Gazeti la Al-Raya: Vichwa Vikuu vya Toleo 457
- Imepeperushwa katika Al-Rayah
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Wagombea kadhaa wa ‘Miss Universe’ wa Indonesia wamesajili malalamishi kwa polisi wakiwatuhumu waandaaji kwa unyanyasaji wa kijinsia.
Wizara ya Kigeni imelalamika, "Tunazingatia kumbukumbu maalum ya Pakistan katika 'Taarifa ya Pamoja kutoka Marekani na India', iliyotolewa mnamo tarehe 22 Juni 2023,
Maoni ya Habari ya Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Pakistan.
Mnamo Julai 21, wanachama wa kikundi cha "Wazalendo wa Denmark" walichoma nakala ya Quran ya Noble mbele ya ubalozi wa Iraq jijini Copenhagen. Walidai kwamba kitendo hiki cha kufedhehesha kilikuwa ni majibu ya kuchomwa kwa ubalozi wa Sweden nchini Iraq.
Bei ya umeme imeongezeka kwa Rupia 18 kwa kila kipimo tangu Julai mwaka jana. Leo umeme, pamoja na ushuru, ni Rupia 50 kwa kila kipimo. Bei za petroli zinagusa Rupia 300 kwa lita. Kiwango cha mfumko wa bei kiko kiwango cha juu katika historia ya Pakistan.
Mnamo tarehe 18 Agosti 2023, Waziri Mkuu wa Muda, Anwaarul Haq Kakar, alitoa kemeo kali dhidi ya watu waliohusika katika kukandamiza na kuchoma makanisa huko Jaranwala mapema wiki hii. Hii ni huku maafisa wakuu wakiwa na mashaka juu ya ukweli wa madai ya kufuru ambayo yalisababisha vurugu hizo.
Wakati wa uwajibikaji wa Serikali kwa Kongamano la Taifa, Waziri wa Sheria wa Imirati ya Kiislamu ya Afghanistan alisema kuwa uasisiwaji wa vyama vya kisiasa ni 'dhidi ya Sharia na mapenzi ya watu' na kwamba uendeshwaji wao ‘umekatazwa katakata’ nchini.
Mnamo tarehe 11 Agosti 2023, BBC iliripoti kwamba Waislamu 23 wa Rohingya walikufa na 30 hawajulikani waliko baada ya mashua iliyobeba wahamiaji wanaotoroka serikali kandamizi ya Myanmar kuzama. Miili ya Warohingya 23 wanaokimbia kwa ajili ya maisha yao kutoka Jimbo la Rakhine wamepatikana baada ya mashua yao kuzama.