Kuihusu Hizb ut Tahrir: Kazi Yetu na Ruwaza Yetu
- Imepeperushwa katika Khilafah
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Hizb ut Tahrir [HT] ni chama cha kisiasa cha kilimwengu ambacho fikra yake ni Uislamu na lengo lake pekee ni kurejesha njia ya maisha ya Kiislamu kwa kuirejesha tena Khilafah. Tokea kuanzishwa kwake mnamo 1953, katika Al-Quds (Jerusalem), fikra yake na njia yake ya kufikia lengo hili zimechimbuka katika ufahamu wa ndani wa Uislamu, Aqida yake na nidhamu zake.



