Uhadaifu wa Utaifa
- Imepeperushwa katika Uchambuzi
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Baada ya wakoloni kuugawanya ulimwengu wa Kiislamu, walifanya kazi kuelekea kubadilisha mfumo wake wa utawala. Mifumo ya bunge ilianzishwa na maafisa wa kikoloni wangejihusisha na raia wao iwapo tu wangekubali kujipanga katika muundo wa vyama vya kidemokrasia. Walioletwa madarakani na wakoloni ni wale waliokubali sheria na kanuni zao. Kuibuka kwa dola za kitaifa katika ulimwengu wa Kiislamu kwa hiyo kunahusishwa kwa namna isiyoweza kutenganishwa na historia ya ukoloni na kulazimishwa na dola za Ulaya zilizotaka kuona ulimwengu wa Kiislamu ukigawanyika.