Gazeti la Al-Raya: Vichwa Vikuu vya Toleo 481
- Imepeperushwa katika Al-Rayah
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Salahudin aliyezaliwa 1137 nchini Iraq, aliibuka kuwa maarufu kipindi cha zahama wakati ardhi za Waislamu zilipokuwa zimesambaratika na kuwa chini ya mwavuli wa Makruseda wavamizi. Alipochukua uongozi Misri mnamo 1169, alianzisha misheni ya kuimarisha Dola ya Khilafah na kuunganisha maeneo kadhaa ya Kiarabu.
Idadi ya Waislamu wa Gaza waliokufa kutokana na mauaji, ukatili na mauaji ya halaiki yaliyofanywa na umbile la Kiyahudi linalokalia kwa mabavu huko Gaza katika muda wa siku 100 zilizopita tangu mafuriko ya Aqsa imezidi elfu 25.
Enyi Majeshi katika Nchi za Kiislamu, Inatosha!
Je, Munasubiri amri ya Watawala ndipo muinusuru Gaza Hashem?!
"Pakistan na IAEA zitaongeza ushirikiano katika matumizi ya amani ya sayansi na teknolojia ya nyuklia, hasa katika kilimo na matibabu, kwa manufaa ya nchi na majirani zake. Hayo yalikuwa matokeo ya safari ya siku mbili ya Mkurugenzi Mkuu Rafael Mariano Grossi nchini Pakistan wiki hii, ambapo alikutana na uongozi wa nchi hii - ikiwa ni pamoja na Mawaziri Wakuu na Mawaziri wa Mambo ya Nje - na kutembelea vituo vingi vya nyuklia nchini kote, ambapo baadhi yake alivizindua.”
Gazeti la Al-Thawra, lililotolewa jijini Sanaa mnamo Jumanne, Januari 29, 2024, lilikuwa na kichwa cha habari kutoka kwenye jukwaa "China huko Arabia: Meli za China zakwepa haki ya Yemen kwa sababu China haikutia madoa mikono yake kwa damu ya Wapalestina na haikushiriki katika uharibifu uliotokea kwa Yemen."
Baada ya mwaliko uliowasilishwa dhidi ya "Israel" kwa tuhma za mauaji ya halaiki kusomwa mbele ya Mahakama ya Kimataifa ya Haki jijini The Hague, Alhamisi, 11/01/2024, serikali ya Ujerumani ilitangaza kupitia afisi yake ya habari kwamba "mashtaka haya hayana mashiko na hayana msingi wowote.”
Haikutarajiwa kwamba tawala za Waarabu zingewanusuru pasi na shaka watu wa Gaza kwa majeshi yao yaliyowekwa kambini, na labda hilo ni bora zaidi. Huenda Mwenyezi Mungu anachukia kutaharaki kwao, basi akawazuia.
Uamuzi uliitaka Israel kuzuia na kuadhibu uchochezi wowote wa umma wa kufanya mauaji ya halaiki dhidi ya Wapalestina huko Gaza na kuhifadhi ushahidi kuhusiana na madai yoyote ya mauaji ya halaiki huko.
Mwanamke mmoja mdogo kutoka Sudan alishiriki katika mashindano yanayojulikana kama ‘Miss World’, ushiriki uliosherehekewa na Yaser Arman, kiongozi katika Baraza Kuu la Uhuru na Mabadiliko akitoa maoni yake kwa ujanja, licha ya athari kubwa ya utamaduni wa uokoaji dhidi ya ubunifu, urembo, na wanawake, Tibah Diab, mshiriki kijana, alionyesha ujasiri na ufahamu, akisubutu kushiriki katika mashindano ya urembo na kujaribu kuakisi sehemu ya turathi, utamaduni, na utambulisho wetu.