Ijumaa, 03 Jumada al-awwal 1447 | 2025/10/24
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Makubaliano ya Aibu ya Kuhalalisha Usalama na Mayahudi na Miradi ya Ugawaji ni Hatari Kubwa Inayolenga Kuvunja Utashi wa Kiota na Ushindi Uliopata

Katika taarifa ambazo, kusema kwa uchache, ni hatari, zilizotolewa na mkuu wa awamu ya mpito, Ahmed al-Sharaa, vipengee vya hali ya sasa ya Syria vilifichuliwa. Alionyesha kwamba “Syria inajua jinsi ya kupigana, lakini haitaki tena vita,” na kwamba “haina chaguo ila kufikia makubaliano ya usalama na Israel,” wakati “kujitolea kwa Israel kwa makubaliano haya ni suala tofauti.” Pia alieleza kuwa matukio ya Sweida yalikuwa tu “mtego uliotayarishwa makhsusi kuzuia makubaliano ya awali juu ya utaratibu wa usalama,” na kwamba “baadhi ya mirengo ndani ya SDF na PKK ilivuruga makubaliano ya Machi na kupunguza kasi ya mchakato huo.” Amesisitiza kuwa “hali ya kaskazini mashariki mwa Syria inatishia usalama wa kitaifa wa Uturuki pamoja na Iraq,” na akadokeza kuwa “ikiwa uwiano hautafikiwa ifikapo Disemba, Uturuki inaweza kuchukua hatua za kijeshi.”

Soma zaidi...

Makongamano Yenye Malengo ya Kufuta Kadhia ya Ardhi Iliyobarikiwa Yanafanyika Wakati Damu ya Watu wake Ikimalizwa

Milipuko ya mabomu inateketeza miili ya watoto mjini Gaza, njaa inatafuna mabaki yao, mizinga inasaga saga uhai na nyumba za watu walio na msimamo thabiti, na ndege zinanyesheza lava zao kwenye hospitali na hema za waliohamishwa. Kutokana na hali ya uhalifu huu, kongamano lililokongamana jana usiku, 22 Septemba 2025, jijini New York, lililoitishwa na Ufaransa na Saudi Arabia, lilitaka kutambuliwa kwa “Dola ya Palestina”.

Soma zaidi...

Maradhi ya Mkurupuko Yawaangamiza Watu kwa Kukosekana kwa Dola ya Ustawi

Maradhi matatu ya kimazingira—kipindupindu, homa ya dengue, na malaria—yanawaangamiza watu katika majimbo ya Khartoum, Al-Jazirah, na Darfur, katikati ya uzembe wa kutisha na aibu ya kukosekana kwa serikali inayojiita “Serikali ya Matumaini”! Kuna matumaini aina gani wakati watu wanaishi katika mazingira yasiyostahili hata kwa wanyama—mazingira yanayotawaliwa na waenezaji magonjwa, ikiwemo mbu wa malaria, mbu wa dengue, na nzi?

Soma zaidi...

Mwaliko wa Kuhudhuria Kikao cha Kisiasa

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan inafuraha kuwaalika wanahabari, wanasiasa, na wale wote wanaopenda masuala ya umma, kuhudhuria na kushiriki katika kikao kipya cha Kisiasa, ambapo Ustadh Ya‘qub Ibrahim, mwanachama wa Hizb ut Tahrir/Wilayah Sudan, atakuwa mgeni, chini ya kichwa: Ulaya na Ushawishi Wake kwa Matukio nchini Sudan.

Soma zaidi...

Majibu ya Vyombo vya Habari kwa Yaliyomo kwenye Makala ya Mwandishi Sabah Muhammad Al-Hassan

Hizb ut Tahrir ni chama cha kisiasa ambacho mfumo wake ni Uislamu, kinataka kurudisha mfumo kamili wa maisha ya Kiislamu kwa kusimamisha Khilafah Rashida ya pili kwa njia ya Utume kwa njia ya kisiasa, na hakitekelezi vitendo vyovyote vya kisilaha si kwa kumwogopa mtu yeyote, bali ni kujifunga na njia ya Mtume (saw) katika kusimamisha dola ya kwanza ya Kiislamu.

Soma zaidi...

Kujibu Matamshi ya Mjumbe wa Marekani Tom Barrack

Kwa mara nyingine tena utawala wa Marekani unaonyesha sura yake halisi kupitia taarifa za mjumbe wake Tom Barrack, katika mahojiano yake yaliyotangazwa na Sky News na mtangazaji mkuu wa IMI International Hadley Gamble, ambaye alijiruhusu kuingilia waziwazi katika masuala ya Lebanon na kubainisha sifa za dori za taasisi ya Jeshi.

Soma zaidi...

“Khiyana ya ‘Ruwaibidha’ (watawala wasiostahiki) na kuidhinishwa kwa mpango wa Trump kwa gharama ya damu ya mashahidi wa Palestina”

Baada ya hotuba ya rais wa Marekani kwenye Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa – ambayo asili ilikusudiwa kuhakiki kadhia ya Palestina – na katika wakati ambapo, kwa msimamo mmoja kutoka zaidi ya dola 150 kati ya dola 193 za Umoja wa Mataifa, “dola ya Palestina” tayari imetambuliwa, Rais Trump aliikejeli jumuiya ya kimataifa kwa kuyaita maneno ya “viongozi” kama “domo tupu.” Pia alikejeli makubaliano ya kimazingira, akaiichukulia mikataba ya uhamiaji kuwa ya kudharauliwa, na akakashifu mchakato wa Ulaya wa kuitambua Palestina kwa kuiita udhaifu. Hotuba yake ilionekana kama dua ya mwisho ya mazishi (fatiha) iliyosomwa juu ya makubaliano ya kimataifa, madai ya mtazamo wa upande mmoja wa Amerika katika masuala ya kimataifa, na tangazo la kulazimisha rai yake juu ya Mashariki ya Kati – haswa suala la Palestina.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu