Gazeti la Al-Raya: Vichwa Vikuu vya Toleo 306
- Imepeperushwa katika Al-Rayah
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Vichwa Vikuu vya Toleo 306
Vichwa Vikuu vya Toleo 306
Mnamo Septemba 16, 2020, Mahakama ya Kijeshi ya Wilaya ya Kusini ya Shirikisho la Urusi huko Rostov-on-Don ilitangaza uamuzi dhidi ya Waislamu 8 kutoka Crimea katika kile kinachoitwa "kesi ya pili ya Bakhchisaray ya Hizb ut Tahrir".
Vazi la mwanamke wa Kiislamu, ima Khimar, jilbab au Niqab kamwe huwa haliko mbali na vyombo vya habari au kurunzi ya kisiasa ndani ya dola za kisekula.
Naibu Waziri wa Kigeni wa Amerika Stephen Biegun amedokeza kuwa ushirikiano usio rasmi kati ya Amerika, Australia, Japan, na India unaweza kuwa mwanzo wa mtindo wa muungano wa NATO katika eneo la Indo-Pasifiki.
Hizb ut Tahrir / Wilayah Bangladesh leo (Ijumaa, 25/09/2020) baada ya swala ya Ijumaa iliandaa maandamano katika misikiti tofauti tofauti jijini Dhaka na Chittagong dhidi ya makubaliano ya khiyana ya Imarati na Bahrain pamoja na umbile la Kiyahudi.
Sisi tunaishi katika mazingira ya kupanuliwa kwa mapinduzi ya Januari ambayo hayakuisha, kama Magharibi na wanaume wake miongoni mwa wanajeshi waliochukua madaraka baada ya mapinduzi walivyodhani,
Jana (26 Septemba 2020) jimbo la Borneo la Sabah lilionekana likienda katika upigaji kura. Matokeo rasmi ya uchaguzi wa 16 wa jimbo la Sabah yanashuhudia muungano wa Gabungan Rakyat Sabah (GRS) ukishinda kwa idadi kubwa ya viti 38 dhidi ya viti vya Warisan Plus' 32 huku wagombeaji huru wakibeba viti vitatu vilivyobaki.
Wakati ambapo India imeweka marufuku ya ghafla kwa usafirishaji wake wa kitunguu kwenda Bangladesh, watawala wetu wa vibaraka wamekuja kuokoa sura ya adui huyu mshirikina kwa kujifanya kama mdomo wake.
Recep Tayyip Erdoğan, Rais wa Uturuki na Mwenyekiti wa Chama cha AK, alihutubia washiriki katika Mkutano wa 140 wa Wakuu wa Mikoa wa Chama cha AK uliofanyika kwa njia ya video.
Tumekuwa tukishuhudia janga kubwa la maambukizi tangu mwanzoni mwa mwaka huu ambalo liliwafanya wengi kuchanganyikiwa, au angalau kuwa na wasiwasi, katika kuelewa baadhi ya fahamu za Kiislamu zilizo wazi bila ya kuwa na ikhtilafu.