Jumamosi, 21 Muharram 1446 | 2024/07/27
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Hatuwezi Kuishi bila Mfumo wa Sasa wa Ulimwengu

Imani kwamba hatuwezi kuishi bila mfumo wa sasa wa ulimwengu labda ndio kikwazo kikubwa kwa usalama wa watu wa Palestina. Iwe kwa kujua, au kutojua, imani hii inaonekana kushikiliwa na watu kote ulimwenguni huku wakiendelea kujaribu kutumia njia za kidemokrasia kuwasaidia watu wa Palestina, licha ya ukweli kwamba wamewafelisha watu kote ulimwenguni.

Soma zaidi...

Operesheni Nyengine Dhidi ya Ugaidi

Uongozi wa juu wa Pakistan umeidhinisha kuanzishwa kwa operesheni mpya ya kijeshi Inayoitwa Azm-e-Istehkam. Mpango huo mpya wa kijeshi unatarajiwa kuangazia vitisho vya usalama wa ndani na wapiganaji wenye silaha wanaovuka kutoka Afghanistan, huku kukiwa na taharuki inayoongezeka kati ya Islamabad na watawala wa Taliban jijini Kabul.

Soma zaidi...

Sintofahamu ya Benki ya Maziwa ya Binadamu: Khilafah kwa Njia ya Utume Inatatua Matatizo ya Kibinadamu kwa Kuregelea Uislamu

Gazeti la ‘The Daily Times’ liliripoti kuwa, “Sindh anasimamisha benki ya maziwa ya binadamu, inauregesha mpango huo kwa Baraza la Itikadi la Kiislamu... Benki ya kwanza ya maziwa ya binadamu nchini Pakistan iliundwa mapema mwezi huu na Taasisi ya Sindh ya Afya ya Mtoto na Matibabu ya Watoto (Neonatology)

Soma zaidi...

Watawala wa Pakistan wanatekeleza Ukamataji ili Kuzuia Hizb ut Tahrir Kutaka Kuhamasishwa kwa Jeshi la Pakistan Kuinusuru Gaza. Badala ya Kushambulia umbile la Kiyahudi, Watawala Wanawashambulia Waislamu

Huku Mayahudi wa Kizayuni wakivuka mipaka yote katika ukatili wao, wito wa kampeni ya kisiasa ya Hizb #ArmiesToAqsa umefika kila barabara na kila kona, kwa Fadhila za Mwenyezi Mungu (swt). Wanafunzi wa vyuo vikuu mbalimbali, viongozi wa kisiasa, wanaharakati wa mitandao ya kijamii na umma kwa jumla sasa wote wanazidi kuimba, “Enyi Majeshi ya Waislamu, nendeni Palestina, nendeni Palestina.”

Soma zaidi...

Jitihada Zinazorudiwa rudiwa, za Kutapatapa za Kuinasibisha Hizb ut Tahrir na Uanamgambo, ni Kwa sababu Magharibi Inaogopa Kuporomoka kwa Mfumo Wake Fisadi wa Kilimwengu, katika Ulimwengu wa Kiislamu

Ni dhahiri kwamba mfumo wa Hizb, Uislamu, ni tishio la kuwepo kwa mfumo wa kilimwengu wa Magharibi. Uislamu unakataa ubwana wa akili ya mwanadamu, na haki ya wanadamu kutunga sheria. Uislamu unatangaza ubwana pekee ni wa Mwenyezi Mungu (swt), na utabikishaji hukmu za Shariah. Uislamu unaamuru kuunganisha Ummah kama Umma mmoja, na unakataa mipaka ya kitaifa ambayo iliwekwa na wakoloni makafiri, ili kuwagawanya Waislamu katika zaidi ya dola hamsini.

Soma zaidi...

Marufuku ya Hijab ya Ubelgiji: Kutopendelea upande wowote kama Haki mpya ya Kimungu (Droit Divin)

Mahakama ya Ulaya ya Haki za Kibinadamu (ECHR) imeidhinisha marufuku ya Ubelgiji ya kuvaa hijab shuleni, uamuzi ambao umezusha mijadala kuhusu uhuru wa kidini na usekula barani Ulaya. Mahakama ilipata kwamba marufuku hiyo, iliyokusudiwa kuhakikisha ‘kutopendelea upande wowote’ katika elimu ya umma, haikiuki Mkataba wa Ulaya wa Haki za Kibinadamu. Kesi hiyo ilianzishwa na mwanafunzi mmoja Muislamu ambaye alidai kuwa sera hiyo inakiuka haki zake za uhuru wa dini na elimu. Hata hivyo, ECHR iliamua kwamba marufuku hiyo ilihalalishwa na haja ya kudumisha ‘kutopendelea upande wowote,’ kama ilivyotarajiwa.

Soma zaidi...

Ash-Sham ndio Nyumba ya Khilafah

Tunaweza kusema kwamba kuwasili kwa Khilafah katika Bait ul Maqdis kuna dalili zaidi ya moja. Ya kwanza ni kwamba Bait ul Maqdis ni eneo la kihistoria, kisiasa na kijografia la ulimwengu wa kale. Ni kitovu cha dini zote na kitovu cha umakini wao. Yeyote anayeidhibiti atatawala ulimwengu wa zamani. Hii ina maana kwamba pale Khilafah itakaposimamishwa, basi Waislamu watatawala ulimwengu mzima licha ya Mayahudi na Wakristo kuwa dhidi yao. Pili ni malipo kwa watu wa Ash-Sham kwa yale yaliyowapata na maumivu, kuvunjika, subira na uvumilivu waliyopitia kwa miongo mingi.

Soma zaidi...

Kifurushi Kipya cha Ushuru Kinathibitisha Jinsi Wale Wanaojipamba kwa Neno “Uadilifu” Walivyo Wakatili

Ufahamu wa mfumo wa mahakama wa Uturuki kuhusu uadilifu ni kuwaadhibu Waislamu wanaopinga ukatili unaofanywa dhidi ya Waislamu nchini Uturuki na duniani kote, na kuwaachilia huru wanasiasa wanaolaghai umma, na ni kuwatangaza Waislamu wenye fikra za Kiislamu, na wanaotamani maisha ya Kiislamu, ambao hawajatenda jinai yoyote, kuwa ni magaidi na kuwahukumu kwenye dhulma, mateso na kifungo.

Soma zaidi...

Tukio la Bek-Abad: Mateso na Mashtaka ya Uongo

Huduma ya Usalama wa Taifa ya Kyrgyz iliwakamata wasichana wawili wenye umri wa miaka 16 na 19 katika kijiji cha Bek-Abad katika eneo la Suzak, na wanatuhumiwa kubadilisha bendera ya dola katika maeneo kadhaa. Mbali na ukaguzi huo uliofanyika mnamo Mei 31 na Juni 4, uliopelekea dada 4 wa Kiislamu kuwekwa chini ya uchunguzi kuhusiana na tukio hilo.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu