Jumamosi, 30 Jumada al-thani 1447 | 2025/12/20
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Enyi Watu wa Sudan, Amerika Inaharakisha Kuvuna Matunda ya Vita vyake nchini Sudan, Kwa hivyo Msiiruhusu Itenganishe Darfur

Wakati wa hotuba yake katika Kikao cha Uwekezaji kati ya Marekani na Saudi Arabia, Rais wa Marekani Donald Trump alisema kwamba Mfalme Mtarajiwa Mohammed bin Salman alikuwa ameomba azimio la mgogoro nchini Sudan, akiongeza kwamba alianza kusoma suala hilo nusu saa tu baada ya maelezo ya Mwanafalme huyo. Trump pia aliandika kwenye tovuti yake ya Kijamii ya Truth kwamba atatumia mamlaka ya urais kusimamisha vita mara moja.

Soma zaidi...

Jibu la Swali: China na Ukombozi Wake Kutoka kwa Mtazamo Wake Mdogo wa Kikanda

 “China inamiliki hisia ya nguvu na mapambano, na kama lengo la China halikufungika tu na kudumisha eneo lake, na kukubali kukabiliana na Amerika kama jibu tu kwa harakati za Amerika kuelekea eneo lake, China haisubutu kupambana na Amerika katika maeneo yao ya ushawishi... na kama isingeanza kutumia ubepari katika nyanja nyingi, haswa katika uchumi... ingekuwa na sauti kubwa kimataifa, na athari yake kwa maslahi ya Amerika ingekuwa na nguvu zaidi. China kwa vyovyote vile ina hisia kali ya nguvu, na inafanya kazi ili kudumisha ubwana wa eneo lake, hata kama iko katika eneo lake...” — Kwa hivyo, je, kizuizi cha China cha mauzo ya nje ya madini adimu ya ardhini kwenda Amerika, kuyauza kwa dhamana za Hazina ya Marekani, kulisasisha jeshi lake, na kujenga jengo kubwa zaidi la kijeshi duniani kusini magharibi mwa Beijing... je, hiki si kiashiria cha ukombozi wa China kutoka kwa mtazamo wake wa kisiasa uliofungika katika eneo lake na upanuzi wa mtazamo huu kushindana na Amerika duniani kote?

Soma zaidi...

Jibu la Swali: Ruwaza ya Marekani ya Kutatua Kadhia ya Cyprus

“Afisi ya rais wa Uturuki ilitangaza mnamo Jumatatu kwamba Rais wa Jamhuri ya Uturuki ya Cyprus Kaskazini, Tufan Erhürman, atatembelea Ankara Alhamisi ijayo, 13/11/2025... Burhanettin Duran, mkuu wa idara ya mawasiliano ya rais wa Uturuki, alisema kwamba ziara ya Erhürman Ankara inakuja kutokana na mwaliko wa Rais Erdoğan, na Duran aliongeza kwamba ziara hiyo itakuwa kituo cha kwanza cha kigeni cha Erhurman... Na mnamo tarehe 19 Oktoba Bodi Kuu ya Uchaguzi ya Uturuki ya Cyprus ilitangaza ushindi wa kiongozi wa Chama cha Republican cha Kituruki, Tufan Erhürman, katika uchaguzi wa rais.” (Shirika la Anadolu, 10/11/2025). Kwa hivyo ni nini kimesababisha maridhiano haya? Ikifahamika kwamba Erhurman, wakati wa kampeni yake ya uchaguzi, alikuwa akitoa wito wa kuunganisha kisiwa hicho, huku Erdogan akitoa wito wa dola mbili? Na je, Amerika iko nyuma ya maridhiano hayo? Na Mwenyezi Mungu akulipe kheri.

Soma zaidi...

Trump Awaongoza Wafuasi wake kutoka kwa Watawala katika Ardhi za Waislamu kwenye Mkataba wa Fedheha na Aibu, Wakiinamisha Vichwa Vyao Nyuma Yake kwa Kuiweka Gaza Hashem chini ya Usimamizi na Ukoloni!

“Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lilipitisha alfajiri ya Jumanne mpango wa Rais wa Marekani Donald Trump kuhusu Ukanda wa Gaza baada ya kuidhinisha rasimu ya azimio lililowasilishwa na Marekani na kuunga mkono mpango wa amani wa Trump katika sekta hiyo, na Rais Trump aliisifu kura ya Baraza la Usalama kuhusu azimio la Gaza kama wakati wa kihistoria...” (BBC, 18/11/2025). Kuhusu Azimio Nambari 2803, lilichapishwa na vyombo vya habari na lilikuwa ni idhini ya mpango wa pointi 20 wa Rais Donald Trump wa kukomesha mzozo mjini Gaza, lililotolewa mnamo tarehe 29 Septemba 2025.

Soma zaidi...

Waislamu Maskini Wanastahili Zaidi Uwekezaji wa Watawala Wapumbavu Kuliko Amerika

Mfalme Mtarajiwa wa Saudi Arabia alifanya ziara nchini Marekani mnamo Jumanne, 18/11/2025, ambapo alionyesha kiwango cha upumbavu wake katika kufuja utajiri wa Ummah, kiwango cha utiifu wake kwa bwana wake Amerika, pamoja na kiwango cha usaliti wake kwa Ummah wa Kiislamu, njama yake dhidi yake, na vita vyake dhidi ya Mwenyezi Mungu (swt) na Mtume Wake (saw) kwa kukubali kujiunga na Makubaliano ya Abraham, yaliyowekwa katika usaliti mwingine ambao unahakikisha njia iliyo wazi ya suluhisho la dola mbili.

Soma zaidi...

Je, Watoto Wafungwa Katika Magereza ya Uvamizi ni Watoto au Wanaume?!

Taasisi za Palestina zinazohusika na masuala ya wafungwa, ikiwemo Klabu ya Wafungwa, zilisema kwamba zaidi ya watoto 1630 kutoka Ukingo wa Magharibi, ikiwa ni pamoja na al-Quds, na makumi kadhaa kutoka Ukanda wa Gaza wamekamatwa na uvamizi tangu mwanzo wa vita dhidi ya Gaza. Waliashiria kuuawa shahidi kwa mtoto mmoja ndani ya Gereza la Megiddo baada ya kukabiliwa na njaa, kunyimwa, na unyanyasaji. 350 kati yao bado wako katika magereza ya uvamizi, wakiwemo wasichana wawili, katika hali ngumu ambazo zinagongana kabisa na viwango vyote vya kimataifa vya ulinzi wa watoto. Wanakabiliwa na uhalifu wa mateso, njaa, na kupuuzwa kimatibabu, vilevile kudhulumiwa kijinsia, pamoja na kutengwa kwa pamoja na kunyimwa kutembelewa.

Soma zaidi...

Ukosefu wa Masuluhisho ya Kudumu kwa Mgogoro wa Rohingya

Gazeti la ‘South China Morning Post’ liliripoti mnamo tarehe 10 Novemba kwamba Umoja wa Mataifa umeonya kwamba Kusini-mashariki mwa Asia kuna hatari ya “janga jengine la kibinadamu” ikiwa uvukaji wa bahari wa wakimbizi waliokata tamaa utaendelea bila kudhibitiwa. Vifo vya watu wasiopungua 21, wakiwemo watoto kadhaa, katika ajali ya boti karibu na pwani ya Malaysia vimeibua hofu ya kuongezeka tena kwa uvukaji hatari wa bahari wa wakimbizi wanaokimbia mzozo nchini Myanmar na hali mbaya katika nchi jirani ya Bangladesh. Kulikuwa na miili 12 iliyopatikana nchini Malaysia na tisa katika nchi jirani ya Thailand – kulingana na mkuu wa eneo wa shirika la bahari la Malaysia, Romli Mustafa.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu