Jumapili, 26 Safar 1448 | 2026/08/09
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Hizb ut Tahrir / Wilayah Tunisia: Matembezi ya Takbira “Ni Dola ya Khilafah Pekee ndiyo Itakayomaliza Kiburi cha Amerika.”

Baada ya Swala ya Ijumaa ya mwisho ya Ramadhan Tukufu 1447 H, matembezi ya Takbira (Allahu Akbar) yaliyoandaliwa na Hizb ut-Tahrir / Wikayah ya Tunisia yalianza kutoka Msikiti wa Al-Fath katika mji mkuu, Tunis. Umati mkubwa wa Watunisia ulishiriki, wakipiga Takbira na Tahlil, na matembezi hayo yaliendelea kupitia barabara kuu za mji mkuu kuelekea Barabara ya Al-Thawra. Mabango yaliinuliwa, bango kuu likiwa limeandikwa, “Ni Dola ya Khilafah Pekee ndiyo Itakayomaliza Kiburi cha Amerika.”

Soma zaidi...

Nusra (Msaada) Inatafutwa Kutoka Kwa Nani?!

Kutafuta Nusra (kuomba msaada) kunapaswa kufanywa kwa yule anayekubali Uislamu na kuuingia, na ambaye ni miongoni mwa watu wa nguvu na ulinzi, ili aweze kuinusuru dini na kusimamisha utawala kwa yale aliyoyateremsha Mwenyezi Mungu. Masharti haya mawili lazima yatimie kwa mnayeitafuta Nusra kwake. Ikiwa hatakubali Uislamu na kuuingia, au si katika watu wa nguvu na ulinzi wenye uwezo wa kuleta mabadiliko, peke yake au pamoja na wengine, basi hatakuwa miongoni mwa watu wa Nusra

Soma zaidi...

Kati ya Magereza ya Wahubiri na Bandari za Silaha…Je, ni Upi Msingi wa Hukumu wa Utawala Huu?

Huku magereza na vituo vya uzuizini vikiwa wazi kwa wabebaji wa Dawah wanaotaka utabikishwaji wa Uislamu, na huku wakiteswa kwa ajili ya riziki zao, wakinyamazishwa, na fikra zao zikikandamizwa—si kwa uhalifu wowote walioufanya, wala uchokozi wowote walioufanya, bali kwa sababu tu wanasema kwamba Uislamu lazima utabikishwe maishani, na kwamba Ummah lazima utawaliwe na sheria ya Mola wake Mlezi—wakati huo huo, bandari zinafunguliwa, barabara zinarahisishwa, na huduma zote zinatolewa kwa kila kitu kinachowatumikia maadui wa Ummah na kuimarisha nguvu zao!

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu