Jumamosi, 18 Jumada al-awwal 1447 | 2025/11/08
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Khilafah pekee ndio inayojali Maslahi ya Watu na ndio Mlinzi wa Haki na Mahitaji yao

Hali mbaya ambayo Sudan imefikia kufuatia vita vya kikatili vilivyoanza miaka miwili iliyopita kati ya vikosi vya jeshi na Vikosi vya Msaada wa Haraka sio siri. La kusikitisha, watu wasio na hatia wa Sudan wamelipia, na wanaendelea kulipia, gharama ya mzozo huu mbaya wa kimataifa unaoendeshwa na silaha za ndani kwa lengo la kuichana nchi na kulinda maslahi ya Amerika, Ulaya, na wengineo!!

Soma zaidi...

Hakuna Wokovu kwa Watu wetu nchini Sudan Wala Amani au Usalama isipokuwa chini ya Mfumo wa Uislamu

Katika yote historia, wingi wa makabila nchini Sudan kamwe haukuwa sababu ya mizozo na vita. Bali, kilichosababisha haya ni mapambano makali ya kisiasa na kijeshi baina ya dola za kikoloni na vibaraka wao, ambayo yaliharibu mazao na vizazi, hasa baada ya wao kuigawanya nchi na kupanda mbegu za fitina na mapigano ya kikabila na kimapendeleo, sawa kabisa na yale yanayotokea leo na kwa usahihi kabisa kama ilivyotokea katika siku za mwanzo za Ujahiliya.

Soma zaidi...

Sudan: Giza la Muundo wa Makubaliano au Nuru ya Katiba Inayotokana na Kitabu cha Mwenyezi Mungu na Sunnah ya Mtume Wake?

Haishangazi kwa mtu yeyote anayefuatilia hali ya kisiasa nchini Sudan kujua kwamba vita hivi viliratibiwa na kusimamiwa na Marekani chafu na yenye nia mbaya ili kufanikisha ajenda yake na kuvunja nguvu za washindani wake wa Ulaya, hasa raia wanaoshirikiana na Uingereza. Vita hivi vinafadhiliwa na Amerika, ni mchezo wao uliolaaniwa. Ushahidi wa wazi zaidi ni kwamba taarifa kuhusu kurefusha vita ilitoka kwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Blinken. Kurefushwa kwa vita hivi si kwa ajili ya utatuzi au kuhifadhi damu au kukomesha uharibifu ambao umeharibu nchi na watu wake; badala yake, ni mapambano ya nyuma na mbele na jaribio la kuweka maono ya kisiasa ambayo yanahakikisha na kuhifadhi maslahi ya Marekani nchini.

Soma zaidi...

“Kujitawala Wenyewe” kwa Mujibu wa Matakwa ya Wakoloni!

Ardhi zetu za Kiislamu zimekuwa jukwaa la kupigania mali na ushawishi kati ya Marekani na Ulaya. Cha kusikitisha ni kwamba, zana za mapambano haya ni baadhi ya wana wa Ummah, iwe katika serikali au vuguvugu la waasi, kama inavyotokea leo nchini Sudan, wakati wanaoshindwa pekee katika vita hivi ni watu wasio na hatia, wasio na nguvu.

Soma zaidi...

Hakuna Suluhisho kwa Suala la Sudan Isipokuwa Kutawalisha Uislamu

Tangu uhuru wake mnamo tarehe 1/1/1956, Sudan imeshuhudia mfululizo wa mapinduzi ya kijeshi. Ya kwanza ilikuwa jaribio lililofeli lililoongozwa na Ismail Kabida, ambaye alijaribu kupindua serikali ya kwanza ya kitaifa iliyoongozwa na Ismail al-Azhari. Hii ilifuatiwa na mapinduzi ya kwanza yaliyofaulu yaliyoongozwa na Luteni Jenerali Ibrahim Abboud mnamo Novemba 1958 dhidi ya serikali iliyochaguliwa ya al-Azhari.

Soma zaidi...

Fahali Wanapopigana, Zinazoumia ni Nyasi “Sudan ni Mfano”

Sijapata katika historia msemo wenye ufasaha zaidi wa uovu wa ukoloni kuliko maneno ya Rabi ibn Amir, Mwenyezi Mungu amuwiye radhi, kwa kamanda wa Kifursi: “Sisi ni watu ambao Mwenyezi Mungu amewatuma kuwatoa wanadamu kutoka katika ibada ya waja wengine hadi kwenye kumwabudu Mola wa waja wote.” Ijapokuwa kauli hii ilitolewa ili kubainisha lengo la ujumbe mtukufu wa Uislamu, unaowakirimu watu kutokana na kumwabudu kwao Mwenyezi Mungu, na kuhifadhi maisha yao, mali zao na heshima zao, hii wakati fulani hujidhihirisha kama kauli iliyo kinyume chake. Rehema ya Uislamu na uhuru unaowadhaminia watu unakinzana na utumwa wa watu na mataifa kwenye ukoloni, ambao unawaona kuwa ni mashini tu za kuzalisha dhahabu na pesa.

Soma zaidi...

Uislamu Uliingiaje Sudan?

Kabla ya kuwasili kwa Uislamu, eneo linalojulikana leo kama Sudan halikuwa umbo lililounganishwa kisiasa, kitamaduni au kidini. Ilikuwa makao ya makabila, desturi, na imani mbalimbali. Upande wa kaskazini, Wanubi walifuata Ukristo wa Kiorthodoksi, na lugha ya Kinubi, pamoja na lahaja zake mbalimbali, ilikuwa njia ya siasa, utamaduni, na mawasiliano. Katika mashariki, makabila ya Beja, vizazi vya Hamu (mwana wa Nuhu), walikuwa na lugha yao wenyewe tofauti, utamaduni, na matendo ya kidini. Upande wa kusini, makabila ya Zanj, yenye sifa na lugha zao za kipekee, yalishikamana na imani za kipagani, na tofauti kama hizo zilikuwepo katika upande wa magharibi.

Soma zaidi...

Mtihani wa Gaza

Mwenyezi Mungu (swt) hakumuumba mwanadamu bila ya kuweka mbele yake mitihani kulingana na ukubwa wa Imani yake na kujitolea kwake katika Dini, ili Mwenyezi Mungu (swt) apate kujua ni nani atakayekuwa na subira mbele ya mitihani hiyo na kuweka tegemeo lake (tawakkul) kwa Mwenyezi Mungu (swt) . Haya ni ili Mwenyezi Mungu (swt) amuepushe na fitna. Ama wale ambao watafeli ndani ya mitihani hiyo, watafeli tu kwa sababu ya hukumu yao mbaya, kughafilika kwao na Amri za Mwenyezi Mungu (swt), na Imani yao dhaifu.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu