Jumapili, 27 Safar 1446 | 2024/09/01
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Je, Watoto wa Kambi ya Wakimbizi ya Al-Rukban Wataachwa Wafe kwa Baridi na Njaa, Huku Wakikosa Mtu Yeyote wa Kuwaokoa?!

Watoto kumi na tano wasio na makao, wengi wao wakiwa wachanga, wamekufa nchini Syria kutokana na baridi kali na ukosefu wa matibabu, kwa mujibu wa ripoti ya UNICEF mnamo Jumanne 15/1/2019. Watoto, 13 kati yao walio chini ya umri wa mwaka mmoja, walifariki katika kambi ya Al-Rukban kusini mashariki mwa Syria, karibu na mpaka wa Jordan. Al-Rukban na kambi nyenginezo zinakumbwa na uhaba mkubwa sana wa misaada ya kibinadamu, pindi wakimbizi wanapowasili baada ya safari nzito baada ya kukimbia ngome ya mwisho ya ISIS mashariki mwa nchi hiyo. Geert Cappelaere, mkurugenzi wa UNICEF wa eneo la Mashariki ya Kati na Afrika Kaskazini, alisema “Baridi kali zaidi na hali mbaya za maisha katika Al-Rukban zimesababisha maisha ya watoto kuongezeka kuwa hatarini,” aliongeza, “Kwa mwezi mmoja tu, kwa uchache watoto wanane wamekufa – wengi wao wakiwa chini ya umri wa miezi minne, na mdogo wao zaidi akiwa umri wa saa moja.”   

Soma zaidi...

Majanga Halisi Maovu Hata Bila ya Kuwepo Dhoruba za Barafu

Wakimbizi katika kambi za kinyama kadha wa kadha wameyaomba usaidizi mashirika ya misaada na wametoa wito kwa msaada wa dharura kutoka kwa mamlaka husika. Wamesema kuwa ni kiwango kidogo pekee cha msaada ndio kimewafikia wakaazi katika kambi, ambacho hakitoshi kwa asilimia 10 ya idadi jumla ya wakimbizi katika kambi, katika wakati ambapo kuna uhaba mkubwa wa mafuta na njia za kujikanza moto katika hali mbaya za anga kama hizo ambazo zimelikumba eneo zima la Ash-Sham.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Tunisia Inatangaza Uzinduzi wa Kampeni: Na nani aliye mbora zaidi katika kuhukumu kuliko Mwenyezi Mungu

Tunisia hivi sasa imo katika kipindi kigumu baada ya wale tuliowafikiria kuwa ni watawala kuyatelekeza majukumu yao msingi na kuziwachia dola za msalaba za kikoloni na wafanyikazi wake ndani ya Umoja wa Ulaya na Shirika la Fedha la Kimataifa kuamua sera za kiuchumi, kifedha na kijamii mpaka nchi ikadhibiti usambaratikaji wa kiuchumi licha ya kwamba kulikuwa na madeni makubwa.

Soma zaidi...

Kuwapokonya Ummah Utawala wao, Kuwakandamiza na Kushambulia Matukufu yao ni Moja katika Uhalifu Mkubwa dhidi ya Uislamu na Waislamu

Tawala za ukandamizaji na udhalimu hususan utawala wa kihalifu na ukandamizaji wa Ash-Sham, umekuwa ukiwapokonya Ummah maamuzi yao, ukiyakosea heshima matukufu yao, na kuwafuatilia kinyama kupitia taasisi za ujasusi ili kuwatia hofu kiasi kwamba watu wameshindwa mpaka kuzungumza na ndugu zao kuhusu masuala ya ummah.

Soma zaidi...

Enyi Waislamu…Waokoeni Watoto wa Yemen!

Mnamo 21/11/2018, ripoti ya Shirika la Uingereza la Okoa Watoto ilisema kuwa takribani watoto 85,000 chini ya umri wa miaka mitano wamekufa kutokana na ukosefu wa lishe bora ndani ya kipindi cha miaka mitatu ya vita ndani ya Yemen.  Idadi hii pekee ni sawa na jumla ya idadi ya watoto walioko chini ya miaka mitano ndani ya Birmingham, jiji la pili kubwa ndani ya Uingereza.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Tunisia Ilikuwa Mwenyeji wa Kongamano la Kimataifa la Wanawake “Familia: Changamoto na Suluhisho la Kiislamu”

Mnamo Jumamosi 27 Oktoba, kwa Baraka za Allah, Alhamdulillah, Kitengo cha Wanawake katika Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir kwa ushirikiano na Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Tunisia kwa ufanisi kilifanya kongamano kubwa na la kuvutia la kimataifa la wanawake jijini Tunis lenye kauli mbiu, “Familia: Changamoto na Suluhisho la Kiislamu” ili kuelezea sababu na suluhisho la Kiislamu juu ya mgogoro unaoathiri utulivu na umoja wa ndoa na maisha ya familia katika jamii kote ulimwenguni, ikiwemo biladi za Waislamu. Tukio hili muhimu lilihudhuriwa na zaidi ya wanawake 250 kutoka kote nchini Tunisia wakiwemo mawakili, walimu, walezi wa watoto, wahandisi, wanafunzi wa vyuo vikuu, viongozi wa jamii, na watetezi wa vijana. Hotuba zilitolewa na wanachama wa kike wa Hizb ut Tahrir kutoka Tunisia, Uturuki, Ardhi Iliyo Barikiwa – Palestina, Pakistan, Lebanon, Indonesia, Ghuba la Kiarabu. Uholanzi, na Uingereza. Kongamano hilo vile vile lilipeperushwa moja kwa moja mtandaoni kwa washiriki wa kimataifa na kutazamwa na maelfu ya watazamaji kutoka katika pembe tofauti tofauti duniani. 

Soma zaidi...

Yemen yakabiliwa na baa la njaa la kutisha lililowahi kutokea ndani ya miaka 100 ya ulimwengu likisababishwa na mzozo kati ya Uingereza na Marekani ambao umeutia nchi hiyo katika vita wasivyostahiki wakiongozwa na vibaraka wa kitaifa na kieneo!

Kwa mujibu wa duru za Umoja wa Mataifa, Yemen kwa sasa inakabiliwa na baa la njaa baya zaidi ulimwenguni kwa miaka 100. Uzani wa janga hilo umefananishwa na ule uliokumba Afrika katika miaka ya themanini. Ripoti ya hivi majuzi ya shirika la habari la BBC imenukuu kuwa kwa mujibu wa Lisa Grande, Msimamizi wa Misaada ya Kibinadamu wa UN nchini Yemen, zaidi ya raia milioni 13 wako katika hatari ya kufa kutokana na ukosefu wa chakula katika miezi mitatu ijayo

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu