Mpango wa Trump wa Gaza ni Mpango Muovu wa Usaliti Unaolenga Kuangamiza Kadhia ya Palestina
- Imepeperushwa katika Habari na Maoni
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Rais wa Marekani Donald Trump alitangaza kuwa Waziri Mkuu wa “Israel” Benjamin Netanyahu amekubali mpango wenye vipengee 20 ambao ungemaliza vita katika Ukanda wa Gaza. Trump na Netanyahu walifanya mkutano wa pamoja na waandishi wa habari baada ya mkutano wao jijini Washington. Trump alisema kuwa amani ya Gaza ilikuwa karibu sana kupatikana na kumshukuru Netanyahu kwa kuidhinisha mpango huo (DW Turkish 29.09.2025).



