Ijumaa, 03 Jumada al-awwal 1447 | 2025/10/24
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Operesheni ya Shujaa Aliyeuawa Shahidi Abdul Muttalib Al-Qaisi Inathibitisha Azma ya Ummah Kupambana na Mayahudi hadi Watakapotokomezwa, Licha ya Watawala wa Kiarabu Kushindwa

Jana, 10 Septemba 2025, kamanda wa Kamandi Kuu ya jeshi la umbile la Kiyahudi alitangaza kuundwa kwa kitengo kipya cha kijeshi, kinachoitwa “Kitengo cha Gilead,” katika Bonde la Jordan, kitakacho kaa kwenye Bonde la Jordan. Kitengo hichi cha kikanda kina jukumu la kulinda mipaka ya mashariki ya Mayahudi katika Bonde la Jordan na Bahari ya Dead. Aliashiria kuwa kuanzishwa kwa kitengo hicho kunajiri ndani ya muundo wa kile alichoelezea kama “masomo ya kujifunza kutokana na kushindwa kugumu kwa Israel mnamo Oktoba 7, 2023.” Uundaji huu mpya unakuja baada ya vitisho vya viongozi wa umbile la Kiyahudi kupanuka hadi nchini Jordan na kwengineko chini ya mwavuli wa mradi wa “Israel Kubwa”, uliotangazwa na Netanyahu, uliobarikiwa na Trump, na kutangazwa wazi na Smotrich, Waziri wa Fedha wa umbile la Kiyahudi.

Soma zaidi...

Matukio ya Kisiasa ya Hivi Majuzi nchini Yemen Yanaonyesha Nini?

Mnamo Alhamisi, 28 Agosti, Waziri Mkuu wa Wizara ya Mabadiliko na Ujenzi, Ahmed Ghaleb Al-Rahwi, aliuawa, pamoja na mawaziri wengine tisa: Waziri wa Sheria na Haki za Binadamu Mujahid Ahmed Abdullah Ali; Waziri wa Uchumi, Viwanda na Uwekezaji Moeen Hashim Ahmed Al-Mahaqri; Waziri wa Kilimo, Uvuvi na Rasilimali za Maji Radwan Ali Ali Al-Rubai; Waziri wa Mambo ya Nje na Wageni Jamal Ahmed Ali Amer; Waziri wa Umeme, Nishati na Maji Ali Seif Mohammed Hassan; Waziri wa Utamaduni na Utalii Ali Qasim Hussein Al-Yafei; Waziri wa Masuala ya Jamii na Leba Samir Mohammed Ahmed Bajaala; Waziri wa Habari Hashim Ahmed Abdul Rahman Sharaf Al-Din; na Waziri wa Vijana na Michezo Mohammed Ali Ahmed Al-Mawlid. Mawaziri wengine kadhaa bado wako katika hali mbaya na ya wastani, akiwemo Jalal Al-Ruwaishan, Naibu Waziri Mkuu wa Masuala ya Ulinzi na Usalama. Umbile la Kiyahudi limeeleza kuwa lilifanya shambulizi hilo, likiwalenga Waziri wa Ulinzi Mohammed Al-Atifi na Mkuu wa Majeshi Mohammed Abdul Karim Al-Ghamari.

Soma zaidi...

Kukabiliana na Mayahudi ni jambo la Aqidah. Kujitayarisha kwa ajili yake Ni Faradhi ya Shariah, na Kuliepuka ni Maangamivu

Baadhi ya wanasiasa wa Syria hivi majuzi wamekuwa wakiendeleza wazo kwamba “hatutauza udanganyifu kwa watu wetu, na kwamba lazima tuchukue hatua ya kweli ili kujenga upya serikali.” Hili linafanywa kwa kisingizio kwamba “tunafahamu uwezo wetu wa kweli, na lugha ya vitisho haitakuwa na manufaa yoyote katika kukabiliana na uvamizi wa Kizayuni,” na kwamba “mazungumzo nao yanaendelea ili kuregea kwenye makubaliano ya 1974!”

Soma zaidi...

Maandamano ya Umwagaji damu nchini Indonesia na Chanzo Chake

Tangu tarehe 25 Agosti, 2025, Indonesia imekuwa ikishuhudia wimbi la maandamano makubwa yaliyorekodiwa katika maeneo 107 katika mikoa 32. Huku baadhi ya maandamano yakiendelea kuwa ya amani, mengi yalizidi kuwa ghasia zilizohusisha uharibifu na uchomaji moto. Maeneo kadhaa yalishuhudia machafuko makubwa zaidi, ikiwemo mji mkuu Jakarta, Java ya Kati, Java Mashariki, Java Magharibi, Yogyakarta, Sumatra Kaskazini, Nusa Tenggara Magharibi, Sulawesi Kusini, na Kalimantan Magharibi. Vituo vya umma, afisi za serikali, na hata mali za usalama wa taifa zilipata uharibifu mkubwa. Jijini Jakarta, kwa mfano, vituo 22 vya mabasi ya TransJakarta na vituo vya treni ya chini ya ardhi vya MRT viliharibiwa, huku hasara ikikadiriwa kuwa karibu rupiah bilioni 50.4 za Indonesia.

Soma zaidi...

Mradi wa Reli wa China–Indonesia: Mkakati wa China Kuidhibiti Indonesia

Indonesia inafikiria kujadili upya deni la mradi wa reli ya mwendo kasi wa Jakarta–Bandung, unaojulikana kama Whoosh, kutokana na mzigo mzito wa kifedha unaouweka kwa mwendeshaji wa reli ya serikali Kereta Api Indonesia (KAI). Waziri wa Biashara Zinazomilikiwa na Serikali Erick Thohir alisema mpango huo utaruhusu KAI kusimamia treni huku serikali ikisimamia miundombinu. Mradi huo wenye thamani ya dolari bilioni 7.3 ulifadhiliwa hasa kupitia mikopo kutoka Benki ya Maendeleo ya China, awali kwa riba ya asilimia 2. Hata hivyo, kukatizwa na maambukizi na masuala ya ardhi yalisukuma gharama zaidi, na kuhitaji ufadhili wa ziada kwa riba ya asilimia 3.4.

Soma zaidi...

Hakuna Wokovu kwa Watu wetu nchini Sudan Wala Amani au Usalama isipokuwa chini ya Mfumo wa Uislamu

Katika yote historia, wingi wa makabila nchini Sudan kamwe haukuwa sababu ya mizozo na vita. Bali, kilichosababisha haya ni mapambano makali ya kisiasa na kijeshi baina ya dola za kikoloni na vibaraka wao, ambayo yaliharibu mazao na vizazi, hasa baada ya wao kuigawanya nchi na kupanda mbegu za fitina na mapigano ya kikabila na kimapendeleo, sawa kabisa na yale yanayotokea leo na kwa usahihi kabisa kama ilivyotokea katika siku za mwanzo za Ujahiliya.

Soma zaidi...

Enyi Waislamu: Waokoeni watu wa Gaza Kabla Hawajaangamizwa Kabisa na Jihadharini Isije Akakushukieni Ghadhabu na Adhabu ya Mwenyezi Mungu

Umbile la Kiyahudi linaendelea na vita vyake vya mauaji ya halaiki katika Ukanda wa Gaza, likilenga maeneo mbalimbali ya Ukanda huo kwa mashambulizi ya anga na mizinga mikubwa, na kusababisha makumi ya vifo na majeruhi kila siku. Kwa wiki kadhaa, limezidisha mashambulizi yake katika mji wa Gaza, eneo lenye wakaazi wengi na watu waliokimbia makaazi yao kutoka sehemu ya kaskazini ya Ukanda huo, kwa ajili ya maandalizi ya kukaliwa tena kimabavu. Linalenga shule na makaazi, linatekeleza operesheni kubwa za ubomoaji inayolenga nyumba zote za makaazi, na kuvunja magorofa ya makaazi, likiambatanisha na maonyo kuhamia sehemu ya kusini ya Ukanda huo.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Yafanya Kisimamo katika eneo la Nile Mashariki

Leo, Jumatano, tarehe 25 Rabi’ al-Awwal 1447 H sawia na 17 Septemba 2025 M, Mashababu wa Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan katika eneo la Nile Mashariki walifanya kisimamo baada ya Swala ya Adhuhuri katika Msikiti Mkuu wa Souq Sitta Al-Wahda. Ndani yake, mabango yaliinuliwa kuwataka Waislamu kusimama kidete kuzuia njama ya kuichana Sudan kwa kuitenganisha Darfur.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu