Jarida la UQAB Toleo 60 - Januari 2022
- Imepeperushwa katika Jarida la UQAB
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Hizb ut Tahrir Wilayah ya Kenya imechapisha toleo jipya la Jarida la UQAB kwa ajili ya mwezi wa Januari 2022 M.
Hizb ut Tahrir Wilayah ya Kenya imechapisha toleo jipya la Jarida la UQAB kwa ajili ya mwezi wa Januari 2022 M.
Kwanza, naomba radhi kwa maswali mengi ambayo yawafikia kutoka kwangu. Lakini tumejifunza kwenye hizb kuwa tupekue na tutafiti, ili fikra yetu ibakie kuwa yenye nguvu na safi kwa uwezo wake Mwenyezi Mungu mtukufu.
Swali kuhusu ukusanyaji wa Qur’an tukufu zama za Abubakar As-Swidiq radhi za Mwenyezi Mungu zimwendee.
Sarafu ya taifa ya Uturuki, lira ya Uturuki, imeporomoka sana katika robo ya mwisho ya mwaka huu, kutoka lira 8.86 za Uturuki kwa dolari moja mwezi Oktoba hadi lira 16.42 za Uturuki kwa dolari moja ya Marekani.
Katika kipindi cha miezi miwili iliyopita, Uturuki ilikuwa ikipitia mgogoro mkubwa wa kiuchumi.
Huku uhusiano ukizidi kuwa mbaya kati ya Beijing na Washington, Rais Joe Biden alitia saini sheria mpya mnamo siku ya Alhamisi (24 Disemba 2021) ya kupiga marufuku bidhaa zinazotengenezwa katika jimbo la Xinjiang la China kwa sababu ya ukandamizaji wa China kwa idadi yake kubwa ya Waislamu wa Uighur walio wachache.
Mwenendo wa kihistoria wa kesi za Hizb ut Tahrir nchini Uturuki umejaa kashfa za kisheria.
BBC iliripoti mnamo tarehe 2 Disemba kwamba miundombinu inayoporomoka ya Afghanistan imesababisha kukaribia kutoweka kwa mfumo wa huduma za afya na ustawi wa jamii.
Waziri wa Mambo ya Nje Shah Mahmood Qureshi mnamo siku ya Alhamisi, tarehe 16 Disemba 2021, alisema kuwa pamoja na wanachama wa jumuiya ya kimataifa na Taliban kuwepo kwenye jukwaa moja, mkutano wa Disemba 19 wa OIC jijini Islamabad utathibitisha kuwa ni ngazi ya kutafuta suluhisho la janga la kibinadamu nchini Afghanistan.