Jumamosi, 30 Jumada al-thani 1447 | 2025/12/20
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Yafanya Kisimamo katika eneo la Nile Mashariki

Leo, Jumatano, tarehe 25 Rabi’ al-Awwal 1447 H sawia na 17 Septemba 2025 M, Mashababu wa Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan katika eneo la Nile Mashariki walifanya kisimamo baada ya Swala ya Adhuhuri katika Msikiti Mkuu wa Souq Sitta Al-Wahda. Ndani yake, mabango yaliinuliwa kuwataka Waislamu kusimama kidete kuzuia njama ya kuichana Sudan kwa kuitenganisha Darfur.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Yakutana na Sheikh Farouq Al-Haj Abdullah Al-Sheikh Dafa’ Allah

Mnamo Jumanne, tarehe 16/09/2025, ujumbe wa Kamati Kuu ya Mawasiliano ya Hizb ut Tahrir katika Wilaya ya Sudan, ukishirikiana na Bw. Abdullah Hussein, mratibu wa kamati hiyo, na Sheikh Abdul Qader Abdul Rahman, mwanachama wa Hizb, ulikutana na Sheikh Farouq Al-Haj Abdullah Abdullah Al-Sheikh Dafa’ Allah, Katibu wa Sekretarieti ya Utamaduni wa Da’wah ya Kabila la Al-Kalaklat.

Soma zaidi...

Chama cha Jumuiya ya Mageuzi ya Yemen (Islah), Sura ya Kiislamu ya Serikali Inayodai kuwa ni ya Kiislamu, Lakini iko Mbali Nao!

Mohammad Abdullah Al-Yadoumi, Mwenyekiti wa Baraza Kuu la chama cha Jumuiya ya Mageuzi ya Yemen (Islah), alitoa hotuba Ijumaa jioni, 12/9/2025, kuadhimisha miaka 35 tangu kuanzishwa kwa chama hicho, ambayo ilikuwa Septemba 13. Hotuba hiyo, iliyopeperushwa na Suhail TV na kudumu kwa zaidi ya dakika  arubaini, ilijumuisha msimamo wa chama hicho juu ya masuala ya ndani na ya kimataifa.

Soma zaidi...

Uchaguzi wa Kidemokrasia si Lolote ila Minong'ono ya Ibilisi

Mnamo 13 Septemba 2025 kinyang’anyiro cha kuwania urais wa Zanzibar kilianza rasmi huku chama tawala – Chama Cha Mapinduzi (CCM) na chama cha upinzani cha ACT-Wazalendo kikizindua kampeni zao. CCM ilisisitiza ‘utulivu’, ‘amani’ na ‘umoja’, huku chama cha ACT Wazalendo kikiweka kipaumbele katika uwajibikaji, usawa, na fursa za kiuchumi.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Kisimamo cha Port Sudan cha Kutibua Mpango wa Kujitenga kwa Darfur!

Kujibu kwa takbira, tahlil, na uungaji mkono, pamoja na vyombo vya habari na uhamasishaji wa kisiasa, kisimamo kilifanywa na Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan kutibua mpango wa kujitenga kwa Darfur kilifanyika mbele ya Msikiti Mkuu mjini Port Sudan. Waumini walikusanyika baada ya swala ya Ijumaa, 20 Rabi' al-Awwal 1447 H - 12 Septemba 2025 M, kwenye Msikiti Mkuu mjini Port Sudan kwa ajili ya kisimamo hicho ikiwa ni sehemu ya kampeni ya hizb kutibua mpango wa kujitenga kwa Darfur.

Soma zaidi...

Kukamatwa kwa Mamia ya Waandamanaji Wanaounga Mkono Palestina kwa Amani nchini Uingereza Yaonyesha Uhalisia wa Kinaya cha Demokrasia

Mnamo Jumamosi, tarehe 6 Septemba, karibu watu 900 walikamatwa katika maandamano ya kuunga mkono Palestina jijini London. Walikuwa wakipinga kuendelea kwa mauaji ya halaiki na njaa kwa raia wasio na hatia mjini Gaza, pamoja na kupigwa marufuku kwa kundi la Palestine Action ambalo serikali ya Uingereza iliharamisha kuwa shirika la kigaidi mwezi Julai. Waliokamatwa ni pamoja na maaskofu, makasisi, walimu, madaktari, wahudumu wengine wa afya, na vizazi vya wahanga wa mauaji ya Holocaust pamoja na waandamanaji walemavu. Wengi walikuwa wazee – katika miaka yao ya 60, 70 na hata 80 – na walijumuisha mzee mmoja kipofu mwenye umri wa miaka 62 aliye katika kiti cha magurudumu.

Soma zaidi...

Sudan: Giza la Muundo wa Makubaliano au Nuru ya Katiba Inayotokana na Kitabu cha Mwenyezi Mungu na Sunnah ya Mtume Wake?

Haishangazi kwa mtu yeyote anayefuatilia hali ya kisiasa nchini Sudan kujua kwamba vita hivi viliratibiwa na kusimamiwa na Marekani chafu na yenye nia mbaya ili kufanikisha ajenda yake na kuvunja nguvu za washindani wake wa Ulaya, hasa raia wanaoshirikiana na Uingereza. Vita hivi vinafadhiliwa na Amerika, ni mchezo wao uliolaaniwa. Ushahidi wa wazi zaidi ni kwamba taarifa kuhusu kurefusha vita ilitoka kwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Blinken. Kurefushwa kwa vita hivi si kwa ajili ya utatuzi au kuhifadhi damu au kukomesha uharibifu ambao umeharibu nchi na watu wake; badala yake, ni mapambano ya nyuma na mbele na jaribio la kuweka maono ya kisiasa ambayo yanahakikisha na kuhifadhi maslahi ya Marekani nchini.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu