Jumapili, 27 Safar 1446 | 2024/09/01
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Mauaji Dhidi ya Watoto wa Yemen yanaendelea, ilhali Wauaji wanacheza dori ya Waweka Amani

Mnamo 26 Aprili, Umoja wa Mataifa ulipeperusha ripoti kwamba idadi ya waliofariki ndani ya Yemen kutokana na mzozo unaoendelea unatarajiwa kupita 230,000 mwishoni mwa 2019. Utafiti kwa kichwa “Tathmini ya Athari ya Vita Juu ya Maendeleo ndani ya Yemen”,  pia iliripoti kuwa Wayemen 131,000 watakuwa wamefariki kutokana na athari mbaya za vita baina 2015 na 2019 mfano kutokana na njaa, maradhi na kukosekana kwa kliniki za afya. Kwa mujibu wa UN mwishoni mwa mwaka, mapigano yatakuwa yamechukuwa maisha ya watu 102,000.

Soma zaidi...

Ongezeko la Takwimu Sio Jipya Bali Halina Budi kwa Zabuni za Kifedha Kabla ya Kongamano la Wafadhili la Brussels kwa Ajili ya Syria

Vita katili nchi Syria dhidi ya raia vimeingia mwaka wake wa tisa mnamo Machi 15. Zaidi ya watu nusu milioni wamekufa, kwa mujibu wa ripoti za kimataifa, na shirika la Uangalizi wa Haki za Kibinadamu la Syria limenakili vifo 19800 vya watoto tangu 2011. Inakisiwa watoto milioni 8.6 wanahitaji msaada wa dharura, na sasa zaidi ya watoto milioni 6 hawana makao au wanaishi kama wakimbizi, na baadhi ya milioni 2.5 yao hawendi shule. Zaidi ya watoto milioni 3 wako katika hatari ya mabomu ya ardhini, huku takriban asilimia 40 ya wale waliouwawa na mabomu ya ardhini wakiwa ni watoto. 

Soma zaidi...

Janga la Watoto Wachanga Linafichua Hali Mbaya ya Sekta ya Afya Nchini Tunisia na Kudhihirisha Kufeli kwa Serikali Hiyo Katika Kuchunga na Kulinda Watu Wake!

Janga chungu liliitingisha rai jumla nchini Tunisia wiki jana! Watoto wachanga kumi na tano walikufa katika Hospitali ya Wassila Bourguiba kwa mujibu wa takwimu rasmi na idadi inazidi kuongezeka. Mnamo Ijumaa, Machi 15, msemaji wa Afisi ya Mkuu wa Mashtaka ya Ummah alisema “idadi ya watoto wachanga waliokufa katika Hospitali ya Wassila Bourguiba ilikuwa ni 15.” Janga hilo lilifuatiwa na jengine baya zaidi, kila mojawapo likiifichua dola hiyo kuwa haiangalii watu wake!

Soma zaidi...

Hakutakuwepo na Hadhi, Usalama na Ustawi kwa Wanawake Waislamu Bila ya Kusimamisha Khilafah Rashidah

Rajab hii inatukumbusha tukio baya mno, miaka 98 iliyopita pale Ummah wa Waislamu ulipopoteza dola yake adhimu, uongozi wake wa Kiislamu, mlinzi na ngao yake –Khilafah. Tokea wakati huo, wanawake Waislamu na familia zao wamejipata katika maangamizi ya mauaji, njaa, uvunjwaji, adhabu, kukosewa heshimu, umasikini wa kupindukia, upweke, ukandamizaji na madhila yasiyovumilika. Tumetoka kutoka kuwa chini ya dola iliyokuwa ina tawaliwa na viongozi wachamungu wakiwahudumia Ummah kwa huruma na kujali mahitaji yao kama alivyoamrisha Mwenyezi Mungu (swt)… kiasi kwamba Ummah upo chini ya viongozi wasiojali lolote kuwahusu, wanaoiba mali zetu kwa kujitajirisha, na kuwaadhibu Waislamu wanaoshikamana kikamilifu na Dini yao. Kutoka kuwa dola kubwa yenye kubeba Jihad kueneza Uislamu ili ikomboe miji, na iliyowafanya maadui zake kutetemeka kwa uoga kila wanapofikiria kumdhuru mwanamke Muislamu…tumekuwa wahanga wa mauaji na uvamizi.

Soma zaidi...

Kitengo cha Wanawake Katika Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir Kimezindua Kurasa Mpya za Facebook: “Familia: Changamoto na Suluhisho la Kiislamu”

Kufuatia mafanikio ya kampeni yetu ya kiulimwengu na kongamano la wanawake la kimataifa mnamo Oktoba 2018, “Familia: Changamoto na Suluhisho la Kiislamu”, Kitengo cha Wanawake katika Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir kina furaha kutangaza uzinduzi wa kurasa zetu mpya za Facebook zinazojitolea kuangazia kadhia zinazo husiana na mgogoro wa kiulimwengu unao athiri “Kiungo cha Familia”. Kurasa hizi mpya, ambazo zitakuwa kwa Kiarabu, Kiingereza, Kituruki na Kiindonesia, zitawasilisha tena shehena ya fasihi zilizo chapishwa katika kampeni na kongamano pamoja na kutafuta mada za ziada kuhusiana na uhalisia, sababu na masuluhisho ya ukosefu wa utulivu na mfarakano unao athiri muundo wa familia katika jamii kote ulimwenguni.

Soma zaidi...

Wanawake wa Palestina Wangali Wanamsubiri Al-Mu’tassim ili Kuitikia Kilio Chao!!

Vyombo vya habari vilichapisha picha na video za majeshi vamizi ya umbile la Kiyahudi yakifurusha katika nyumba moja ya familia ya Jerusalem eneo la Aqaba Al-Khalidiya katika mji wa kale wa Jerusalem kwa kutumia nguvu za kijeshi. Vyombo hivyo vya habari vilionyesha nduru na malalamishi ya wanawake waliolalamikia shambulizi la polisi wa Kiyahudi katika nyumba hiyo, wakimpiga na kumkamata mwenye nyumba hiyo, na kuwaacha wao bila ya ulinzi na makao baada ya nyumba yao kuchukuliwa.

Soma zaidi...

Mwaelekea Wapi, Enyi Munao Simamia Muongozo wa Utoaji Fatwa wa Kiulimwengu?!!

Baadhi ya wanaume wa Al-Azhar wanaendelea kutembea juu ya barabara ya kuushambulia Uislamu na Hukmu zake pasi na maono wala hofu kwa Mwenyezi Mungu (swt). Wanaendelea kuifanya Al-Azhar Al-Sharif – ambayo ilikuwa ndio ngome dhidi ya njama za maadui wa Uislamu – jukwaa ambalo wanavishambulia vipengee vya Uislamu na Hukmu zake zinazo husiana na wanawake. Meza ya Utoaji Fatwa wa Kiulimwengu ya Jumba la Fatwa la Misri (Dar al-Ifta) zilisema kuwa, “fatwa juu ya kadhia ya ndoa kwa watoto wadogo zimeifunga ndoa kwa watoto wadogo katika mahusiano ya kijinsia pekee, na kwamba Hizb ut Tahrir imeifunga ndoa katika mahusiano ya kijinsia pekee, ikiondoa upande wa kisaikolojia, kiafya, kiakili na mambo ya kimwili, na kuweka mbali kiwango cha uvumilivu na jukumu ambalo mkataba wa ndoa unalazimisha juu ya pande zote mbili …” Hili, kwa kuanzia, linagongana na yale ambayo Quran Tukufu imeeleza kuhusu fahamu ya ndoa kama utulivu na huruma.

Soma zaidi...

Jinsi Siasa Inavyo Fanana na Zamani … Matukio Yanaendelea Kama Wanavyo Endelea Watazamaji!

Wanajeshi madhalimu wa umbile la Kiyahudi walimuua msichana kutoka Palestina kwa kummiminia risasi katika kituo cha upekuzi cha al-Za’im, mashariki mwa ardhi iliyo kaliwa Al-Quds (Jerusalem). Shahidi huyo ni mwanafunzi wa shule ya upili aliyekuwa amebeba mkoba wake wa shule wakati wa kuuwawa kwake; aliuwawa kutokana na madai ya kujaribu kutekeleza oparesheni ya kudunga kisu. Majeshi hayo vamizi yalizuia wahudumu wa ambulensi kutomfikia ili kumpa tiba. Aliachwa kuvuja damu hadi kufa.   

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu