Jumatatu, 03 Rajab 1447 | 2025/12/22
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Al-Waqiyah TV: Kwa Nini Kuwahisabu Watawala ni Faradhi ya Kisheria

Unapomteua mtu wa kutekeleza jukumu ambalo asili yake ulikabidhiwa, hii ina maana kwamba ni wajibu wako wa Shariah kumfuatilia na kumhisabu ikiwa ameghafilika, anafanya makosa, au anadhulumu, na kadhalika. Ni jambo la kawaida kwa Ummah kuendelea kuwa macho juu ya mtawala. Haya ni faradhi yake ya Shariah na Shariah yake kwa wakati mmoja. Maana ya faradhi yake ya Shariah ni kuwa Ummah utakuwa ni wenye dhambi ukilipuuza hili. Haki yake Shariah ni kwamba mtawala atatenda dhambi ikiwa atauzuia kutekeleza wajibu wa kuhisabu, ufuatiliaji, na ushauri, na kadhalika.

Soma zaidi...

Wakati Mahouthi Wakishangilia Uhamasishaji wa Makabila ya Bakil na Hashid na Kupigwa kwa Ngoma za Vita Baina Yao!

Mnamo Jumamosi, 26/07/2025, Sheikh Hamid Mansour Radman aliuawa katika eneo la Al-Hayit, Wilaya ya Ayal Surayh, katika Mkoa wa Amran, na mkwe wake, Hamir Saleh Rattas Falyatah (Abu Udhr) mkuu wa idara ya polisi ya Al-Hayit. Mauaji ya Sheikh Radman yalikuja baada ya kuondoka nyumbani kwake, kufuatia mzozo wa kifamilia. Muuaji anashikilia wadhifa wa mkuu wa idara ya polisi, ambaye wajibu wake ni kulinda maisha, mali, na heshima, na kuhakikisha faraja na usalama wa jamii, kuondoa shida zake, kudumisha amani kote, na kuwazuia wakjukaji na wavamizi dhidi ya maisha ya watu – sio kumuua bamkwe wake kwa kukusudia kwa kumpiga risasi kwenye barabara ya umma!

Soma zaidi...

Tarehe 5 Agosti 2024 ni Siku ya Uasi wa Watu dhidi ya Dhalimu na Utawala wa Kidhalimu, ambao ungali Unaendelea; kinachojulikana kama 'Tangazo la Julai' ni Hati ya Usaliti wa Vyama vya Kisiasa vinavyounga mkono Marekani ili kuangamiza Uasi wa Watu

Wananchi wakiwa wamekata tamaa sana, wamepita mwaka mmoja tangu kuanguka kwa Hasina katika uasi mkubwa dhidi ya dhalimu Hasina na utawala dhalimu mnamo Agosti 5, 2025. Kwa sababu baada ya kuanguka kwa dhalimu Hasina, vibaraka wa Marekani na vyama vya kisiasa vyenye uchu wa madaraka vimechukua mshiko wa kubainisha hatima ya watu na kuweka vikwazo katika kutekeleza matumaini na matarajio ya watu na wameendelea na majaribio yao maovu na kuteka nyara uasi huo. Kinachojulikana kama 'Tangazo la Julai' ni hatua isiyo na aibu ya jaribio hili ovu. Watu wamekataa utumwa wa Marekani na sarakasi za kisiasa kwa chuki. Yaliyo mbali na kuakisi matarajio ya watu, Tangazo hili la Julai halitambui hata matukio kama vile njama ya India huko Pilkhana na mauaji ya halaiki ya watu wanaopenda Uislamu huko Shapla Chattar.

Soma zaidi...

Ni Lazima ikumbukwe kwamba Marekani ni Nchi ya Kikoloni; Kujisalimisha kwa Sera zake za Ushuru Kutahatarisha Ubwana wa Taifa!

Marekani, mchuuzi wa kimataifa wa ubepari, imeibua 'dhoruba ya ushuru' duniani kote, ikipuuza kanuni za uchumi wa soko huria – moja ya falsafa kuu za ubepari – na sheria na kanuni za kile kinachojulikana kama Shirika la Biashara Duniani (WTO) ililounda. Hii, kwa mara nyingine, inathibitisha kwamba mfumo wa kibepari hauna utu na wa kinyonyaji. Serikali ya mpito ya Bangladesh imetabanni sera ya utiifu katika kukabiliana na hatua za ushuru za Marekani. Tayari wamefanya uamuzi wa kujitoa mhanga kununua ndege 25 za gharama kubwa aina ya Boeing, pamoja na kuagiza pamba na LNG kutoka Marekani, ingawa nchi nyingi zinaghairi oda zao kutokana na utendakazi duni wa Boeing. Na wanafanya mikutano ya moja kwa moja na Marekani, wakiweka umma katika giza kupitia 'makubaliano fiche ya kihistoria' (NDA).

Soma zaidi...

Sudan: Janga la Karne Lililofichika Machoni mwa Ulimwengu

Dola ya Kiislamu, mlinzi wa watu wake, haipo. Waislamu wameishi katika taabu, mateso, na majanga duniani kote. Sudan hivi sasa inakabiliwa na moja ya majanga mabaya zaidi ya kibinadamu katika historia ya kisasa kutokana na mapigano ya umwagaji damu ambayo yamekuwa yakiendelea kwa miaka miwili kati ya jeshi na Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF), na kusababisha maafa ya kutisha ambayo hakuna anayezungumza au kujaribu kuzuia. Huu ni mzozo uliosahaulika ambao vyombo vya habari haviupi mwanga, na ambao maelezo yake hayafichuliwi na dola yoyote au hata taasisi zake.

Soma zaidi...

Mbwa Mwitu Hapaswi Kulaumiwa kwa Uvamizi wake ikiwa Mchungaji ndiye Adui wa Kondoo

Watoto watatu walifariki katika Jimbo la Khartoum baada ya kupokea dozi ya chanjo ya ukambi. Wizara ya Afya imefungua uchunguzi kuhusu dhurufu za vifo vyao. Sudan Tribune iligundua kuwa watoto wawili walikufa ndani ya saa moja baada ya kupokea chanjo ya ukambi, huku mtoto wa tatu akifa siku tisa baada ya kusaidiwa kupumua katika Hospitali ya Al-Balak mjini Omdurman. (Sudan Tribune, Agosti 5, 2025)

Soma zaidi...

Hotuba Iliyotolewa na Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilaya ya Sudan Mbele ya Msikiti Mkongwe jijini Port Sudan mnamo Ijumaa tarehe 1/8/2025 M

Je, hili linaweza kuwaziwa kutoka kwenu?! Vipi mnaweza kula, kunywa na kulala na hali ndugu zenu mjini Gaza wanauawa, wanahamishwa na kuwekwa njaa na Mayahudi wanaokalia kimabavu eneo la Isra ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw)?! Dhambi liko juu ya shingo zetu sote ikiwa hatutawanusuru ndugu na dada zetu wa Gaza. Hatutaweza kuwanusuru isipokuwa majeshi ya Umma yasonge, kwani wao ni watoto wenu na ndugu zenu, na hakuna kitakachowaondoa Mayahudi isipokuwa dola ya Waislamu; Khilafah.

Soma zaidi...

Mahusiano ya Kigeni ni Jukumu la Dola Pekee, kwa kuwa Dola Pekee ndiyo iliyo na Haki ya Kuchunga Mambo ya Ummah Kivitendo

Baadhi ya vyombo vya habari viliripoti kuwa wajumbe kutoka Muungano wa Vyama na Mavuguvugu ya Sudan Mashariki, wakiongozwa na Sheiba Dirar na kuandamana na kundi la watu mashuhuri, walikutana na Rais wa Eritrea Isaias Afwerki mnamo Jumamosi, 2 Agosti 2025, afisini kwake huko Adi Halo, ambapo wajumbe hao walijadiliana naye hali ya sasa ya Sudan kwa jumla, kwa kuzingatia changamoto zinazoikabili Sudan Mashariki. Ujumbe huo pia ulisisitiza umuhimu wa uratibu na nchi jirani ili kusaidia utulivu wa nchi na kukabiliana na migogoro ya kisiasa na usalama.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Yaandaa Kisimamo Mbele ya Msikiti Mkongwe jijini Port Sudan cha Kuinusuru Gaza

Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan imeandaa kisimamo mbele ya Msikiti Mkongwe jijini Port Sudan leo, Ijumaa, 7 Safar 1447 H sawia na tarehe 1 Agosti 2025 M, baada ya swala ya Ijumaa. Wanachama wa Hizb waliinua mabango yenye alama ishara: “Angusheni viti vya utawala vinavyozuia kusonga kwa majeshi kuinusuru Gaza.”

Soma zaidi...

Serikali ya Muungano Msingi ni Hatua ya Juu katika Kuharakisha Mpango wa Amerika wa Kutenganisha Darfur

Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF), kupitia muungano wao unaoitwa Muungano Msingi wa Sudan "Ta'sis," ulitangaza mnamo Jumamosi, 26/7/2025, uteuzi wa Rais na Makamu wa Rais wa Baraza la Rais, na Waziri Mkuu, ambayo ina maanisha kuundwa kwa serikali sambamba katika mamlaka inayoendeshwa na jeshi kutoka mji wa Port Sudan, mashariki mwa nchi.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu