Jumanne, 06 Muharram 1447 | 2025/07/01
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Ukamataji wa Waislamu nchini Urusi

Vikosi vya usalama vilipandikiza kazi za SIM wakati wa upekuzi katika nyumba za Waislamu, kesi za kushiriki katika shirika la kigaidi zilitungwa, jamaa zao walisema katika malalamiko kwa wanaharakati wa haki za binadamu. Kwa jumla, watu 48 walizuiliwa wakati wa operesheni ya vikosi vya usalama huko Nalchik na Nartan, Kavkazsky Uzel (tovuti ya habari) iliripoti mnamo Juni 3, ikinukuu wanaharakati wa haki za binadamu.

Soma zaidi...

Sheria ya Kimataifa ni Sheria ya Pori - Hairuhusiwi Kuiendea

Chini ya ufadhili wa Daniel Capoli, Mratibu wa Masuala ya Kibinadamu katika misheni ya Kamati ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu (ICRC) nchini Yemen, ICRC huko Sana'a ilipanga, mnamo Jumanne na Jumatano, 20-21/05/2025, kwa ushirikiano na Wizara ya Habari na Wizara ya Mambo ya Nje, kozi ya mafunzo katika Wizara ya Mambo ya Nje kwa wafanyikazi wa vyombo vya habari na taasisi ya waandishi wa habari. Kozi hiyo ilishughulikia sheria za kimataifa, misingi na malengo yake, na istilahi zinazohusiana na sheria za kimataifa za kibinadamu, haswa katika suala la haki za binadamu katika ulinzi na maisha yenye staha, kuzuia ghasia, na kukidhi mahitaji ya vikundi vilivyo hatarini zaidi vinavyofinikwa na ulinzi wake, na vile vile kulinda raia dhidi ya athari za uhasama na kuharamisha mateso yasiyo na haja au madhara kupita kiasi.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Yemen Inawapongeza Watu wa Imani na Hekima na Umma wa Kiislamu kwa Sikukuu ya Idd al-Adha iliyobarikiwa

Hizb ut Tahrir / Wilayah Yemen inatoa pongezi zake za dhati na baraka zenye thamani kubwa zaidi kwa watu wa imani na hekima, na kwa Amiri wa Hizb, mwanachuoni mkubwa Ata Bin Khalil Abu Al-Rashtah, na kwa wanachama wote wa Hizb, na kwa Ummah mzima wa Kiislamu kwa sikukuu ya Idd al-Adha iliyobarikiwa mwaka huu wa 1446 H. Mwenyezi Mungu airudishe kwao, juu yetu, na juu ya ulimwengu wote kwa kheri, baraka, na furaha.

Soma zaidi...

Kutoka Pakistan hadi ash-Sham: Je, Kweli Tulimshinda Bashar au Tulimbadilisha tu kwa Nakala zake?!

Wakati miji yote ilipokombolewa kutoka mikononi mwa dhalimu wa ash-Sham, Bashar, tulifikiri ushindi ulikuwa umefika. Tuliamini kuwa wakati umefika wa kusimamishwa Khilafah kwa njia ya Utume—hali ile ile iliyobashiriwa na Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw)—ambayo itatawala kwa Qur’an na Sunnah na ilionekana iko tu kwenye kona. Walakini, kuvunjwa moyo kulilingana na ukubwa wa mihanga, na usaliti ulifuata takriban miezi sita baada ya wanamapinduzi kuingia Damascus kwa takbira na shangwe za ushindi. Usaliti ulikuja kutoka kwa wale tuliotarajia wangejenga upya juu ya magofu—sio kujisalimisha kwao!

Soma zaidi...

Pongezi kutoka Hizb ut Tahrir/ Wilayah ya Sudan Kwa Mnasaba wa Idd Al-Adha 1446 H

Sisi, katika Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan, tunafuraha kuwapongeza watu wetu nchini Sudan na Umma wote wa Kiislamu kwa mnasaba wa Idd Al-Adha. Mwenyezi Mungu airudishe kwetu, tukiwa Ummah ulioungana chini ya bendera ya Al-Uqab, bendera ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw), chini ya kivuli cha Khilafah Rashida kwa njia ya Utume.

Soma zaidi...

Ujerumani Yapoteza Fursa ya Kihistoria

Katika maadhimisho ya miaka 60 ya kuanzisha mahusiano ya kidiplomasia na umbile la Kiyahudi, Jamhuri ya Shirikisho ya Ujerumani inapoteza fursa yake ya kihistoria ya kujikomboa kutoka katika hatia iliyotungwa dhidi ya Mayahudi. Badala yake, shauku ya kile kinachoitwa "maslahi makuu ya kitaifa" - kisingizio kinachotumiwa kuhalalisha uungaji mkono usio na masharti kwa umbile la Kiyahudi - yamefikia kilele kipya kwa tangazo kwamba kuunga mkono umbile hili ni "msingi wa kuwepo kwa Ujerumani"!

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir/ Wilayah Pakistan: Jeshi la Anga la Pakistan lazima liongoze kampeni ya anga (Operesheni Kimbunga cha Al-Aqsa) dhidi ya umbile la Kiyahudi na Makruseda!

Jeshi la India lilithibitisha kwa mara ya kwanza mnamo 31 Mei 2025 kwamba lilikuwa limepoteza idadi isiyojulikana ya ndege za kivita katika mapigano na Pakistan mnamo Mei mwaka jana. Enyi mwewe wa nchi hii safi! Umbile la Kiyahudi linafanya mauaji makubwa dhidi ya watoto wetu, dada na babu zetu, na hamkusonga! Kwa fadhila na upendeleo wa Mwenyezi Mungu ﷻ, muna uwezo wa kuongoza “Vita Vikuu vya Angani” dhidi ya vikosi vya kikatili vya Netanyahu na Trump.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Yahuisha Ibada ya Takbira Katika Mwezi wa Dhul-Hijjah kwa Matembezi ya Kishindo katika Soko Kuu la Port Sudan

Baada ya swala ya Alasiri mnamo siku ya Jumatatu, tarehe 6 Dhul-Hijjah 1446 H, sawia na tarehe 2 Juni 2025 M, Mashababu wa Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan walihuisha ibada ya takbira katika mwezi wa Dhul-Hijjah. Ustadh Muhammad Jami’ (Abu Ayman), Msaidizi wa Msemaji wa Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Sudan, alihutubia waumini katika Msikiti wa Ibn Mas’ud katika soko kuu la Port Sudan baada ya Swalah ya Alasiri, akiwakumbusha juu ya ubora wa siku hizi zilizobarikiwa za Dhul-Hijjah, na jinsi Maswahaba – Mwenyezi Mungu awe radhi nao – walivyozitukuza siku hizi kwa takbira na tahleel. Kisha akaanza kupiga takbira, ikifuatiwa na dua. Baadaye wote wakatoka kwa matembezi ya kishindo wakiwa wamebeba Rayah (bendera) ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw), na alama kubwa isemayo: "Kuhuisha Ibada ya Takbira katika Mwezi wa Dhul-Hijjah."

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu