Gazeti la Al-Raya: Vichwa Vikuu vya Toleo 428
- Imepeperushwa katika Al-Rayah
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Enyi maafisa wa Kiislamu wa majeshi ya Waislamu! Tunajua nyoyo zenu zinauma, mnapoiona nchi yenu ikiwa katika hali ya kukata tamaa kiuchumi, chini ya minyororo ya wakoloni wa IMF, huku raia wengi wakishuka chini ya mstari wa umaskini, wakishindwa kukidhi mahitaji ya chakula kwa familia zao.
Ardhi zote za Waislamu ziko chini ya ufaradhi wa kutawaliwa kwa Uislamu, kupitia Khilafah. Kama vile Swalah, hatuna mfano mwengine wa kuuiga, isipokuwa ule wa Mtume ﷺ. Khulafaa Rashidun (ra) walitawala kwa Uislamu kwa mujibu wa njia yake ﷺ, na sisi pia ni lazima.
Watu wa Yemen husherehekea Ijumaa ya kwanza ya mwezi wa Rajab kila mwaka, tukio muhimu kwao, ambalo ni kuingia kwa watangulizi wao katika Uislamu. Ndani yake wanatoa sifa na shukrani zao kwa Mwenyezi Mungu kwa neema ya Uislamu.
Katika wakati ambapo mashirika rasmi na vyombo vya habari vya serikali vinakusanya maoni ya umma dhidi ya serikali ya Netanyahu yenye msimamo mkali - na serikali zote za kigaidi na itikadi kali - tangu kushinda uchaguzi, na uhamasishaji huu wa vyombo vya habari unaanza na kulaani uvamizi wa Ben Gvir wa Msikiti wa Al-Aqsa.
Wazo la utekelezaji wa hatua kwa hatua wa hukmu za Mwenyezi Mungu duniani ni mojawapo ya mawazo hatari sana ambayo ni ngeni kwa Uislamu.
Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Ardhi Iliyobarikiwa - Palestina inamuomboleza mmoja wa wanaume wa Hizb ut Tahrir, mbebaji da’wah kutoka kizazi cha kwanza katika safu zake, aliyesamehewa, kwa idhini ya Mwenyezi Mungu
Baada ya tukio la hivi majuzi la kuchomwa moto Qur'an, kwanza mbele ya ubalozi wa Uturuki jijini Stockholm mnamo Januari 21, na hivi karibuni zaidi kwenye swala ya Ijumaa mnamo Januari 27, mbele ya msikiti mmoja jijini Copenhagen, wanasiasa ghafla wako mbioni kuosha mikono yao.
Ongezeko la vijana wanaojihusisha na makundi ya Nazi mamboleo na itikadi kali za mrengo wa kulia “ni la kutisha sana”, afisa mmoja wa upelelezi wa kukabiliana na ugaidi amesema. Naibu Msimamizi Gareth Rees alisema polisi hawawezi tena "kuendelea kuwakamata watu hili haliwezi kutatua” suala hilo.
Hizb ut Tahrir / Wilayah Pakistan imeandaa kampeni kwa kichwa “Rudisheni Khilafah” katika mitandao ya kijamii kwa mwezi mzima wa Rajab 1444 Hijri, kwa mnasaba wa kumbukumbu ya miaka 102 ya kuanguka dola ya Kiislamu – Khilafah – kwa wakoloni makafiri.