Khalidiya katika mji wa kale wa Jerusalem kwa kutumia nguvu za kijeshi. Vyombo hivyo vya habari vilionyesha nduru na malalamishi ya wanawake waliolalamikia shambulizi la polisi wa Kiyahudi katika nyumba hiyo, wakimpiga na kumkamata mwenye nyumba hiyo, na kuwaacha wao bila ya ulinzi na makao baada ya nyumba yao kuchukuliwa.

Soma zaidi...

Pamoja na Kampeni ya Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir Dhidi ya Ukatili wa Uchina kwa Waislamu Eneo la Mashariki Turkestan

Uchina kama taifa la kirasilimali haijihusishi tu kuzitumia kilafi rasilimali za kiasili za mataifa yanayo endelea hususan bara la Afrika na kulazimisha juu yao mzigo wa mikopo usio himilika, pia inatekeleza kampeni ya ghasia, vurugu na ukatili dhidi ya Uislamu na Waislamu wa Turkestan Mashariki, eneo ambalo lilivamiwa kinguvu na kutekwa na Uchina.

Soma zaidi...

Mwaelekea Wapi, Enyi Munao Simamia Muongozo wa Utoaji Fatwa wa Kiulimwengu?!!

Baadhi ya wanaume wa Al-Azhar wanaendelea kutembea juu ya barabara ya kuushambulia Uislamu na Hukmu zake pasi na maono wala hofu kwa Mwenyezi Mungu (swt). Wanaendelea kuifanya Al-Azhar Al-Sharif – ambayo ilikuwa ndio ngome dhidi ya njama za maadui wa Uislamu – jukwaa ambalo wanavishambulia vipengee vya Uislamu na Hukmu zake zinazo husiana na wanawake. Meza ya Utoaji Fatwa wa Kiulimwengu ya Jumba la Fatwa la Misri (Dar al-Ifta) zilisema kuwa, “fatwa juu ya kadhia ya ndoa kwa watoto wadogo zimeifunga ndoa kwa watoto wadogo katika mahusiano ya kijinsia pekee, na kwamba Hizb ut Tahrir imeifunga ndoa katika mahusiano ya kijinsia pekee, ikiondoa upande wa kisaikolojia, kiafya, kiakili na mambo ya kimwili, na kuweka mbali kiwango cha uvumilivu na jukumu ambalo mkataba wa ndoa unalazimisha juu ya pande zote mbili …” Hili, kwa kuanzia, linagongana na yale ambayo Quran Tukufu imeeleza kuhusu fahamu ya ndoa kama utulivu na huruma.

Soma zaidi...

Jinsi Siasa Inavyo Fanana na Zamani … Matukio Yanaendelea Kama Wanavyo Endelea Watazamaji!

Wanajeshi madhalimu wa umbile la Kiyahudi walimuua msichana kutoka Palestina kwa kummiminia risasi katika kituo cha upekuzi cha al-Za’im, mashariki mwa ardhi iliyo kaliwa Al-Quds (Jerusalem). Shahidi huyo ni mwanafunzi wa shule ya upili aliyekuwa amebeba mkoba wake wa shule wakati wa kuuwawa kwake; aliuwawa kutokana na madai ya kujaribu kutekeleza oparesheni ya kudunga kisu. Majeshi hayo vamizi yalizuia wahudumu wa ambulensi kutomfikia ili kumpa tiba. Aliachwa kuvuja damu hadi kufa.   

Soma zaidi...

Maradhi ya Utaifa Yamepelekea Kukamatwa kwa Wanawake na Watoto Wanaonyanyaswa wa Rohingya na Serikali ya Saudia

Mamia ya Waislamu wa Rohingya wanawake na watoto, waliokimbia mauwaji na ubakaji wa halaiki kutoka kwa Mabudha wenye misimamo mikali nchini Myanmar, wanaendelea kuzuiliwa pasipo kujulikana hatima yao katika Kituo cha Kizuizi cha Shumaisi nchini Saudi Arabia, baada ya kutafuta hifadhi katika dola hiyo.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu