Jumamosi, 06 Dhu al-Hijjah 1447 | 2026/05/23
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Ni Rasmi: Mamlaka nchini Tunisia Zinasaidia Amerika na Umbile la Kiyahudi katika Mauaji ya Halaiki dhidi ya Watu Wetu huko Gaza na Palestina yote

Mji wa Vicenza wa Italia ulishuhudia hafla ya kusainiwa kwa itifaki ya mwisho ya taratibu za kupanga mazoezi ya kijeshi ya Simba wa Afrika 2025 nchini Tunisia. Makubaliano hayo yalitiwa saini kati ya Kanali Mwandamizi wa Tunisia Mguidich Mejid na Kanali wa Marekani Drew Conover, Mkurugenzi wa Mafunzo wa Jopo Kazi la Jeshi la Marekani la Kusini mwa Ulaya.

Soma zaidi...

Uhadaifu wa Utaifa

Baada ya wakoloni kuugawanya ulimwengu wa Kiislamu, walifanya kazi kuelekea kubadilisha mfumo wake wa utawala. Mifumo ya bunge ilianzishwa na maafisa wa kikoloni wangejihusisha na raia wao iwapo tu wangekubali kujipanga katika muundo wa vyama vya kidemokrasia. Walioletwa madarakani na wakoloni ni wale waliokubali sheria na kanuni zao. Kuibuka kwa dola za kitaifa katika ulimwengu wa Kiislamu kwa hiyo kunahusishwa kwa namna isiyoweza kutenganishwa na historia ya ukoloni na kulazimishwa na dola za Ulaya zilizotaka kuona ulimwengu wa Kiislamu ukigawanyika.

Soma zaidi...

Ni ipi Hatua Inayofuata?

Tangu kuvunjwa kwa Khilafah, tunaona kwamba siku baada ya siku Ummah wetu unadhalilika zaidi na zaidi. Kuanzia vita dhidi ya nyumba ya familia, hadi mabomu yanayoangushwa, na hadi watawala wanaotuma vikosi vyetu vya majeshi kwenye matukio kama vile Phoenix Express. Haya ndiyo ambayo sisi kama Ummah tunayaona na hatuwezi kufahamu jinsi tulivyofika mbali hivi sana na pale tulipowahi kuwa mahali pa heshima na adhama. Tulikuwa Ummah ambao ulikuwa juu ya dunia, ambao wanadamu walitamani kuwa sehemu yake kuanzia kwa mfumo wetu wa elimu hadi mfumo wetu halisi wa mahakama. Tulikuwa na haki na uadilifu tofauti na mfumo mwingine wowote duniani, unaoleta amani na utulivu kwa wanadamu wote.

Soma zaidi...

Kuchochea Migogoro ya Kimadhehebu ni Mtazamo Uliofichuliwa wa Mayahudi katika Kushinikiza Mauaji na Suala la Kuhama Makao!

Mauaji nchini Lebanon yanaendelea tangu Mayahudi walipoanza uvamizi wao wa kikatili na wa kinyama dhidi yake na watu wake kwa jumla, na dhidi ya watu wa kusini haswa, hadi idadi ya wahasiriwa nchini Lebanon ikazidi 3200, na idadi ya waliojeruhiwa ikafikia 14,000, na karibu watu milioni 1.2 wamelazimika kuyahama makaazi yao, katika sera inayotekelezwa na adui huyu mnyakuzi nchini Lebanon, na alifanya hivyo hapo awali na anaendelea kufanya vitendo hivi katika Ukanda wa Gaza unaoheshimika kwa zaidi ya mwaka mmoja!

Soma zaidi...

Waislamu nchini Denmark Kamwe Hawatajioanisha na Maadili ya Serikali ya Mauaji ya Halaiki

Katika mahojiano ya kina na ya jukwaani na Jyllands-Posten mnamo Novemba 18, 2024, Waziri Mkuu Mette Frederiksen anafanya juhudi kubwa kutoa taswira kali ya idadi ya Waislamu wa nchi hiyo. Anatuhumu Quran kuwashajiisha Waislamu kufanya uhalifu, kuwapiga watoto wao, na kujihusisha na tabia ambayo inaleta ukosefu wa usalama katika maeneo ya umma. Hatari inayodaiwa kuletwa na Waislamu wanaoishi Denmark inalinganishwa na tishio la “Urusi na Putin.”

Soma zaidi...

Bila Mfumo wa Elimu ya Kiislamu, Haramu inakuwa ni Sharti la Kusoma

Mnamo tarehe 16 Novemba, gazeti la Times la India liliripoti kwamba Chuo Kikuu cha Uttarakhand Sanskrit huko Haridwar kimeanzisha hatua za kutekeleza uamuzi wa Mahakama ya Upeo juu ya mavazi ya wanafunzi ndani ya chuo kikuu na madarasani, Makamu wa Chansela wa Chuo Kikuu Dinesh Chandra Shastri aliiambia TOI mnamo Alhamisi. Hatua hiyo imekuja baada ya malalamiko kuwa “wanafunzi kadhaa wa Kiislamu wa kike wanaendelea kuvaa burka au hijabu wakiwa chuo hicho kikuu.”

Soma zaidi...

Baada ya Mwaka Mmoja wa Mauaji ya Halaiki (na Miaka 76 ya Ukaliaji Kimabavu), Watawala wa Ruwaibidha Wakusanyika Tena Kuendeleza Kejeli na Usaliti wao

Ni mwaka mmoja kamili baada ya watawala wa Waarabu na Waislamu kukusanyika kujadili kadhia ya Palestina kufuatia mkasa wa Oktoba 7, wanakutana tena mahali pale pale, pamoja na mtu yule yule, wakishughulikia tatizo lile lile, na hatimaye kutoa maazimio yale yale! Zaidi ya viongozi 50 wa dola za Waislamu walihudhuria Mkutano wa Waarabu na Waislamu mnamo tarehe 11/11/2024, akiwemo Waziri Mkuu wa Malaysia. Kwa kutabiriwa, mapendekezo yaliyochakaa yaliwasilishwa, na Mkutano huo ulihitimishwa kwa maazimio yaliyochakaa vilevile. Kikubwa kinachotolewa na watawala hao ni kulaani mauaji ya halaiki ya Gaza na ‘Israel’ na kuomba Umoja wa Mataifa (UN) - shirika lile lile lililohusika na kuzaliwa kwa umbile halifu la Kiyahudi.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Tunisia: Matembezi ya Ukombozi “Gaza Inamwachia Mwenyezi Mungu Kiwango cha Usaliti jijini Riyadh na inataka Msaada kwa Umma na Majeshi yake!”

Matembezi ya hamsini na nane ya kunusuru Palestina na mateka Al-Aqsa, ambayo yaliandaliwa na Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Tunisia, yalifanyika katika mji mkuu, Tunis, baada ya swala ya Ijumaa, chini ya kichwa “Gaza Inamwachia Mwenyezi Mungu Kiwango cha Usaliti jijini Riyadh na inataka Msaada kwa Umma na Majeshi yake!”

Soma zaidi...

Watawala wa Iran ni Uhalisia tu wa Sauti na Maonyesho ya Fataki Hawana Uhusiano Wowote na Ushindi au Ukombozi

Kamanda wa Walinzi wa Mapinduzi ya Iran, Meja Jenerali Hossein Salami, alithibitisha katika ufunguzi wa mazoezi ya mapambano ya usalama ya “Nasrallah” kwamba “umbile la Kizayuni linakosea ikiwa linadhani kuwa Hizbullah itatoka nje ya uwanja kwa kuwauwa viongozi wake,” na kubainisha kuwa “chama hicho ni vuguvugu kubwa ambalo haliwezi kuzimwa wala kumalizwa.” Akalitisha umbile la Kiyahudi kwa kusema: “Leo tuna nyinyi machoni mwetu, na tutapigana mpaka mwisho, na hatutakuruhusuni kudhibiti hatma ya Waislamu, na tutalipiza kisasi, nanyi mtapata pigo chungu, na lazima musubiri.”

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu