Ripoti ya Kadhia ya Hamza si ya Kuaminika, na Inadhihirisha Uwongo katika Kesi za Ugaidi Tanzania
- Imepeperushwa katika Habari na Maoni
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Mnamo tarehe 2 Septemba, 2021 Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) nchini Tanzania Bw. Camilius Wambura alitoa ripoti yake kuwa Hamza Mohamed (30) mfanyabiashara na mwanachama wa chama tawala (CCM) aliyeuawa na polisi siku ya tarehe 25 Agosti 2021 baada ya kuwaua askari watatu na mlinzi mmoja jijini Dar es Salaam kwamba alikuwa gaidi wa kujitoa muhanga.